Maendeleo ya teknolojia ya China yamekuwa na manufaa makubwa kwa nchi za dunia ya tatu

Maendeleo ya teknolojia ya China yamekuwa na manufaa makubwa kwa nchi za dunia ya tatu

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG31444040194.JPG


Mwishoni mwa mwezi Mei (30 Mei) China iliadhimisha siku ya saba ya wafanyakazi wa sekta ya sayansi na teknolojia. Siku hii iliadhimishwa kwa mwito wa kuhimiza utamaduni wa uvumbuzi, na kuendelea kujienga China kuwa nchi yenye nguvu kwenye sekta ya sayansi na teknolojia, huku ikifanya juhudi kuelekea kujitegemea kwenye mambo ya sayansi ya teknolojia kwa kiwango cha juu.

Zaidi ya miaka 50 iliyopita China ilikuwa ni moja kati ya nchi zilizo nyuma kwenye sekta ya sayansi na teknolojia. Kama ilivyo sasa kwa nchi nyingi za Afrika, wakati huo China ililazimika kutumia fedha nyingi kupata teknolojia kutoka nchi za magharibi, lakini mchango wa teknolojia hizo kwa maendeleo ya nchi haukuwa mkubwa sana. Hii ni kutokana na kuwa kutokana na sababu za kisiasa, nchi za magharibi hazikupenda kuizuia China teknolojia zake.

Maendeleo ya sayansi na teknolojia ya China yalianza kushika kasi mwaka 2006, baada ya China kuanzisha mpango wa muda wa kati na muda mrefu wa maendeleo ya sayansi na teknolojia. Lengo la mpango huo lilikuwa ni kuifanya China kuwa jamii inayotegemea sayansi na teknolojia kabla ya kufikia mwaka 2020, na kuwa nchi inayoongoza duniani kwenye sekta ya sayansi na teknolojia kabla ya mwaka 2050. Wakati ikielekea kwenye lengo hilo mpango ni kuwa China itatumia asilimia 2.5 ya pato lake la taifa GDP kwenye masuala ya utafiti na uendelezaji wa teknolojia (R&D), na mchango wa sayansi na teknolojia kwa maendeleo ya nchi ufikie asilimia 60.

Kwa wanaofuatilia maendeleo ya China, mambo haya yanaonekana kuendelea kama ilivyopangwa. Si kwenye sekta ya uzalishaji viwanda, afya, kilimo, anga ya juu na hata Tehama, China kwa sasa inazikaribia nchi zinazoongoza duniani kisayansi kwenye sekta hizi, na katika baadhi ya maeneo tayari imezitangulia nchi nyingine.

Tunafahamu kuwa China mara nyingi inarudia kauli yake ya “kujenga jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja”. Maneno haya yanaonekana kwenye ushirikiano kati ya China na nchi za dunia ya tatu, hasa za Afrika kwenye sekta ya teknolojia. China pia haipendi kuona nchi zilizo nyuma kiteknolojia zinapata taabu kama ilivyopata taabu wakati inaweka msingi wake wa maendeleo.

Kwa sasa tunaweza kuona watu wa Afrika wanaweza kufurahia baadhi ya teknolojia za kiwango cha juu duniani, ambazo ingekuwa ni vigumu sana kuzipata kutoka nchi za magharibi. Tukiangalia sekta ya ujenzi, kila mtu anaweza kuona kuwa ujenzi katika nchi nyingi za Afrika umeboreka, sio tu kutokana na makampuni ya ujenzi kutoka China yanatekeleza ujenzi, bali pia teknolojia za ujenzi, zana za ujenzi na hata mienendo ya wajenzi inaboreka kutokana na ushirikiano. Tukiangalia kwenye sekta ya afya, zamani ilikuwa ni ndogo kusikia matibabu ya moyo hasa upasuaji ukifanyika barani Afrika, lakini sasa limeanza kuonekana kuwa ni jambo la kawaida kutokana na ushirikiano kwenye sekta ya afya kati ya China na nchi za Afrika, sio tu umesaidia kuwapa mafunzo ya utaalamu wa afya watu wa Afrika, bali pia umesaidia kujengwa kwa hospitali za kisasa katika nchi mbalimbali za Afrika.

Lakini pia maendeleo ya sayansi na teknolojia nchini China yameimarisha uwezo mkubwa wa uzalishaji wa bidhaa za matumizi ya kila siku, ambazo sasa zinauzwa katika miji mbalimbali ya Afrika. Zamani bidhaa hizo zilionekana kama ni za anasa, na ziliagizwa tu na matajiri au waafrika waliokuwa wanakwenda Ulaya na Marekani. Kwa sasa si ajabu sana kuona mtu wa kijijini Afrika akiwa na simu janja iliyounganishwa kwenye mtandao wa internet, au kuwa na vitendea kazi vya kisasa na gharama nafuu vilivyotengenezwa China.
 
Si kweli kua miaka 50 iliyopita walikua nyuma kiteknolojia.

kwetu Sisi wachina walitujengea reli ya tazara Kwa mda wa miaka 5. 1970/1975.

Walitumia vifaa vyao mitambo Yao na wakaweka treni na mabehewa Yao.

Walituletea radio zao vyerehani vyao baskeli na vifaa vingi.

Ni makosa Sana kujifananisha na china ukweli unafichwa .

China ilikua mbele kiteknolojia miaka mingi.

Kuna mtume aliwaasa Uma wake utafute ELIMU mpaka china Enzo hizo.

Niko ELIMU ilikuweko
 
Si kweli kua miaka 50 iliyopita walikua nyuma kiteknolojia.
kwetu Sisi wachina walitujengea reli ya tazara Kwa mda wa miaka 5. 1970/1975.
Walitumia vifaa vyao mitambo Yao na wakaweka treni na mabehewa Yao.
Walituletea radio zao vyerehani vyao baskeli na vifaa vingi.
Ni makosa Sana kujifananisha na china ukweli unafichwa .
China ilikua mbele kiteknolojia miaka mingi.
Kuna mtume aliwaasa Uma wake utafute ELIMU mpaka china Enzo hizo.
Niko ELIMU ilikuweko
Hiyo iliyojengwa miaka mitano miaka hiyo kwa leo wangejenga kwa miezi mitano.

Tukubali tu jamaa wako vizuri
 
kwetu Sisi wachina walitujengea reli ya tazara Kwa mda wa miaka 5. 1970/1975
Nchi za Magharibi waliubeza mradi wa ujenzi wa reli ya TAZARA kuwa hautakamilika

Wachina wakaumaliza mwaka mmoja mapema tofauti na walivyopanga

Nchi za Magharibi ziliumia sana na kufedheheka
 
Back
Top Bottom