KWELI Maeneo nje ya Jiji la Dar es Salaam yalikabiliwa na upungufu wa Mafuta ya Petroli mwaka 2023

KWELI Maeneo nje ya Jiji la Dar es Salaam yalikabiliwa na upungufu wa Mafuta ya Petroli mwaka 2023

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Kuna maeneo fulani nimepita ya mkoa wa dodoma wilayani huko; nimekuta kuna msururu mrefu sana wa vyombo vya moto kwenye moja ya petrol station. Nikajaribu kuuliza kuna shida gani hapa? Wenyeji wanasema mafuta ya petrol hamna kabisa wilayani hapo.

Baadhi ya vituo vya mafuta vimesitisha huduma. Pia majuzi nilisikia kuna sehemu hapa tz pia kuna shida ya mafuta.
mafutapic.jpg
 
Tunachokijua
Julai 13, 2023, Mtumiaji mmoja wa JamiiForums alitoa taarifa inayodokeza uwepo wa uhaba mkubwa wa mafuta ya Petroli Wilayani Ngara.

Kwa mujibu wa maelezo yake, hiyo ilikuwa ni siku ya 4 mfululizo tangu uhaba huo wa mafuta uanze kuonekana.

Madai haya hayakuishia hapo. Julai 14, 2023, mtumiaji mwingine wa JamiiForums alizungumzia tatizo hilo kuwepo huko Liwale. Hali kadhalika, Julai 17, 2023, tatizo hili liliripotiwa kwa mara ya 3 kuwepo nchini.

Hali halisi ilivyo
JamiiForums imezungumza na Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Titus Kaguo aliyethibitisha uwepo wa changamoto hii. Amesema:

"Ni kweli kuna changamoto hususani maeneo mikoa iliyopo pembezoni kidogo, kulitokea hitilafu katika mfumo wa upakuaji, hivyo ukasababisa mafuta kuchelewa kufika katika maeneo ya mbali. Lakini mafuta yapo, yasingekuwepo ungeshuhudia Dar es Salaam kukiwa na changamoto."

"Kutokana na changamoto hiyo baadhi ya watu wamechukulia hali hiyo kununua mafuta kwenye madumu au Mapipa na kuuza kwa gharama ya juu, hali ambayo tunaichukulia kama ulanguzi.

"Mfumo wa usafirishaji nao unaleta changamoto ambapo lori linachukua siku nne hadi kufika Kigoma au Katavi au Kagera, hivyo kufanya huduma hiyo kusuasua.

"Changamoto ya ulanguzi hakuna anayejionesha na hakuna risiti anayopewa, bali tunasikia watu wakilalamika na kwa kuwa wanauziwa nje ya vituo hiyo ni Police Case, lakini cha muhimu tunafuatilia kumaliza tatizo hilo"


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), ni taasisi ya udhibiti wa huduma za nishati na maji inayojitegemea, iliyoundwa kwa Sheria ya EWURA Sura ya 414 ya Sheria za Tanzania na marekebisho yake Na. 6 ya mwaka 2019.

EWURA, ilianza kazi rasmi Septemba, 2006 ikiwa na wajibu wa kusimamia shughuli zote za kiuchumi na kiufundi katika sekta za Nishati (umeme, petroli na gesi asilia); na Maji (majisafi na usafi wa mazingira).

Hii ni taarifa ya Julai 17, 2023.
Shida ni bandari, wakipewa DP hii shida haitojitokeza Tena wanapakuwa mizigo kwa wakati.😀😀
 
Nishati ya mafuta ni muhimu sana; ila ni nishati inayotumia sana fedha ya kigeni (uagizwaji) na haizalishi fedha ya kigeni.
 
Issue ni kwamba wanunuzi wa mafuta wananunua mafuta kwa kutumia Dola za Marekani.

Sasa mambo mawili yametokea:

1. Dola za mMarekani hazipatikani

2. Dola za Marekani zikipatikani ziko juu sana .

Hivyo wanunuzi wa mafuta wanasita pia kukunua ili wanasubiri Dola ishuke
 
Baadhi ya vyombo vya habari UCHWARA na vigazeti UCHWARA wameripoti baadhi ya vituo vya mafuta kuishiwa mafuta au kugoma kuyauza.
Tuvipuuze vigazeti na viredio hivi UCHWARA au ni KWELI kuna uhaba?.

Koment fupi fupi nitazijibu

Sent from my TECNO CI6 using JamiiForums mobile app
 
Mafuta Yapo. Kwakuwa kesho Jumatato Bei itapanda sana sana tu kutokana na Kushuka kwa Thamani ya Shilingi dhidi ya Dolla baaasi wafanyabiashara wameficha Mzigo ili Jumatano wauze kwa bei juu wapate faida kubwa.
Hakuna Uhaba wa Mafuta Mkuu note that.
 
Baadhi ya vyombo vya habari UCHWARA na vigazeti UCHWARA wameripoti baadhi ya vituo vya mafuta kuishiwa mafuta au kugoma kuyauza.
Tuvipuuze vigazeti na viredio hivi UCHWARA au ni KWELI kuna uhaba?.

Koment fupi fupi nitazijibu

Sent from my TECNO CI6 using JamiiForums mobile app
Changanya mafuta ya alizeti na mafuta ya taa utapata dizeli.
 
Tulieni mpaka kesho mafuta yapande kwanza. Kila ng'ombe anakula kutokana na urefu wa kamba yake
 
Back
Top Bottom