MADHARA YA HARUFU MBAYA

kilambimkwidu

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2017
Posts
6,097
Reaction score
7,199
Wakuu,
Baada ya hustle za muda mrefu nmepata kaz kwenye kampuni ya usafi. Kaz yangu ni utingo kwenye gari la maji-taka Tabora mjini.

Kaz sio mbaya kimaslah ya fedha lkn nafanya kaz kwenye mazingira ya harufu kali mno. Juzi tulikua na kazi kwenye nyumba ya waarabu flan huku Kanyenye, daaah ile harufu ilinizidia ikabidi niruhusiwe nikalale chini ya mti nipigwe upepo maana nguvu ziliniishia nikaanguka na mpira wa kunyonyea.

Mazingira ya kaz ni salama kwakua tunazo protective gears ili kutuepusha na contamination za sewage. Tatizo ni harufu, haizuiliki aise.

Je naweza kupata madhara gan kwa kunusa harufu mbaya?

Kilambimkwidu
 
Juzi tulikua na kazi kwenye nyumba ya waarabu flan huku Kanyenye, daaah ile harufu ilinizidia ikabidi niruhusiwe nikalale chini ya mti nipigwe upepo maana nguvu ziliniishia nikaanguka na mpira wa kunyonyea.

HAPO UMEUA MKUU POLE SANA
 
Hyo kazi huwa ni nzur lakn harufu mbaya huwa inadumaza akili,fanya utafiti kwenye hilo
Akili huwa inadumaa kwa kuwa Mara nyingi inakosa oxygen ya kutosha,cuz ili akili ifanye kazi vzr inahtaji pure oxygen ya kutosha!
 
Kiongozi, nimependa sana intro yako. Inaonekana wewe ni mkweli sana. Wachache sana hapa JF wanaweza kuandika kazi wanayoifanya, inayorandana na ya kwako.

Harufu kama harufu haina shida. Mungu aliumba harufu mbaya ili binadamu ajue hicho sio kitu kizuri na kina madhara.

Tatizo la harufu linakuja kama hiyo harufu imeambatana na gesi. Gesi nyingi zinaweza kusababisha kutokupumua vizuri au kunyima baadhi ya viungo vyako oxygen.
 
Madhara yako ila ni ya mda mrefu saana maana mwili unatakiwa kupokea hewa safi kwa hiyo faya kazi ukiona umebanwa pumzi toka nje ili mapafu yapate hewa safi. Na unaweza kuumwa kichwa mara kwa mara jitaidi kunywa maji mengi baada ya kazi yako kuondoa kwa haraka hewa chafu
 
Hyo kazi huwa ni nzur lakn harufu mbaya huwa inadumaza akili,fanya utafiti kwenye hilo
Akili huwa inadumaa kwa kuwa Mara nyingi inakosa oxygen ya kutosha,cuz ili akili ifanye kazi vzr inahtaji pure oxygen ya kutosha!
Hapa pana ukweli mkuu,nawafahamu vijana wawili wakifanya kazi ktk lorry za kuzoa taka hapa K/koo na mitaa yake,mwanzo walikuwa vizuri tu ila kadiri miaka ilivyokuwa inasogea wakaanza kufanya vitu vya ajabu...nadhan kazi ni kazi ila kazi kama hii inatakiwa isiwe permanently iwe ni ya kuzugia tu kwa afya ya mfanyaji!
 
 
Hyo kazi huwa ni nzur lakn harufu mbaya huwa inadumaza akili,fanya utafiti kwenye hilo
Akili huwa inadumaa kwa kuwa Mara nyingi inakosa oxygen ya kutosha,cuz ili akili ifanye kazi vzr inahtaji pure oxygen ya kutosha!
Kumbeeee...ndo mana wale Wa uswazi wengi akili zao hazina akili
 
duuu pole na hongera
kazi ni kazi but nahic nature ya hizo kazi unatakiwa ufanye muda mchache sana kwa uelewa wangu mdogo na mazingira tunayoishi naonaga kama wanaofanya izi kazi kwa muda huwa hawako sawa kiakili hata ukiwaangalia kwenye magari duu
 
Ukirudi nyumbani fanya aroma therapy,fukiza/washa udi,ubani au chochote chenye kuleta harufu nzuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…