Madereva Watanzania 51 wakutwa na maambukizi mpakani mwa Kenya na Tanzania. Visa vya Coronavirus Kenya vyafikia 912

Madereva Watanzania 51 wakutwa na maambukizi mpakani mwa Kenya na Tanzania. Visa vya Coronavirus Kenya vyafikia 912

Mambo mengi ni uongo tu nyie nae..kwanza mleta mada huyu nishaanza kumsitukia siku hizi atakua ni mKenya au ni kati ya wale waliobanwa na JPM kwa kula hela za wananchi..hatujapata Corona kwenye mabasi na minada waje wapate madereva wa maroli ilihali dereva anasafiri akiwa peke yake au na tingo wake tu,vitu vingine ni vya kushughulisha akili tu. mbona Maralia hamuisemi ilihali inaishi Afrika hapa miaka nenda rudi na inaua.
If we keep acting normally
This disease will act Abnormally

Kama unashindwa kuzuia waliopata ugonjwa wasisambae Tanzania unatagemea nini kifuatacho?
Hiyo ni sample ya Truck drivers tu
Think BIG

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Rate
Mambo mengi ni uongo tu nyie nae..kwanza mleta mada huyu nishaanza kumsitukia siku hizi atakua ni mKenya au ni kati ya wale waliobanwa na JPM kwa kula hela za wananchi..hatujapata Corona kwenye mabasi na minada waje wapate madereva wa maroli ilihali dereva anasafiri akiwa peke yake au na tingo wake tu,vitu vingine ni vya kushughulisha akili tu. mbona Maralia hamuisemi ilihali inaishi Afrika hapa miaka nenda rudi na inaua.

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
Rate of death due to Malaria inafanana na rate of death due to COVID19??
 
Mambo mengi ni uongo tu nyie nae..kwanza mleta mada huyu nishaanza kumsitukia siku hizi atakua ni mKenya au ni kati ya wale waliobanwa na JPM kwa kula hela za wananchi..hatujapata Corona kwenye mabasi na minada waje wapate madereva wa maroli ilihali dereva anasafiri akiwa peke yake au na tingo wake tu,vitu vingine ni vya kushughulisha akili tu. mbona Maralia hamuisemi ilihali inaishi Afrika hapa miaka nenda rudi na inaua.

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
Siwatetei wakenya. Nikiangalia ulichoandika. Hata ugonwja wenyewe wa covid huufaham vizuri.
Ukiupata sio kuwa unaanguka na kufa hapo hapo..
Huchukua siku 14 kuja kuonekana.
Ktk hizo siku 14 muhusika haonyehi dalili zozote zile..
Na anaweza alafanya kazi zake kawaida.. ila baada ya siku 14 muhusika ataona dalili kwenye mwili wake.

Corona huwez ipata kwa kupima joto au unaangalia n macho. So hoja yako ni weak sana.
Nchini kwetu hata contact tracing ni ishu kufanya.. maabara zimesimama kupima.. ww utajauaje kama mtu anao ama lah?

Malaria na corona vitu viwili tofauti. Corona unangolea virus.. malaria sio virus. Ni plusmodium.
And sio aggressive kama corona. Mpaka mbu ahusike.
Corona akuna cha mbu.m mgusuano tu tayari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama upimaji ni uleule unaolalamikiwa hata mpimaji akipimwa atakutwa +ve tu.

Huo siyo upimaji ni usambazaji wa virus kwa makusudi.
 
Kumbe bado wanang'ang'ania kuingia nchini Kenya? Tena kabla ya kukubaliwa kuingia lazima wapanue midomo yao hadi jino la mwisho lionekane ili wahudumu wa afya waweze kuokota sampuli. Kuna uzi humu ambao unadai kwamba wana mpango wa kusitisha usafirishaji wa bidhaa kuingia nchini Kenya. Vipi joto la jiwe, DC wa Longido amelegeza kamba au ni wenye bidhaa ndio wanataka hela liwe liwalo?

Nimecheka sana hapa...
Bila Kenya sijui wataishi vipi hawa, yaani bado wanang'ang'ania....
 
Wanatumika na MABEBERU ili kuichafua Tanzania duniani 🤣🤣🤣🤣🤣

Kenya wana chuki na sisi, kwanza corona Tz imeisha hata shule zinafunguliwa may be this week!🤣🤣🤣🤣🤣
 
Wanachojua wao ni KUKOMOANA tu wakati Kenyatta analinda raia wake kwa kuhakikisha madereva wote wa mizigo wanaoingia Nchini mwao hawana COVID. Leo tu madereva 51 kutoka Tanzania wamekutwa na COVID, halafu tunaambiwa corona imepungua Nchini. 😳

🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 nao ni mabeberu weusi. wamefunga mpaka wa Holoholo
 
Nimecheka sana hapa...
Bila Kenya sijui wataishi vipi hawa, yaani bado wanang'ang'ania....
Ubabe wao wote unaishia pale OSBP Namanga, sio shughuli ya mzaha mzaha jombaa. No retreat, no surrender! Hapiti mtanzania pale kabla maafisa wa GOK-MOH hawajaona jino lake la 42. [emoji1]
BB142a0T.img
 
Huu ni utapeli wa Kenya. Haiwezekani kila siku madereva wa Tanzania na Burundi wawe positive lakini hatusikii wakipima wa Rwanda wala Uganda. Inaonekna Kenya inalazimisha business subortage kwa Tanzania. Sasa ni wakati wa kuwajibu.
 
