Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

ndio matatizo ya kusali kwenye makanisa ya manabii wauongo!! mnachanganywa mpaka akili!
 
Mkuu hana ubaya wowote, Tatizo ni chama kujifanya kikubwa kuliko Taifa,
 
Bila shaka unajutia uzi huu uliounzisha 2015...bila shaka unajutia kile ulichokuwa unawaza....bila shaka unatubu juu ya maashi yako haya...TUMEKUSAMEHE BURE 2017
 
Kumbe ni Hoja za kusifia.Hongera sana JPM kwa kasi ya VodaCCM maana naona jinsi unavyowabatisa kwa moto Wapinzani. Kila siku Polisi wapo tayari kuwakamata na kuwafungulia mashtaka hata kwenye Kampeni bado wanafunguliwa mashtaka
 
Nimetafakari sana, nimegundua kuwa kwa hakika watanzania tulikuwa tunahitaji Rais kama Magufuli.
Ninachosikitika zaidi ni kwamba, baadhi ya watanzania wenzetu ama kwa makusudi au kwa kutokujua wanabeza kazi nzuri anazozifanya Rais wetu Magufuli na serikali yake.

Watanzania wengi walikuwa wanaimba MABADILIKO bila kujua gharama za hayo mabadiliko.
Binafsi naona haya ndiyo mabadiliko tuliyoyasubiri kwa miaka mingi sasa. Kimsingi huwezi kusema unafanya mabadiliko halafu ukabaki katika hali ile ile.

Tunapotaka mabadiliko ya kiuchumi hatunabudi kujifunga mkanda kwanza ili kutengeneza miundombinu ya kiuchumi na hivyo kurahisisha maendeleo ya huo uchumi.

Mimi naamini kuwa, kama tutakwenda kwa mwendo huu , kwa hakika baada ya miaka michache Tanzania itakuwa ni yenye maendeleo makubwa sana.

Naomba tumuunge mkono Rais wetu Magufuli ili kufikia malengo haya. MAENDELEO HAYAJI KAMA NDOTO.
 
Maendeleo hayaji kwa kuminya uhuru wa habari nchini, kutoheshimu katiba, kupindisha sheria za nchi. Kuwa busy kutaka kuviua vyama vya upinzani. Kutumia pesa chungu nzima ambazo hazijaidhinishwa na Bunge, kutoa rushwa kwa Wabunge wa MACCM ili wapitishe muswaada Uchwara, kukwapua mabilioni ya wahanga, kusema uongo kwamba nchini hakuna njaa, kuendesha nchi kwa style ya one man show. Kulipukalipuka bila kutafakari kwa kina na kufukuza watu kazi kwa uonevu.

 
kweli watanzania inabidi tupimwe akili kitu kikiwa cheupe hata ukiwa mbali kwa cm 100 utakiona ni cheupe na kikiwa cheusi utakiona ukiona walalimikaji wanakuwa wengi kuzzidi wanaokusuppot jua kuna tatizo mahal,haingii akilini kila mtu aliye bado unasema upo sawa
 
hatuwezi kupata mabadiliko ya kweli kama CCM bado ipo madarakani.

Nchi inakabiliwa BAA LA NJAA, rais anasema tusitangaze kama kuna njaa. Mwenzake wa Kenya ameshatanga kwa raia wake. [Afu unasema ndo rais wa wanyonge).

Walisema sukari imefichwa kumbe ni uongo, bei imepanda mpaka sasa serikali imeshindwa kuishusha (inajinasibu ni serikali ya wanyonge, sijui wanyonge gani)

Tanzania ya sasa inatawaliwa ktk misingi ya udini {ukiristu} na ukanda

Zabuni za ujenzi Chato kapewa mtoto wa dada yake{afu unasema ndo rais tuliyemuhitaji}.

Mpaka sasa hakuna fedha za mfadhili yoyote iliyotolewa kusapoti bajeti yetu, Makusanyo yote ya ndani ya ndani yanatumika kulipa mishahara na madeni tu.

Pamoja na kubana matumizi , shilingi ya Tanzania imezidi kuporomoka dhidi ya Dollar ya marekani, na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa za kuinusuru

Na kila anaelalamika mnasema alikuwa mpigaji hata kama ni mjasiriamali aliekopa hela benki kufanya biashara zake halali.

Watu wamepiga hela za Lugumi, hakuna hatua zozote za kumwadhibu aliehusika.

Walituaminisha kwenye kampeni mwaka 2015, Lowassa ni fisadi. Wamejenga mahakama ya mafisadi. Mpaka sasa hawawezi kumkamata ilhali wana kila kitu cha kumkamata.

Serikali ya CCM imeishiwa Pumzi, inaelekea KUFA.

Si mzima wewe, ukapimwe akili
 
Waliodumaa akili ufipa wanafikili mabadiliko ni kuzungusha mikono tu, kisha mnarudi nyumbani kulala
 
Kuanzia Leo kwaheri UKAWA nimehamia Rasmi CCM kutokana Utendaji wa Rais Magufuli

Nawashauri Vijana wenzangu pia mnifuate huku tuepuke siasa za Kilaghai kwa kweli nilihadaika sana sasa nimeamua kujiunga CCM Rasmi.
Umefuata mtu sio sera vijana hawawezi kuchukua ushauri wako.... kwa hyo magu akistaafu siasa si ina maana utahama tena ccm??
Mkuu usiwe mfuasi wa watu simamia itikadi na sera maana watu wanapita ila sera na itikadi zikiwa imara husimama milele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…