Maelfu ya Warusi waanza kujitokeza na kuandamana kupinga kinachofanyika dhidi ya ndugu zao Ukraine

Maelfu ya Warusi waanza kujitokeza na kuandamana kupinga kinachofanyika dhidi ya ndugu zao Ukraine

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Ifahamike Ukraine na Urusi ni watu wamoja, na lugha inayotumika sana Ukraine ni Kirusi, maelfu ya Warusi hawaungi mkono huu uvamizi dhidi ya ndugu zao, ukiingia kwenye mitandao ya kijamii wengi wanatukana sana maana hawaelewi nini sababu za mauaji yanayoendelea au tija yake kwa Urusi, pia kuna taarifa baadhi ya wanajeshi wa Urusi wamenza kujisalimisha Ukraine na kugoma kuendelea kuua ndugu zao bila kuelewa nini sababu kuu.

Putin kwenye hili kachemsha, ingekua vita dhidi ya watu wa tabaka tofauti, Warusi wengi wangemuelewa, lakini hapa ni mauaji kwa ndugu zao kabisa wanaochangia vinasaba, na hakutumia muda wake vizuri kuwaelewesha ulazima au umuhimu wa mauaji haya, kakurupuka tu na kutuma majeshi yaanze uvamizi.

Huu uvamizi umesababisha Warusi wengi walio ugenini waishi kwa aibu ya kutojitambulisha popote utaifa wao.

https://www.news10.com/news/ukraini...sian-platoon-surrendered-to-ukrainian-forces/

 
The Taliban is closely following the military conflict between Russia and Ukraine and calls on the parties to dialogue. The Taliban authorities called on the warring parties to resolve the conflict by peaceful means. https://t.co/wcRCQdliNO

Hivi vita vitaibua mengi, Mchina anasubiri matokeo yake kisha alianzishe dhidi Taiwan na Hongkong, naye Kiduku anapasha misuli moto dhidi ya wabaya wake.
 
Ifahamike Ukraine na Urusi ni watu wamoja, na lugha inayotumika sana Ukraine ni Kirusi, maelfu ya Warusi hawaungi mkono huu uvamizi dhidi ya ndugu zao, ukiingia kwenye mitandao ya kijamii wengi wanatukana sana maana hawaelewi nini sababu za mauaji yanayoendelea au tija yake kwa Urusi, pia kuna taarifa baadhi ya wanajeshi wa Urusi wamenza kujisalimisha Ukraine na kugoma kuendelea kuua ndugu zao bila kuelewa nini sababu kuu.

Putin kwenye hili kachemsha, ingekua vita dhidi ya watu wa tabaka tofauti, Warusi wengi wangemuelewa, lakini hapa ni mauaji kwa ndugu zao kabisa wanaochangia vinasaba, na hakutumia muda wake vizuri kuwaelewesha ulazima au umuhimu wa mauaji haya, kakurupuka tu na kutuma majeshi yaanze uvamizi.

Huu uvamizi umesababisha Warusi wengi walio ugenini waishi kwa aibu ya kutojitambulisha popote utaifa wao.

https://www.news10.com/news/ukraini...sian-platoon-surrendered-to-ukrainian-forces/

Upuuzi.....
 
Maelfu wapi Media za west wanajaribu kufanya kama kuna maelfu ya watu wakati ni kawaida tu kutokea vikundi vidogo kupinga kama huku wako watu watapinga tu haijalishi ni nini sera zao pinga kila kitu. Huu mziki mkubwa hauzimwi na vikaratasi barabarani. Hao CNN sijui BBC wanajitahidi kupaka rangi watu waamini lakini wapi ngoma imefika mji mkuu wa Ukraine.
 
Mumeshaambiwa muache ku'shake makalio......au bado hamjaelewa hiyo lugha. +254 na u much know
9c12090db53a48c68a830cd45b7195fe(5).jpg
 
Maelfu wapi Media za west wanajaribu kufanya kama kuna maelfu ya watu wakati ni kawaida tu kutokea vikundi vidogo kupinga kama huku wako watu watapinga tu haijalishi ni nini sera zao pinga kila kitu. Huu mziki mkubwa hauzimwi na vikaratasi barabarani. Hao CNN sijui BBC wanajitahidi kupaka rangi watu waamini lakini wapi ngoma imefika mji mkuu wa Ukraine.

Mpaka sasa waliokamatwa na kutiwa jela kisa maandamano wametimia 1,600
Hicho sio kikundi kidogo, ingekua ugomvi wa Urusi dhidi ya Marekani au kwingine angeleeweka, ila hapa anaua jamii ya Warusi.
 
