Pre GE2025Madiwani Kigoma ujiji walalama miradi ya maendeleo kukwama hivyo kuonekana hawajatimiza wajibu wao, waishutumu TAMISEMI wakitaka uchunguzi ufanyike
Wananchi na madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji wamekataa kuendelea na mkandarasi anayejenga Soko Kuu la Mwanga na Soko la Samaki katika Mwalo wa Katonga, wakidai ameshindwa kutekeleza mradi kwa wakati na kusababisha hasara kwa wafanyabiashara waliokosa maeneo ya kufanyia biashara zao.
Mvutano huo umeibuka wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo uliofanywa na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, ambapo madiwani na wananchi walimkataa mkandarasi mshauri, wakisema ameshindwa kusimamia kazi ipasavyo.
Soko la Mwanga lilivunjwa takribani miaka mitatu iliyopita kwa lengo la kulijenga upya kwa viwango vya kisasa, lakini mpaka sasa ujenzi wake unasuasua, hali iliyoongeza malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara.
Kutokana na hali hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Baraka Lupori, ametoa tamko rasmi la kutaka mkataba wa mkandarasi huyo usitishwe mara moja ili taratibu za kumpata mkandarasi mwingine zianze. Pia, ameishauri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) ichunguzwe, akidai kuwa wakandarasi wanaopatikana kupitia ofisi hiyo mara nyingi wamekuwa wakisababisha ucheleweshaji wa miradi mkoani humo.
Ina maana hao TAMISEMI wanatoa tenda Kwa wakandarasi hata kama hawana vigezo?.. basi kama ni ndio basi either Kuna upendeleo mkubwa katika utoaji wa hizo tenda
Wananchi na madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji wamekataa kuendelea na mkandarasi anayejenga Soko Kuu la Mwanga na Soko la Samaki katika Mwalo wa Katonga, wakidai ameshindwa kutekeleza mradi kwa wakati na kusababisha hasara kwa wafanyabiashara waliokosa maeneo ya kufanyia biashara zao.
Mvutano huo umeibuka wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo uliofanywa na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, ambapo madiwani na wananchi walimkataa mkandarasi mshauri, wakisema ameshindwa kusimamia kazi ipasavyo.
Soko la Mwanga lilivunjwa takribani miaka mitatu iliyopita kwa lengo la kulijenga upya kwa viwango vya kisasa, lakini mpaka sasa ujenzi wake unasuasua, hali iliyoongeza malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara.
Kutokana na hali hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Baraka Lupori, ametoa tamko rasmi la kutaka mkataba wa mkandarasi huyo usitishwe mara moja ili taratibu za kumpata mkandarasi mwingine zianze. Pia, ameishauri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) ichunguzwe, akidai kuwa wakandarasi wanaopatikana kupitia ofisi hiyo mara nyingi wamekuwa wakisababisha ucheleweshaji wa miradi mkoani humo.
Ina maana hao TAMISEMI wanatoa tenda Kwa wakandarasi hata kama hawana vigezo?.. basi kama ni ndio basi either Kuna upendeleo mkubwa katika utoaji wa hizo tenda
Shida ni kubwa jana Mchengerwa huko Dodoma alimpiga pin mkandarasi asipewe kazi hata ya jero kisa mambo kama hayo ya ujiji, lakini siku zote walikuwa wapi yaani ni kama wamekurupushwa usingizini
Wanatafuta huruma kwa Wananchi, ila kimsingingi hao madiwani hawafai kuaminiwa tena na wapiga kura.
Mradi una miaka zaidi ya mitatu, mmekaa kimya siku zote huku mkiuma na kupuliza, baada ya kuona mnataka kunyanganywa tonge mdomoni ndiyo mnajifanya wanafiki eti mnataka kupambania maslahi ya wananchi.
Shida ni kubwa jana Mchengerwa huko Dodoma alimpiga pin mkandarasi asipewe kazi hata ya jero kisa mambo kama hayo ya ujiji, lakini siku zote walikuwa wapi yaani ni kama wamekurupushwa usingizini