Madaraka ni dhamana ya muda mfupi sana, kutoka kupigiwa magoti hadi kusindikizwa nje ya Ikulu

Madaraka ni dhamana ya muda mfupi sana, kutoka kupigiwa magoti hadi kusindikizwa nje ya Ikulu

Uchaguzi wao wa kwanza uliomuondoa baba wa taifa lao madarakani, walitumia katiba hiyo hiyo. Nahisi suala la katiba mpya Tanzania tunalipa sana promo, tatizo Tanzania sio katiba, tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe, sio katiba. Kama uliufatilia vizuri uchaguzi wa Zambia hu wa juzi, jamaa walitaka kuchakachua matokeo kama hapa kwetu, walifunga hadi mitandao ya simu kama ilivyo fanyika hapa kwetu, wananchi hawakukubali na kilichotokea ni historia, ndio huyo bwana Rungu anaondoka Ikulu bila escort. Tusisingizie katiba, sisi ndio sio
Ni muhimu kupata katiba mpya kwa sababu mambo yote kuhusu haki na miongozo mbalimbali itakuwemo , Masuala ya Ma DED kuwa wasimamizi wa uchaguzi yatafutiliwa mbali , ndani ya Katiba mpya mtaondoa makada wa ccm kuwa viongozi wa Tume ya uchaguzi
 
Wananchi wakiamua itawezekana lakiini historia ya upole wa watanzania ndiyo inayofanya mambo yawe yalivyo. Mambo ya kuudhi ni mengi lakini wanashindwa kuonesha kuwa hawajapendezwa nayo, ni kulalamika tu pasipo actions(vitendo) na hasa hao wa maisha ya chini zaidi. Huwaambii kitu kuhusu watawala, na huwasaidia pia kuwaweka madarakani kwani wao hasa ndiyo hupiga kura kuliko daraja la kati..
Watanzania sio wapole..ni bahati mbaya tu kwamba asilimia kubwa sana ni wanafiki na waoga. Binadamu wengi ambao wanahisiwa kuwa wapole sio wapole bali ni wanafiki au waoga. Na unafiki huzalishwa na uoga. Hakuna muoga asiyekuwa mnafiki na hakuna mnafiki asiyekuwa muoga...hata serikali inakabiliwa na tatizo hilo ...
 
Sasa mkuu 'denoo', kama wametapakaa kila sehemu, na ninakubaliana nawe juu ya hili, hiyo katiba mpya ambayo wao hawaipendi kabisa itapatikana kwa njia zipi bila ya wao kulazimishwa(kwa njia zipi?) ambazo njia hizo hizo pia zingeweza kuwaondoa kwenye madaraka!

Maoni yangu ni kwamba ni vyema, na sahihi kabisa tukiweza kutengeneza katiba mpya bila ya mashinikizo, lakini ukweli ni kwamba CCM hili hawalitaki kabisa. Lakini na kutolitaka kwao hakutazuia kamwe uwepo wa katiba mpya sasa, kwa sababu hawana uwezo tena wa kulizuia hili.

Sana sana, wanachoweza kufanya ni kukubali katiba mpya itengenezwe, na kwa wingi wao wavungevunge huko huko kwenye mchakato wa kuiandaa hiyo katiba ili wapate pa kujishikizia na kuendelea kushikilia madaraka, hata kama watakuwa wamedhoofishwa kuliko ilivyo sasa.

Katiba mpya haizuiliki tena. CCM wasipochukua tahadhari hili litawafyekea mbali.
Hakika .
 
Lakini nadhani mara nyingi unasahau tofauti kati ya hao na sisi (Tanzania).

Hapa kwetu ni CCM zaidi ya mtu huyo mmoja. Kuna akina Lungu wengi sana ndani ya CCM ambao wanahakikisha kuendelea kuwepo kwao kuna uhakika mradi CCM iendelee kuwepo.

Sasa tuna akina Pinda huko ndani ya CCMwanaohakikisha hilo. linaendelelea. Na kwa bahati mbaya sana, hawa hawaonekani mbele za macho ya wananchi. Wao wanafanya mambo yao kimya kimya huko huko ndani ya chama. Wanaamua nani awe mbele kuwasulubu waTanzania, huku wao wakiwa nyuma ya huyo msulubishaji, ambaye ndiye sisi sote tunadhani tukimwondoa tutapata nafuu, kumbe wapi.

