Madeleka aitupia lawama mahakama kesi ya Afande Fatma Kigondo anayekabiliwa na tuhuma za kuratibu ubakaji wa "Binti wa Yombo"

Madeleka aitupia lawama mahakama kesi ya Afande Fatma Kigondo anayekabiliwa na tuhuma za kuratibu ubakaji wa "Binti wa Yombo"

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Anayetajwa kuwa Afisa wa Jeshi la Polisi, Fatma Kigondo, amejikuta akihusishwa na tuhuma nzito za kuratibu tukio la ubakaji wa kundi na ulawiti wa binti anayeishi Yombo Dovya, Dar es Salaam.

Tuhuma hizo zinamweleza kuwa aliwatuma vijana wanne, akiwemo askari wa vyombo vya usalama, kutenda uhalifu huo mnamo Mei 2024 jijini Dodoma.
1728294852419.png
Kesi hiyo, iliyofunguliwa na wakili Paul Kisabo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Dodoma, inaendelea kusikilizwa tarehe 7 Oktoba 2024, baada ya kuahirishwa mnamo Septemba kutokana na uhamisho wa wakili aliyekuwa akisimamia, Francis Kisenyi.

Wakili Peter Madeleka, ambaye pia ni sehemu ya kesi hiyo, amesema kwamba kutokana na uzito wa tuhuma zinazomkabili Afisa Fatma, anapaswa kuwekwa gerezani akisubiri hukumu.

Madeleka amesisitiza kuwa sheria inapaswa kuchukua mkondo wake ili kuhakikisha haki inatendeka kwa mlalamikaji, ambaye amedai kukumbana na madhila makubwa.


 
Ni haki yake ya kikatiba kuhifadhiwa gerezani kama P diddy ili kulinda usalama wake
 
Madeleka ashakula million sabini alizochangiwa na wananchi kwaajiri ya hii kesi
 
Madeleka ni mtu wa mfumo kesi tata anapewa yeye baadae ziishe kimyakimya
 
M
Anayetajwa kuwa Afisa wa Jeshi la Polisi, Fatma Kigondo, amejikuta akihusishwa na tuhuma nzito za kuratibu tukio la ubakaji wa kundi na ulawiti wa binti anayeishi Yombo Dovya, Dar es Salaam.

Tuhuma hizo zinamweleza kuwa aliwatuma vijana wanne, akiwemo askari wa vyombo vya usalama, kutenda uhalifu huo mnamo Mei 2024 jijini Dodoma.
Kesi hiyo, iliyofunguliwa na wakili Paul Kisabo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Dodoma, inaendelea kusikilizwa tarehe 7 Oktoba 2024, baada ya kuahirishwa mnamo Septemba kutokana na uhamisho wa wakili aliyekuwa akisimamia, Francis Kisenyi.

Wakili Peter Madeleka, ambaye pia ni sehemu ya kesi hiyo, amesema kwamba kutokana na uzito wa tuhuma zinazomkabili Afisa Fatma, anapaswa kuwekwa gerezani akisubiri hukumu.

Madeleka amesisitiza kuwa sheria inapaswa kuchukua mkondo wake ili kuhakikisha haki inatendeka kwa mlalamikaji, ambaye amedai kukumbana na madhila makubwa.

View attachment 3117713
Maskini mijishangazi, tu toto twa 2000 wamewafunika kila upande.
 
Huyu mama mumewe alishafariki siku nyingi tena alikuwa Polisi mkubwa tu.
Huyu mama ana kibenten chake na ndicho alikuwa akikiilia WIVU hadi kufikia kuratibu huu unyama!
Analindwa na mkubwa flani ambae mumewe alimlelea sana huko "kazini"
 
Back
Top Bottom