Mpaka sasa waliokamatwa na kutiwa jela kisa maandamano wametimia 1,600
Hicho sio kikundi kidogo, ingekua ugomvi wa Urusi dhidi ya Marekani au kwingine angeleeweka, ila hapa anaua jamii ya Warusi.
Hao ni kama chadema wa urusi maandamano yanakuaga makubwa tu tena zaidi ya hapo na wanatulizwa,,,,.....putin sio kama hajui kuna vinega ndani ya nchi yake na alishajiandaa na hilo....hao wameanza kuandamana tokea siku ya kwanza ukraine inavamiwa
 
Mpaka sasa waliokamatwa na kutiwa jela kisa maandamano wametimia 1,600
Hicho sio kikundi kidogo, ingekua ugomvi wa Urusi dhidi ya Marekani au kwingine angeleeweka, ila hapa anaua jamii ya Warusi.
Ni kweli warusi wengi hii Vita hawaitaki sema kwavile jamaa ni mbabe na hawana cha kufanya wanabaki kuumia moyoni wanachofanyiwa ndugu zao,wengi humu wamejaa ushabiki,unafurahia binadamu mwenzako kuuliwa,na ni nchi huru ina maamuz yake
 
Eti kakaa Kibera huko Anaangalia Propaganda Kisha huyoo JF Upuuzi mtupu
Maelfu wapi Media za west wanajaribu kufanya kama kuna maelfu ya watu wakati ni kawaida tu kutokea vikundi vidogo kupinga kama huku wako watu watapinga tu haijalishi ni nini sera zao pinga kila kitu. Huu mziki mkubwa hauzimwi na vikaratasi barabarani. Hao CNN sijui BBC wanajitahidi kupaka rangi watu waamini lakini wapi ngoma imefika mji mkuu wa Ukraine.
 
The Taliban is closely following the military conflict between Russia and Ukraine and calls on the parties to dialogue. The Taliban authorities called on the warring parties to resolve the conflict by peaceful means. https://t.co/wcRCQdliNO

Ha ha ha!! Hata hawa naona hawakubaliani na Putin....
 
Ifahamike Ukraine na Urusi ni watu wamoja, na lugha inayotumika sana Ukraine ni Kirusi, maelfu ya Warusi hawaungi mkono huu uvamizi dhidi ya ndugu zao, ukiingia kwenye mitandao ya kijamii wengi wanatukana sana maana hawaelewi nini sababu za mauaji yanayoendelea au tija yake kwa Urusi, pia kuna taarifa baadhi ya wanajeshi wa Urusi wamenza kujisalimisha Ukraine na kugoma kuendelea kuua ndugu zao bila kuelewa nini sababu kuu.

Putin kwenye hili kachemsha, ingekua vita dhidi ya watu wa tabaka tofauti, Warusi wengi wangemuelewa, lakini hapa ni mauaji kwa ndugu zao kabisa wanaochangia vinasaba, na hakutumia muda wake vizuri kuwaelewesha ulazima au umuhimu wa mauaji haya, kakurupuka tu na kutuma majeshi yaanze uvamizi.

Huu uvamizi umesababisha Warusi wengi walio ugenini waishi kwa aibu ya kutojitambulisha popote utaifa wao.

https://www.news10.com/news/ukraini...sian-platoon-surrendered-to-ukrainian-forces/


Tunapambania maslahi mapana ya nchi,our motherland Russia.
Hata marekani baadhi ya raia walipinga USA kuivamia Iraq,Afghastan,Vietnam(kipindi Cha vita baridi).
Hata hapa bongo Kuna watanganyika hawapendi kuona huu muungano wetu na Zenj,wanatamani Zenj iachwe iende.
Sio ajabu,Cha muhimu ni maslahi mapana ya nchi.
 
Ni kweli warusi wengi hii Vita hawaitaki sema kwavile jamaa ni mbabe na hawana cha kufanya wanabaki kuumia moyoni wanachofanyiwa ndugu zao,wengi humu wamejaa ushabiki,unafurahia binadamu mwenzako kuuliwa,na ni nchi huru ina maamuz yake

Amesababisha chuki kwa Warusi duniani "Russophobia" iongezeke kwa kiasi kikubwa sana, sasa hivi Warusi wengi walio ugenini wanaficha uraia wao kwa aibu.
Mpaka sasa miji 40 nchini Urusi wameanza kujitokeza kwenye maandamano...

 
Back
Top Bottom