Mara kadhaa watoa huduma za Afya hapa nchini wamekuwa wakishutumiwa kwa kutoa huduma chini ya matarajio ya wateja wao yaani clients. Inawezekana kabisa kukawa na ukweli katika hili au pengine ukweli huu unaongezwa chumvi sana. Ninashawishika kuweka mada hii katika JF kwa lengo la kutoa ushuhuda wa utendaji uliotukuka niliouona kutoka kwa wahudumu katika hospitali zetu za serikali hapa nchini.
Hivi karibuni nilipata mkasa ambapo mwanafamilia yangu alipata ajali ya moto nikalazimika kutafuta huduma katika hospitali za serikali hapa Jijini Dar es salaam. Nilikuwa na hofu endapo atapata huduma stahiki ukizingatia hali yake ilivyokuwa. Awali alipelekwa Hospitali ya Mkoa (jina linahifadhiwa) na kisha kupata rufaa katika Hospitali ya Taifa yaani Muhimbili National Hospital (MNH).
Nilichokishuhudia katika hospitali hizi mbili ni kitu cha ajabu ambacho sikufikiria kukutana nacho katika hospitali zetu. Ni kweli kuna changamoto za mazingira magumu sana ya kazi, ukosefu wa vitendea kazi pamoja na madawa lakini kipekee na mbele za Mungu aliye Hai ninapenda kutoa shukurani na pongezi nyingi kwa timu ya Madaktari vijana ambao kwa kweli wamejipanga vizuri hasa eneo la Casuality au Emergency pale MNH. Kwa macho yangu nilishuhudia upendo mkubwa na roho ya kizalendo waliokuwa nayo wale vijana. Wanajituma na pia wana lugha nzuri kwa wagonjwa. Vile vile wanaonekana wameenda madarasa vizuri. Pengine hili limewaongezea uelewa wa nini maana ya UHAI wa mtu kwamba ukitoka haurudi tena hivyo ni lazima upiganiwe kwa gharama zozote.
Nilishuhudia mtoto wa miaka kati ya 7 na 10 akiletwa kutoka mojawapo ya satellite hospitals akiwa na majeraha ya kuanguka mtini. Aliletwa na bibi yake na kwa haraka ilikuwa wazi kuwa wametoka katika familia yenye uchumi mgumu sana. Vipimo zaidi ya vitano (x-ray, damu, etc) vilihitajika kuchukuliwa ambapo wanandugu (bibi) alitakiwa kulipia. Kama nilivyosema awali, bibi hakuwa na uwezo wa kulipia hata shilingi mia, nilishangaa kuona vijana wale wanapitisha karatasi kwa ajili ya kuchangia huduma za vipimo. Walitoa kwa moyo wa upendo (hata kama mtu haamini hili lakini ndio ukweli), nilihisi kuguswa sana na uzalendo huu. Katika dunia ya leo aghalabu mara chache unaweza kushuhudia mambo haya yakitendeka. Nilijisikia furaha sana kutambua kuwa kuna wazalendo katika nchi hii wenye kuipenda nchi yao na watu wao licha ya mazingira magumu sana ya kazi.
Sina cha kuwalipeni enyi watoa huduma wa Emmergency Muhimbili zaidi ya kuwaombea kwa Mungu awajaze Baraka zake ziwafuate popote pale mtakapokuwa ninyi na vizazi vyenu. You showed me what it takes to be a Doctor/Nurse/Pharmacist and others in the Health Sector. Rai yangu kwa serikali ni kwamba watazameni kwa jicho la tatu watoa huduma hawa. Boresheni mazingira yao ya kazi, watatufanyia mengi mazuri. Zile fedha za ESCROW ziende huku jamani, wapeni hawa watusaidie sisi wenye nchi hii.
Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo na pia ALLAH kwa upande wa pili awabariki sana enyi Madaktari wa MNH.
BIG UP THE YOUNG DOCTORS AT MUHIMBILI CASUALITY; IM PROUD OF YOU GUYS.
Hivi karibuni nilipata mkasa ambapo mwanafamilia yangu alipata ajali ya moto nikalazimika kutafuta huduma katika hospitali za serikali hapa Jijini Dar es salaam. Nilikuwa na hofu endapo atapata huduma stahiki ukizingatia hali yake ilivyokuwa. Awali alipelekwa Hospitali ya Mkoa (jina linahifadhiwa) na kisha kupata rufaa katika Hospitali ya Taifa yaani Muhimbili National Hospital (MNH).
Nilichokishuhudia katika hospitali hizi mbili ni kitu cha ajabu ambacho sikufikiria kukutana nacho katika hospitali zetu. Ni kweli kuna changamoto za mazingira magumu sana ya kazi, ukosefu wa vitendea kazi pamoja na madawa lakini kipekee na mbele za Mungu aliye Hai ninapenda kutoa shukurani na pongezi nyingi kwa timu ya Madaktari vijana ambao kwa kweli wamejipanga vizuri hasa eneo la Casuality au Emergency pale MNH. Kwa macho yangu nilishuhudia upendo mkubwa na roho ya kizalendo waliokuwa nayo wale vijana. Wanajituma na pia wana lugha nzuri kwa wagonjwa. Vile vile wanaonekana wameenda madarasa vizuri. Pengine hili limewaongezea uelewa wa nini maana ya UHAI wa mtu kwamba ukitoka haurudi tena hivyo ni lazima upiganiwe kwa gharama zozote.
Nilishuhudia mtoto wa miaka kati ya 7 na 10 akiletwa kutoka mojawapo ya satellite hospitals akiwa na majeraha ya kuanguka mtini. Aliletwa na bibi yake na kwa haraka ilikuwa wazi kuwa wametoka katika familia yenye uchumi mgumu sana. Vipimo zaidi ya vitano (x-ray, damu, etc) vilihitajika kuchukuliwa ambapo wanandugu (bibi) alitakiwa kulipia. Kama nilivyosema awali, bibi hakuwa na uwezo wa kulipia hata shilingi mia, nilishangaa kuona vijana wale wanapitisha karatasi kwa ajili ya kuchangia huduma za vipimo. Walitoa kwa moyo wa upendo (hata kama mtu haamini hili lakini ndio ukweli), nilihisi kuguswa sana na uzalendo huu. Katika dunia ya leo aghalabu mara chache unaweza kushuhudia mambo haya yakitendeka. Nilijisikia furaha sana kutambua kuwa kuna wazalendo katika nchi hii wenye kuipenda nchi yao na watu wao licha ya mazingira magumu sana ya kazi.
Sina cha kuwalipeni enyi watoa huduma wa Emmergency Muhimbili zaidi ya kuwaombea kwa Mungu awajaze Baraka zake ziwafuate popote pale mtakapokuwa ninyi na vizazi vyenu. You showed me what it takes to be a Doctor/Nurse/Pharmacist and others in the Health Sector. Rai yangu kwa serikali ni kwamba watazameni kwa jicho la tatu watoa huduma hawa. Boresheni mazingira yao ya kazi, watatufanyia mengi mazuri. Zile fedha za ESCROW ziende huku jamani, wapeni hawa watusaidie sisi wenye nchi hii.
Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo na pia ALLAH kwa upande wa pili awabariki sana enyi Madaktari wa MNH.
BIG UP THE YOUNG DOCTORS AT MUHIMBILI CASUALITY; IM PROUD OF YOU GUYS.