Wanabodi,
Ni miaka miwili sasa, Mh. Rais anapambana katika kuimarisha mapungufu yaliyokuwepo katika vipindi vilivyopita. NINAONA HAJA YA KUMPONGEZA, hasa kwa kuzingatia JAMII FORUMS ni moja kati ya forum makini ambazo zinaaminika sasahivi duniani. Tumpongeze kwa mazuri aliyoyafanya na kama kuna mabaya, basi tutupie ushauri mzuri, naamini watatusikia. Nimewaza sana nikaona kauli yake hata kwa wanahabari Kagera imenitia moyo sana. ANATUPENDA, NA UKIMUANGALIA USONI, UNAONA KABISA ANAYASEMA KUTOKA ROHONI.
Ni vizuri, pamoja na kwamba kuna baadhi ya mambo yanatakiwa kuboreshwa zaidi na kurekebishwa, ni vizuri KUSHURUKU, KUPONGEZA na kuendelea KUSHIKAMANA katika kuitoa Tanzania hapa ilipo kwenda mbele zaidi. Leo ni miaka miwili ya uongozi wake, ukiweka kwa asilimia za kiutendaji, basi amepata zaidi ya hamsini. Hii ni ishara nzuri. Kikubwa zaidi kinachoonekana kwa haraka ni yale makubwa yanayowagusa Watanzania wote. Laini, maanin i baada ya miaka minne hivi jitihada zake zitaeleweka vizuri kabisa na wote tutaungana kwa pamoja.
Kama Upinzani wa Tanzania ungemuunga mkono kwa 100%, siamini kama leo nchi hii ingekuwa na sura ya kutokuelewana kama inavyotaka kuonekana huko katika majukwaa. Kauli mbalimbali zinazokinzana zisingekuwepo. UMOJA na MSHIKAMANO ungekuwa mkubwa zaidi. Sisi kama Watanzania, tujitafakari, hasa wenzetu ambao ni viongozi wa kisiasa maana ndio wanauwezo mkubwa wa kuwashawishi wafuasi wao kuyatii maagizo yao na kutuunganisha Watanzania.
NAMPONGEZA MH. RAIS, HAJASAFIRI KWENDA NJE YA BARA LA AFRIKA KWA MIAKA MIWILI SASA.