Madhara ya kula nyama ya Nguruwe/Kitimoto kwa afya yako...

Madhara ya kula nyama ya Nguruwe/Kitimoto kwa afya yako...

Mmeanza tena vitisho vyenu,hivi we uliyeleta hii mada umeshawahi kula hii kitu au unataka kutunyima raha tu wenzio!:shut-mouth::shut-mouth:
 
tehe...tehe...tehe...... wiki hii tumepumzika na sembe sasa tunazungumzia kupiga marufuku mboga!
tunawashukuru wachangiaji mimi ninachoamini vingi tunavyokula vinamadhara visipoliwa kwa uangalifu lakini kingine (hili sina mashiko nalo) madhara yanayoweza kufanywa na nguruwe wa china hayawezi kulingana na nguliwe wetu hawa achilia mbali ifike sehemu tukubali MUNGU katuumba tofauti.
vinginevyo tuishi kizamani zaidi tuone kama tutaweza tule ugali na mboga za majani tena zisizomwagiliwa wala kuwekewa mbolea ya aina yoyote japo usishangae kwenye unga wa ugali ukipitisha sumaku kuna vumbivumbi la chuma lina nasa.
 
Kila kitu mnataka ufafanuzi utadhani nyie hamna ubongo
Ndio maana mnapotezwa na wanaojiita walimu wa dini!

Soma kila kitu kiko hapo!

Pole sana endelea kupotosha watu kwa kuhalalisha ulaji wa nguruwe na majibu yako yanaonesha hauelewi nini Paul alikuwa amekusudia! Unasoma tu neno jinsi lilivo kavukavu!
 
Hivi wewe unajua kusoma?
Huoni hapo Paulo alikuwa anaandika mambo haya kuhusiana na nyakati zilizokuwa mbele yake na sio alizokuwa anaishi?
Yaani alikuwa anazungumzia future!

Haujajibu umebisha tu!
 
uploadfromtaptalk1380632049554.jpgsooooo sweeeet..yummy
 
Rosemary Alvarez alijikuta akiwa na maumivu ya kichwa na mkono kukosa nguvu. baada ya kufanyiwa scanning ikaoneka kama ni "brain tumor", pindi alipofanyiwa upasuaji alikutwa na "mnyoo (taenia solium)" akiwa hai unakula brain yake. Chanzo hasa cha mnyoo huo ni kula nyama ya nguruwe ambayo kitaalamu anaprotein nyingi kuliko mnyama yoyote na hivyo kuvutia parasite wengi kwa mnyama huyu . Je ni watanzania wangapi wanapata uangalizi wa kugundua afya zao na wanakula nyama hii kila siku tena inayofugwa katika mazingira si salama?. soma zaidi kwenye link hii hapa chini

Source : ABC News: It's Not a Tumor, It's a Brain Worm


Angalia hapa Mchina huyu pia akitolewa minyoo mingi usoni ambayo pia ilisababishwa na utamaduni wa kula nyama ya nguruwe:



Je wewe ni mpenzi wa kitimoto?, fikiria tena.




Mkuu hii thread ilibidi uwapelekee wapuuzi ama wajinga wasiojuwa ukweli kuhusu wanyama na maradhi yao. Hii thread imekaa kiuharakati harakati....Nyama ya nguruwe haina madhara wala tatizo na ni nzuri tu. Ikumbukwe kuwa majuu (Ulaya na America) nyama ya nguruwe ndiyo inayoliwa sana shinda nyama aina yeyote ile na kama hii nyama ingekuwa na madhara kihivyo basi tungepata many cases za watu kuwa na brain tumor. Huyu jamaa huenda ana mazoea ya kula nyama mbichi (ni ugonjwa huu) au la hakupika vizuri hiyo nyama kabla ya kula kwani ilitakiwa apike ipasavyo (iive) ili kuua vijidudu ndipo ale. Wanyama wengi tu tunaowala mbona wana minyoo? I can prove this to you, jaribu kula nyama mbichi ya ng'ombe ama mbuzi for weeks kama hautopata minyoo. Usilete mambo ya kizanzibari hapa (unafiki), lete habari za kiukweli na zenye msingi. Au la ukishindwa basi tuongelee masuala ya unga na tindikali hapa nchini.
 
Last edited by a moderator:
Jumapili hii kuna mzee anaangusha nguruwe wawili pale Kivule, nimeshaweka oda ya kilo tatu
 
Jumapili hii kuna mzee anaangusha nguruwe wawili pale Kivule, nimeshaweka oda ya kilo tatu

Kivule ipi? Kilo 2 tafadhali aniwekee... kuna nyama lakini hii ya huyu kiumbe ni next to delicious...
 
