Madeni ya Taifa: Kuna kitu very serious CAG amekisema. Hii kitu haiko sawa. Je, tunakwenda wapi?

Madeni ya Taifa: Kuna kitu very serious CAG amekisema. Hii kitu haiko sawa. Je, tunakwenda wapi?

Mkuu Petro E. Mselewa, kwanza asante kwa bandiko hili Ripoti ya CAG: Bunge limehitimisha mjadala leo, nini kitafuata? Waliohusika na ufisadi na ubadhirifu watafanywaje?
Very objective, mimi msimamo wangu kuhusu Bunge letu, kwenye hoja ya bunge kuisimamia serikali, bado haujabadilika ni ule ule wa bunge lililopita Wabunge Wetu wa Ajabu!, Wanaachaje Bunge Lijipendekeze Kwa Serikali!, Wanajua Wajibu Wao?. Check 'n' Balance Itoke Wapi?
Na hapa Je, Bunge letu ni Bunge Butu?. Angalia Bunge la Uingereza lenye meno linavyong'ata Serikali. Je, Kuna ubaya tukiiga?
Japo Rais Samia ametoa maelekezo makali kwa maofisa masuhuli, hii ni kesi ya nyani kumpelekea ngedere!.
Kilichopaswa kufanywa on the first place ni kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG, alipaswa apishe kwanza, akiwa cleared ndipo arudishwe!.
P
Raid Samia yuko sahihi.

Baada ya CAG kuwasilisha ripoti yake kwa Bungeni hatua zinazofuata ni kama ifuatavyo;

1. Ripoti hiyo hujadiliwa na kamati husika za Bunge kama vile Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).

2. Kamati hizo husikiliza na ufafanuzi kutoka kwa viongozi au taasisi za serikali ambao zimeorodheshwa kwenye ripoti ya CAG ili kueleza kuhusu masuala yaliyoibuliwa katika ripoti hiyo ya CAG.

3. Kamati hizo hutengeneza ripoti yao ya maoni kuhusu ripoti ya CAG na huwasilisha kwa Bunge kwa ajili ya majadiliano na kupitishwa.

4. Bunge hupitia ripoti ya kamati na kuamua hatua stahiki za kuchukua, kama vile kutoa maagizo kwa serikali, kuwajibisha watendaji waliohusika na matumizi mabaya ya fedha za umma, au kufanya marekebisho ya sheria na kanuni.

5. Serikali huchukua hatua stahiki kulingana na maagizo ya Bunge na kuhakikisha kuwa utekelezaji wake unafuatiliwa na CAG kuhakikisha uwajibikaji na uwazi katika matumizi ya fedha za umma nchini Tanzania.

Ni muhimu kujua ripoti ya CAG inapaswa kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria na sio mihemko kwani CAG hukagua kwa njia mbali mbali ikiwemo kukagua nyaraka.

Kazi za CAG nchini Tanzania zinasimamiwa na Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na. 11 ya mwaka 2008. Sheria hii inatoa mamlaka kwa CAG kufanya ukaguzi wa hesabu za umma kwa niaba ya Bunge na kuwasilisha ripoti kwa Rais, Spika wa Bunge,bunge, Kamati za PAC na LAAC, na kwa umma kwa ujumla.
 
Wanabodi,

Tanzania ni nchi yetu sote na sio mali ya mtu na inaendeshwa kwa msingi mkuu wa katiba kwa mujibu wa sheria, taratibu kanuni, haiwezekani jambo lililopitishwa na Bunge kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, halafu lisitekelezwe kama sheria ilivyoelekeza, halafu wakati huo huo kuna jambo jingine ambalo halijajadiliwa na Bunge, halijatengewa budget na serikali, hivyo halijaombewa hiyo budget, ikatengwa, ikawasilishwa Bungeni, ikajadiliwa, ikapitishwa, lakini likaibuka from nowhere jambo jingine kubwa linalohitaji fedha ndefu, ambalo sio la dharura, likajiibukia tuu from nowhere, budget yake haijatengwa popote, haijaombwa popote, lakini kwa vile fedha zimo ndani ya chungu chetu, kwenye hazina yetu, ukapitishwa uamuzi, fedha hizo zichotwe bila idhini ya Bunge, na jambo hilo likatekelezwa na huku tunamtazama mzigo wa madeni chachefu na hatarishi ya muda mrefu na hayajalipwa!. Jee jambo hili jipya limetekelezwa kwa fedha kutoka votes gani, iliyoidhinishwa na nani na kwa mamlaka gani, au sheria ipi?!.

Naomba umsikilize kwa makini hapa, CAG, Prof. Mussa Assad kuna kitu very very serious anakizungumza kupitia Habari ya Channel Ten.

