Sasa mkuu 'denoo', kama wametapakaa kila sehemu, na ninakubaliana nawe juu ya hili, hiyo katiba mpya ambayo wao hawaipendi kabisa itapatikana kwa njia zipi bila ya wao kulazimishwa(kwa njia zipi?) ambazo njia hizo hizo pia zingeweza kuwaondoa kwenye madaraka!
Maoni yangu ni kwamba ni vyema, na sahihi kabisa tukiweza kutengeneza katiba mpya bila ya mashinikizo, lakini ukweli ni kwamba CCM hili hawalitaki kabisa. Lakini na kutolitaka kwao hakutazuia kamwe uwepo wa katiba mpya sasa, kwa sababu hawana uwezo tena wa kulizuia hili.
Sana sana, wanachoweza kufanya ni kukubali katiba mpya itengenezwe, na kwa wingi wao wavungevunge huko huko kwenye mchakato wa kuiandaa hiyo katiba ili wapate pa kujishikizia na kuendelea kushikilia madaraka, hata kama watakuwa wamedhoofishwa kuliko ilivyo sasa.
Katiba mpya haizuiliki tena. CCM wasipochukua tahadhari hili litawafyekea mbali.