Nyie kuleni tu!

Biblia inasema mmeshakula mpaka watoto wenu na vinyesi vilevile!

Kwa hivyo sioni ajabu nyie kutetea hii nyamafu!
 
Kivule ipi? Kilo 2 tafadhali aniwekee... kuna nyama lakini hii ya huyu kiumbe ni next to delicious...

Teh teh teh teh!

Ulikuwa unataka kusema nini hapa?
Next to delicious! !
But not yet delicious? ??

Teh teh teh teh teh!
 
Mimi nahisi wanaoping hii kitu wantafuta jinsi ya kuifanya iwe harali ili waweze nawao kuhusika kwenye kuchinja. Nguruwe amewakosesha mapato na ndo maana wanatafuta sana elimu ya nguruwe ili wakiona ni bora waseme sisi ndo wachinjaji pekeee mungu katuteua.
 
Qur-an ina weka wazi kua, tusile mzoga, Nguruwe na mnyama alie chinjwa na mtu asie Muislam.
Basi hapo tutumie sheria ya mzee Mwinyi "Anayetaka kula nyoka ruksa....."
kikubwa tudumishe amani ya nchi yetu.Anayetaka mapigano awahi syria.
 
bulama hahahaaaa dah kesho naanza nayo..dah hii sredi ya 2008?
 
Last edited by a moderator:
Ukweli ni kwamba sio kula kitimoto inasababisha minyoo ya ubongo ila ni kula mayai yanayopatikana kwenye majani, mboga, maji etc ndio yanaenda kuanguliwa tumboni na kuwa larva ambao hupenetrate kwenye utumbo na kuingia kwenye damu. Wakishaingia kwenye damu huingia moja kwa moja kwenye ubongo na kuwa cysticerci(buva) ambayo huleta neurocysticercosis. Ukila nyama ya nguruwe unakula cysticerci ambao wanaenda kukomaa na kuwa minyoo mikubwa(taenia-tegu) ambayo hukaa tumboni na kuanza kutaga mayai ambayo ukinya kwenye majani, maji(yanayotumika kumwagilia mboga-dar). Nguruwe akila majani hula mayai ambayo huanguliwa tumbôni na kuwa larva ambao huingia kwenye damu na kukaa kwenye organ mbali mbali ikiwamo misuli(nyama.). Hivyo kutokula nguruwe hakukufanyi ukwepe ugonjwa huu provided eneo unaloishi kuna wafugaji wa nguruwe.
 
Kisamvu? kisamvu cha kopo? mbona sikijui hicho! kinauzwa supermarket au dukani kwa mangi? Tuagizie tukanunue nasi tuonje kikoje!

mkuu lugha za vijana hizi utaziweza wewe?
inabidi uwe ushakaa uswahilini au vijiweni ndio utaenda sawa na hizi lugha.

kisamvu cha kopo ni KABANG /TIgo mkuu
 
Hakika ni kuwa Agano la Kale katika Biblia imekataza ulaji wa nguruwe na akafanywa

kuwa ni haramu: “Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu ni najisi. Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao wala msiguse mizoga yao” (Walawi 11: 7 – 8).

Agizo hilo limerudiwa katika Kumbukumbu la Shari’ah 14: 7 – 8 na pia Isaya 66: 17.

Na katika Agano Jipya, Yesu naye amesema kuwa hakuja kutangua shari’ah na mafundisho ya manabii bali kukamilisha (Mathayo 5: 17). Kwa ibara hiyo ni kuwa Yesu pia aliharamisha ulaji wa nguruwe.
 
WALAJI WA NGURUWE KUPATA KIFAFA




CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimehadharisha walaji wa nyama ya nguruwe nchini, kuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata kifafa.Utafiti wa kisayansi uliofanywa na SUA, umebaini

kuwa baadhi ya nguruwe wana minyoo aina ya tegu ambao nyama yao ikiliwa bila kuiva vizuri, mlaji atapata minyoo hiyo ambayo huingia kichwani na kusababisha kifafa.Akizungumza na gazeti hili

hivi karibuni, Mhadhiri na Mtafiti wa Idara ya Sayansi ya Wanyama na Uzalishaji ya SUA, Profesa Faustine Lekule, alisema sampuli za utafiti huo kutoka Mbeya, zimebaini nguruwe wengi wakiwamo

wanaosafirishwa katika miji mikubwa wameathirika na minyoo hiyo.Kwa mujibu wa Profesa Lekule, wataalamu wa SUA wanaosimamia Mradi wa Utafiti wa Kuboresha Ufugaji wa nguruwe kwa mkoa