Nimefarijika sana hiki kichwa kinaingia tena kazini this time, kumsaidia Mama.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tarehe 29 Julai, 2024 wakati wa Mkutano wa 15 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alitangaza uamuzi wa Serikali kuunda kamati ya kutathmini na kushauri kuhusu masuala ya kodi nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Mhe. Rais ameunda Tume ya Rais ya Kutathmini na Kushauri kuhusu Masuala ya Kodi (Presidential Commission on Tax Reforms) na kumteua Balozi Ombeni Yohana Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo. Aidha, wajumbe wa Tume walioteuliwa ni kama ifuatavyo:

i. Prof. Florens Luoga - Aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT) na Profesa Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam;

ii. Prof. Mussa Juma Assad Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Profesa Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; Bw. Leonard Mususa - Aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa PricewaterhouseCoopers (PwC) Tanzania;

iv. CPA. Aboubakar Mohamed Aboubakar Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU);

V. Balozi Mwanaidi Sinare Maajar - Mshauri wa Masuala ya Sheria;

vi. Bw. David Tarimo - Mtaalam na Mshauri wa Masuala ya Kodi na aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Ushauri wa Kodi, PwC;

vii. Balozi Maimuna Kibenga Tarishi - Katibu Mkuu Mstaafu; na

viii. Bw. Rished Bade Kamishna wa Fedha za Nje, Wizara ya Fedha na aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

View attachment 3057904
Nina imani na hii Tume kwasababu baadhi ya wajumbe wake nawafahamu kwa karibu ni watu niliofanya nao kazi, naelewa uwezo wao, uimara wao na uadilifu wao, watu wa type hii, ndio wanamsaidia Samia kwa kumwambia ukweli na sio wasaidizi wake uchumi wakiongozwa na msaidizi mkuu wa uchumi, the chancellor of exchequer ambaye ni chawa, atamsaidia nini Samia na kuisaidia nchi!
Juzi kati niliandika humu na magazetini Wasaidizi wa Magufuli walimuogopa hadi kushindwa kumsaidia, Je Wasaidizi wa Samia wanamsaidia kwa kumweleza ukweli au nao wanamuogopa? Tumsaidie au..? hiki kikosi kazi kitamsaidia ila Mama nae akubali kuambiwa ukweli na afuate ushauri.

Kile kikosi kazi cha siasa jilijazwa machawa na badala ya kumsaidia ndio kwanza kimeyarudia Madudu yale yale!.
Nina imani sana na Prof. Assad, nimeisha zungunza nae sana na haya ni baadhi ya kauli zake
Huyu ataisaidia sana hii Tume na atamsaidia sana Samia kwa kumweleza ukweli.
P
 
Nimefarijika sana hiki kichwa kinaingia tena kazini this time, kumsaidia Mama.
Nina imani na hii Tume kwasababu baadhi ya wajumbe wake nawafahamu kwa karibu ni watu niliofanya nao kazi, naelewa uwezo wao, uimara wao na uadilifu wao, watu wa type hii, ndio wanamsaidia Samia kwa kumwambia ukweli na sio wasaidizi wake uchumi wakiongozwa na msaidizi mkuu wa uchumi, the chancellor of exchequer ambaye ni chawa, atamsaidia nini Samia na kuisaidia nchi!
Juzi kati niliandika humu na magazetini Wasaidizi wa Magufuli walimuogopa hadi kushindwa kumsaidia, Je Wasaidizi wa Samia wanamsaidia kwa kumweleza ukweli au nao wanamuogopa? Tumsaidie au..? hiki kikosi kazi kitamsaidia ila Mama nae akubali kuambiwa ukweli na afuate ushauri.

Kile kikosi kazi cha siasa jilijazwa machawa na badala ya kumsaidia ndio kwanza kimeyarudia Madudu yale yale!.
Nina imani sana na Prof. Assad, nimeisha zungunza nae sana na haya ni baadhi ya kauli zake
Huyu ataisaidia sana hii Tume na atamsaidia sana Samia kwa kumweleza ukweli.
P
Kaka Pascal nikupongeze kwa maandiko yako yenye manufaa. Shida ya watawala wetu ni moja, utashi wa kutekeleza mapendekezo. Zinaandikwa ripoti nyingi na zinatoa mapendekezo mengi mazuri. Ila serikali haina political will ya kutekeleza mapendekezo/maboresho hayo ya tume. Toka enzi za Mkapa na tume za Jaji Francis Nyalali (marekshisho ya sheria mbovumbovu), tume ya Jaji Kisanga, tume ya Jaji Warioba na tume zingine kibao. Hizi tume huwa zinaandika taarifa nzuri sana na kuainisha mapungufu yanayotakiwa kufanyiwa kazi, lakini serikali haina utashi wa kutekeleza maboresho hayo. Hata tume ije na mapendekezo mazuri kiasi gani, serikali huwa haitekelezi.
 
uwezo wao, uimara wao na uadilifu wao, watu wa type hii, ndio wanamsaidia Samia kwa kumwambia ukweli na sio wasaidizi wake uchumi wakiongozwa na msaidizi mkuu wa uchumi, the chancellor of exchequer ambaye ni chawa, atamsaidia nini Samia na kuisaidia nchi!
Acha kuchafua watu...
 
Back
Top Bottom