Hii porojo ya kuwa zinafanyiwa utafiti na zinatokana na mimea imekuwa ikitumika muda mrefu kunadi mfumo wa kisasa wa tiba za viwandani, ambazo ni biashara zaidi kuliko tiba na mbaya ni kuwa zinatokana na kemikali kwa kiasi kikubwa na zina madhara mengi ya ziada kwa watumiaji.
Mimi si mtafiti, lakini takwimu chache zinaonesha kuwa kiwango cha vifo vya uzazi kimeongezeka huku Afrika kweusi baada ya kununua propaganda za biashara ya tiba kutoka kwa Wazungu, miaka inavyoenda pia, licha ya kukua kwa teknolojia ya madawa na vifaa tiba bado kiwango cha maisha kinapungua kwa kiasi kikubwa sana, kwanini?
Mataifa kama China na Japan, Serikali zao zimewekeza kwenye tiba za asili kwa teknolojia ya kisasa na nadhani ndizo nchi zenye watu wanaoishi muda mrefu.
Sisi tunacho kitengo cha tiba asili pale Muhimbili, lakini kinadumazwa kwa makusudi ili biashara ya madawa ya viwanda vya nchi za mabepari izidi kusitawi (na tuendelee kufa). Wewe ni shuhuda, kwa umri wako huu umeshuhudia tiba elekezi ya Malaria ikibadilika kila baada ya miaka kadhaa kwa sababu tofauti, unadhani ni kwanini?
Unadhani hawajui kuwa aloe vera, mbegu za jamii ya machungwa, mbegu za papai, shubiri, muarobaini na mimea lukuki inatibu Maleria kwa ufanisi wa asilimia mia na bila kuacha madhara mengine?
Ni vigumu na inataka akili ngumu kuwaamini watu wale wale waliodhamiria kukuua kwa madawa na sumu waje wakupe tiba sahihi. Teh!
#RevolutionWillNotBeTelevised