wa Mbeya ili kuinua pato la kaya, unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Denmark (DANIDA), walibaini hatari hiyo baada ya kuchukua sampuli ya nyama ya nguruwe kwa ajili ya

vipimo."Majibu ya sampuli ambazo wataalamu wamezichukua kutoka kwa nguruwe wa wafugaji kwenye baadhi ya vijiji, wamebainika kukumbwa na hatari hii. "Lazima jitihada za makusudi

zichukuliwe katika kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili kati ya watafiti na Serikali," alisema Profesa Lekule.Alisema maambukizi ya tegu au minyoo ya nguruwe yanatokana na tabia za baadhi

ya wafugaji kutozingatia ufugaji bora kwa kuwaacha kujitafutia chakula na maji mitaani na kula kinyesi cha binadamu.Kwa mujibu wa Profesa Lekule, baadhi ya wafugaji wamekuwa wakijisaidia

vichakani na kuwaacha nguruwe kutafuta malisho katika vichaka na kula kinyesi chao, hali inayochangia ongezeko la maambukizi ya minyoo ya tegu hao.Baada ya kula kinyesi minyoo

humwingia mwilini na kumdhoofisha na baadaye binadamu anapokula nyama ambayo haijaiva vizuri, minyoo hiyo humwingia na kusababisha kifafa baada ya kuingia kichwani.Alisema athari za

kuenea kwa maambuziki hayo inaweza kutokea katika miji mikubwa ikiwamo Dar es Salaam kwa kuwa nguruwe wa Mbeya husafirishwa na kuuzwa maeneo hayo."Hatua hii inaweza kusababisha

kusambaa kwa ugonjwa huu, hivyo ushirikiano kati ya wafugaji, wafanyabiashara, Serikali na wataalamu wa afya katika kufikia hatua ya kumaliza changamoto hii unahitajika," alibainisha

Profesa Lekule.
(Kwa hisani ya Venance Gilbert at Thursday, December 26, 20130)

UFUGAJI BORA WA NGURUWE
Nguruwe ni mnyama mwenye faida, ni rafiki kwa mazingira na hahitaji gharama kubwa

"Ufugaji wa Nguruwe ni lazima uwe wa kisasa ili kupata mazao bora. Unaweza kupata kila unachohitaji wewe, familia na hata ndugu zako kutokana na ufugaji wa nguruwe", anasema Bwana

Lomaiyani Molel kutoka Arusha. Jamii nyingi hapa Tanzania huchukulia nguruwe kama mnyama mchafu na asiyefaa kuwa karibu naye na hata kwa matumizi kama lishe. Zaidi, nyama yake

inapendwa na haina madhara kwa afya na inapendekezwa kuliwa zaidi kuliko nyama nyekundu. Unaweza kuanzisha mradi wa nguruwe kwa gharama ndogo lakini baada ya kipindi cha miezi tisa tu ukaanza kujipatia kipato kutokana na ufugaji huo.

Ufugaji

Kwa kawaida nguruwe wanafugwa na watu wa kada zote, wafugaji wadogo wadogo na hata wakubwa. Aina hii ya ufugaji huweza kumpatia mkulima kipato pamoja na lishe kwa familia, na hauhitaji gharama kubwa.

Banda

Nguruwe wanahitaji kuwa na banda lililojengwa kwa vifaa nafuu. Unaweza kutumia mchanga na simenti kuweka sakafu, ama ukatumia udongo wa mfinyanzi kwa ajili ya kuweka sakafu. Ukubwa wa banda unategemeana na idadi ya nguruwe unaotaka kufuga. Mita 3 kwa mita 2.5 zitawaweka guruwe 8-10 wanaonenepeshwa kwa soko au nguruwe jike mmoja na nguruwe ndume mmoja.

Malisho

Ulishaji wa nguruwe ni rahisi kwa kuwa wanakula aina mbalimbali za vyakula kulingana na mazingira wanayofugwa. Unaweza kuwalisha kwa kutumia majani laini ya aina mbalimbali, na pia hulishwa kwa kutumia masalia ya nafaka (pumba). Unaweza kuwalisha kwa kutumia mashudu au pumba aina ya Wheat Poland. Pia unaweza kuwalisha kwa kutumia mabaki ya jikoni.

Kuzaliana

Nguruwe hubeba mimba kwa kipindi cha siku 114, ambazo hugawanyika kwa miezi 3, wiki 3 na siku 3. Nguruwe mmoja ana uwezo wa kuzaa watoto 6 hadi 14 kwa mara moja. Watoto wa nguruwe (piglets) huanza kula chakula cha kawaida wanapofika umri wa mwezi mmoja na nusu mpaka miezi miwili. Endapo nguruwe watapata matunzo mazuri, baada ya miezi 8 wanakuwa na uzito kati ya kilo 50-70 na wanaweza kuuzwa.

