Binafsi nimefurahishwa na kasi ya Dkt. Magufuli. Naamini wapo pia wengi wanaoungana nami katika furaha hii. Magufuli ameanza kwa kasi ambayo kama ataimaintain, Tanzania haimalizi miaka mitano itakuwa tayari ni nchi yenye kipato cha kati.
Hata hivyo wapo baadhi yetu ambao wanakejeli kasi hiyo. Hao kwangu ni watu waliozoea ubwete na bora liende!. Wanamwona Magufuli kuwa ni mtu atakayekuwa kauzibe kwao!
Wapigaji wote, wavivu wote na wazee Wa madili wote watamchukia Magufuli ila mi niseme na niwaombe tu kwamba tumpe support huyu jamaa kiukweli atatufikisha mahali Fulani!
Tuwafichue wote wanapanga kumhujumu (najua wanajulikana), tuwakatae kwani hawana nia njema na taifa letu.
Tumwunge mkono kukiuka katiba na sheria zilizopo? Yapo mazuri anafanya katika hilo hakuna atakayekataa kumwunga mkono. Lakini anapokosea halafu mnakimbilia kumsifia na kumwunga mkono huo upuuzi hauwezekani kwa watu waelewa. Huwezi kuapa, unamnyooshea Mungu biblia halafu unasigina ile katiba kwa makusudi, ukiambiwa unakuja juu.