Si umeona mwenyewe alivyoondoka Magufuli, nafuu sasa ipo wapi?
Ndio maana tunataka Katiba mpya ili hawa mamluki wanatufanya tuendelee kuumia wasipate upenyo
 
Uchaguzi wao wa kwanza uliomuondoa baba wa taifa lao madarakani, walitumia katiba hiyo hiyo. Nahisi suala la katiba mpya Tanzania tunalipa sana promo, tatizo Tanzania sio katiba, tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe, sio katiba. Kama uliufatilia vizuri uchaguzi wa Zambia hu wa juzi, jamaa walitaka kuchakachua matokeo kama hapa kwetu, walifunga hadi mitandao ya simu kama ilivyo fanyika hapa kwetu, wananchi hawakukubali na kilichotokea ni historia, ndio huyo bwana Rungu anaondoka Ikulu bila escort. Tusisingizie katiba, sisi ndio sio
Mkuu 'Mazindu Msambule', umeandika vizuri sana, lakini umesahau kitu kinachotutofautisha sisi Tanzania, na hao wengine.
CCM, CCM, CCM..., ipo kila mahali, mahakamani, Bungeni, Jeshini, Usalama (wa CCM), Tume ya Uchaguzi, Mitaani tunakoishi, kila mtaa kuna CCM inayohakikisha ni wao tu ndio wenye kuamua kila kitu.

Katiba yetu ilivyo, mtu wa CCM ambaye ni Mwenyekiti na rais wa nchi, yupo juu ya katiba hiyo, anaamua kama 'mungu' hatma ya waTanzania wote.

Mimi sijui kama huko Zambia na kwenyewe kuliwahi kuwepo chama chenye muundo kama wa CCM kikiambatana na Katiba kama tuliyonayo sisi.
 
Naomba nikustushe/kukumbushe.

Uliwahi kumsoma mtu anayejulikana kwa jina la 'Iboya' hapa JF?

Hii ndiyo timu mpya na mambo mapya!

Hebu angalia #9 hapo juu.
ni miongoni mwa watu duni niliowapuuza kabisa hapa jf , kwanza siamini kama ana ubongo
 
Kuna mwingine hapa walianza kumwita hadi Mungu... huku yeye alichekelea.
 
Uchaguzi wao wa kwanza uliomuondoa baba wa taifa lao madarakani, walitumia katiba hiyo hiyo. Nahisi suala la katiba mpya Tanzania tunalipa sana promo, tatizo Tanzania sio katiba, tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe, sio katiba. Kama uliufatilia vizuri uchaguzi wa Zambia hu wa juzi, jamaa walitaka kuchakachua matokeo kama hapa kwetu, walifunga hadi mitandao ya simu kama ilivyo fanyika hapa kwetu, wananchi hawakukubali na kilichotokea ni historia, ndio huyo bwana Rungu anaondoka Ikulu bila escort. Tusisingizie katiba, sisi ndio sio
Nakubaliana na wewe. Na viongozi wa CCM walishauona huu udhaifu ndiyo maana hawaogopi. Uchaguzi wa 2020 ulivyokuwa wa hovyo na ujambazi wa wazi, ingekuwa nchi nyingine Magufuli asingefia madarakani. Ila katiba ikiandikwa upya na izibe loopholes za wizi wa kura kadiri iwezekenavyo, mambo yanaweza kubadilika. Tatizo ni kuwa CCM hawatakubali kwa sababu wanajua itawaweka kwenye wakati mgumu.
 