Matunzo

Baada ya nguruwe kuzaa anatakiwa kupatiwa chakula cha kutosha na cha kutia nguvu ili kupata maziwa ya kutosha kwa ajili ya watoto wake. Watoto wa nguruwe wachomwe sindano ya madini ya chuma (Iron injection) baada ya siku moja au mbili toka kuzaliwa. Hii ni muhimu sana vinginevyo wanaweza kufa wote. Kata meno (tooth clipping) baada ya miezi mitatu. Unaweza kuhasi madume (castration) baada ya miezi miwili.

Magonjwa yanayoathiri nguruwe

Kuna aina nyingi za magonjwa yanayoshambulia nguruwe, lakini yapo yale yaliyozoeleka ambapo ni lazima kukabiliana nayo ili kuwa na ufugaji wenye tija.

Ugonjwa wa miguu na midomo

Ugonjwa huu huathiri nguruwe sehemu za miguu na midomo. Ni ugonjwa ambao hushambulia nguruwe mara kwa mara hasa wasipokuwa na matunzo mazuri. Ugonjwa wa miguu na midomo, hudhoofisha nguruwe kwa haraka sana, ikiwa ni pamoja na kupungua uzito.

Chanjo: Chanjo kwa ajili ya ugonjwa wa midomo na miguu (FMD vaccine) hutolewa kila baada ya mwaka mmoja. Hii inasaidia kuwaweka nguruwe wako katika hali nzuri zaidi bila kushambuliwa na magonjwa hayo.

Tiba: Ugonjwa huu hauna tiba halisi. Inapotokea nguruwe wakawa wameshambuliwa kinachofanyika ni kutibu magonjwa nyemelezi kwa kutumia antibiotics.

Homa ya Nguruwe (Swine fever)


Virusi vinavyosababisha ugonjwa wahoma ya nguruwe huenea kwa harakasana miongoni mwa makundi yanguruwe, na huua kwa haraka sana,lakini hauna madhara kwa binadamuna hauambukizwi kwa binadamu.Nguruwe walioambukizwa waanshikwana vindonda ama mapunyekwenye ngozi. Pia masikio na ngozihuwa mekundu.


Chanjo: Ugonjwa huu hauna chanjo wala tiba. Kinachofanyika mlipuko unapotokea ili kuwa salama ni kuwateketeza nguruwe wote walioathirika na kuanza upya. Unaweza kuteketeza kwa kuwachoma moto.


Muhimu: Baada ya kuwateketeza nguruwe wagonjwa, safisha banda kisha nyunyiza dawa aiana ya Acon au Ectomin, na uache banda wazi kwa kipindi cha wiki moja kabla ya kuweka nguruwe wengine.

Ugonjwa wa mapafu (Pneumonia)

Huu ni ugonjwa unaoshambulia sehemu za koo na mapafu ya nguruwe, ambapo husababisha kukohoa na kupumua kwa shida. Ugonjwa huu husababishwa na bacteria (Secondary bacterial), joto kupita kiasi, vumbi na gesi inayotokana na madawa makali.

Tiba: Homa ya mapafu kwa nguruwe inatibika kwa kutumia antibiotics. Pamoja na kuwaweka wanyama sehemu safi, isiyo na baridi kali au joto la kupitiliza kiwango.

Kimeta (Anthrax)

Huu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria wanaojulikana kama Bacillus anthracis, wadudu hawa wanabaki kuwa hai kwa muda mrefu na wanaweza kuwa kwenye udongo wakiwa hai kwa kipindi cha miaka mingi.

Chanjo: Chanja nguruwe wako dhidi ya kimeta kama utakavyoelekezwa na wataalamu wa mifugo walio karibu nawe.

Tiba: Unaweza kutibu nguruwe wako kwa kutumia dawa aina ya Penisilin au Oxytetracycline.

Muhimu: Homa ya nguruwe ni lazima iwekewe karatini kwa sababu husambaa kwa haraka sana. Nchini Tanzania mlipuko wa homa ya nguruwe umekuwa ukitokea mara kwa mara maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Malawi na katika mkoa wa Mbeya.

Ushauri: Kwa ushauri zaidi juu ya ufugaji wa Nguruwe na magonjwa ya wanyama, unaweza kuwasiliana na Mtaalamu wa mifugo Bwana Oletikoishi Wawaa, simu 0754 207 987.



Chanzo. MNYALUKOLO: WALAJI WA NGURUWE KUPATA KIFAFA
 
Back
Top Bottom