Mh rais kiukweli heshima Mjini imeanza kurudi, wale waliokuwa wanatupita bila hata kutusalimia sasa hivi wanatusalimia, wale dada zetu waliokuwa wakikuona tu mbele yao wanajifanya wanaongea na simu, siku hizi wanatusalimia.
Amani mtaani imerudi waliokuwa wanatusumbua na sauti za Subaru zao kwa sasa wanaziendesha kwa heshima tena kwa wiki mara moja.
Kwa heshima Mkuu naomba ukaze tena kidogooooo ili wale ambao bado wanatusumbua mtaani na chenji zao ziishe ili tuwe sawa.
Naomba uwai kurudi kutoka ethiopia maana naona watu wameanza maneno maneno na vurugu, wengine wameshaanza kuangusha mpaka train yetu. Ukichelewa wanaweza ata angusha ndege yetu.
Mkuu bado kidogoooo.
Haya mabadiliko tuliyalilia muda mrefu ndani ya chama chetu.
Kidumu chama cha mapinduzi