Uchaguzi wao wa kwanza uliomuondoa baba wa taifa lao madarakani, walitumia katiba hiyo hiyo. Nahisi suala la katiba mpya Tanzania tunalipa sana promo, tatizo Tanzania sio katiba, tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe, sio katiba. Kama uliufatilia vizuri uchaguzi wa Zambia hu wa juzi, jamaa walitaka kuchakachua matokeo kama hapa kwetu, walifunga hadi mitandao ya simu kama ilivyo fanyika hapa kwetu, wananchi hawakukubali na kilichotokea ni historia, ndio huyo bwana Rungu anaondoka Ikulu bila escort. Tusisingizie katiba, sisi ndio sio
Bro you speak it....that fact! watanzania hawajajua tatizo ni sisi wenyewe
 
Uchaguzi wao wa kwanza uliomuondoa baba wa taifa lao madarakani, walitumia katiba hiyo hiyo. Nahisi suala la katiba mpya Tanzania tunalipa sana promo, tatizo Tanzania sio katiba, tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe, sio katiba. Kama uliufatilia vizuri uchaguzi wa Zambia hu wa juzi, jamaa walitaka kuchakachua matokeo kama hapa kwetu, walifunga hadi mitandao ya simu kama ilivyo fanyika hapa kwetu, wananchi hawakukubali na kilichotokea ni historia, ndio huyo bwana Rungu anaondoka Ikulu bila escort. Tusisingizie katiba, sisi ndio sio
Acha kudanganya katiba Zambia ilibadikishwa kabla Kaunda hajatoka madarakani!
 
Ni muhimu kupata katiba mpya kwa sababu mambo yote kuhusu haki na miongozo mbalimbali itakuwemo , Masuala ya Ma DED kuwa wasimamizi wa uchaguzi yatafutiliwa mbali , ndani ya Katiba mpya mtaondoa makada wa ccm kuwa viongozi wa Tume ya uchaguzi
tume ya uchaguzi inafumuliwa inaundwa upya vipi bado unataka katiba mpya?
 
tume ya uchaguzi inafumuliwa inaundwa upya vipi bado unataka katiba mpya?
Katiba Mpya ndio msingi wa Haki , kuna mambo ya kijinga ndani ya katiba ni lazima yaandikwe upya hata hii tume ya uchaguzi ipo kwa sababu ya katiba yenu mbovu , Mahera au Jecha wanaccm wasiojificha ni aibu kuongoza tume ya uchaguzi
 
Katiba Mpya ndio msingi wa Haki , kuna mambo ya kijinga ndani ya katiba ni lazima yaandikwe upya hata hii tume ya uchaguzi ipo kwa sababu ya katiba yenu mbovu , Mahera au Jecha wanaccm wasiojificha ni aibu kuongoza tume ya uchaguzi
nyie kinajulikana mnachotaka kibadirishwe hapo ni kwenye tume tu yaani hayo mengine wala hivi ukiulizwa sehemu gani nyingine unataka ibadirishwe utasema ni wapi? inawezekana hata katiba yenyewe huijui vizuri mnauchu wa madaraka sana mbona ya kwenu mmeshindwa kuiboresha mpaka mwenyekiti anajiamria aondoke lini kwenye madaraka? hilo hamlioni? hamna huruma na raia wa tanzania mna uchu wa madaraka
 
nyie kinajulikana mnachotaka kibadirishwe hapo ni kwenye tume tu yaani hayo mengine wala hivi ukiulizwa sehemu gani nyingine unataka ibadirishwe utasema ni wapi? inawezekana hata katiba yenyewe huijui vizuri mnauchu wa madaraka sana mbona ya kwenu mmeshindwa kuiboresha mpaka mwenyekiti anajiamria aondoke lini kwenye madaraka? hilo hamlioni? hamna huruma na raia wa tanzania mna uchu wa madaraka
Tunataka serikali tatu; serikali ya Tanganyika, serikali ya Zanzibar na serikali ya Muungano. Tunataka viti maalum vifutwe, tunataka madaraka ya Rais yapunguzwe na aweze kushtakiwa akivunja katiba na mengine mengi.
 
Rais wa zamani wa Zambia Edgar Lungu anatajwa kuwa miongoni mwa viongozi wa kiafrika waliopenda kuabudiwa , ilifikia hadi Mawaziri kumpigia Magoti .

View attachment 1909417

Picha ya Chini akisindikizwa kuondoka Ikulu baada ya kukataliwa na wananchi kwenye sanduku la kura

View attachment 1909418

Kwenye maisha ya kila siku tunapaswa kuheshimiana na kuthaminiana .
Huyo sio Haichelema alikuepo ni waziri mwingine wa Edgar Lungu...
 
Back
Top Bottom