Wananchi wa Kenya wanamlaani sana Rais wao wanaomba hata tubadilishane na viongozi wao wa juu wote tuwape Magufuli wetu!! Chuki zao hazisaidii wao wanawaza kupiga hela za IMF na Mikopo ya Corona ya World Bank ambayo haimfikii mwananchi wa chini zaidi ya kumpima tu na kumfungia ndani na kutuma idadi kwa mabwana wakubwa wao wawape hela zingine huku walala hoi wakifa kwa njaa!! Mungu anawaona kwa kweli

Kapitie #UKAIDI WA MAGUFULI ndo ujue kiasi wanamuona raisi wetu
 
Tunafanya kosa kubwa sana kuvaa mask na kuhangaika kupita kiasi kujilinda na corona. Corona ni virus ambao hawawezi kuingia kirahisi kwenye mwili wa mtu mwenye kinga madhubuti, na vitu vinavyosaidia kubomoa kinga mwili ni pamoja na hofu na kupungukiwa kiasi cha oksjeni mwilini. Inasikitisha kwamba wataalam wetu wamelala kuelimisha watu juu ya kupandisha kinga ya mwili kupitia Chakula na tumaini yaani kuondoa hofu ambapo Raisi was Tanzania amekuwa akifanya siku zote. Muda unaongea, Corona ni ugonjwa mdogo sana.
 
Je? Wajua kwamba hata kushika hela ikiwa na corona unaambukizwa? Na, je? Wajua mwili wetu unatengeneza kinga/askari wenyewe? Inawezekana miili ya watanzania imejenga kinga dhidi ya corona virus, na mwishowe ugonjwa utaonekana wa kawaida sana baada ya muda. Njia anayotumia Raisi Magufuli kujikinga na Corona is the best ever in the World. Inawezekana Raisi anajua hilo na ndiyo maana anasema tupige Kazi.
 
Safi sana, pima wote wanaong'ang'ania kuingia Kenya, ingekua hawa Watanzania ndio wanapima Wakenya na kugundua wengi kiasi hiki sasa hivi wangekua wanalialia eti Kenya ina ajenda ya kuwaambukiza, yaani juzi waligunduliwa 78 wote kwa siku moja, leo 51 yaani wanataka kuja mamia yao wakiwa na kirusi, kama vipi maafisa waongezwe kwenye huo mpaka, hawa watatumaliza.

Niliskliza hotuba ya mkulu wao nikachoka, eti anadai dereva hana haja ya kupimwa kisa kaendesha lori mwenyewe kilomita zaidi ya 1,000. Ukweli rais Magufuli kuna mambo anafanya mazuri ila kuna maneno humtoka mpaka unasshindwa kweli kama alihudhuria darasa hata moja la sayansi, au labda ana washauri wabovu sana kuwahi kutokea.

Wataalam wameeleza jinsi hiki kirusi kinaambukiza na kusambaa, uwezekano upo mkubwa kwa dereva kuendesha lori kilomita zote hizo bila kugundua, maana kawaida wengi husafiri kama siku nne au tano, ila kirusi hadi kijitokeze vizuri kinahitaji siku kama kumi hivi, sasa mheshimiwa rais anataka mamia ya madereva wake walioathirika waachiwe waingie kwenye mataifa majirani kisa wamejiendeshea malori wenyewe.

Hotuba zake zimejaa kejeli dhidi ya mataifa ambayo yamechukua hatua za tahadhari, halafu watu wanahoji kwanini Tanzania inatengwa na SADC na EAC, maana hivi kwa kweli wakikutana marais wote wanajadili mikakati halaafu mmoja wao hana mikakati zaidi ya kukejeli wenzake, ni dhahiri hawataendana, hapa inabidi Watanzania wafungiwe wabaki huk huko kwao watajuana wenyewe, wakujifia atajifia na wa kupona atapona. Yeyote kati yao anayetaka kuvuka mpaka apimwe tena sana na kuhakikisha yuko salama, au raia yeyote anayetokea Tanzania hata iwe mtalii, mzungu, Mchina wote wapimwe mara mbili mbili na hata ikitokea hawana, zchukuliwe namba zao za simu na wenyeji wao, na wapi wanakwenda, wafuatiliwe huko hadi ziishe siku 14.
Nyie wanafiki mtu akipimwa kenya vipimo vinasema ana korona akija kupima tanzania anakutwa hana alafu mbona hamtaki kufuata takwimu alizotoa rais jana kuwa maambukizi yameshuka sana tanzania
 
Back
Top Bottom