Poleni sana ambao nitawakwaza, Sawa mimi ni Mpinzani tena nina kadi
ambayo nimeilipia, lakini upinzani hauwezi kunifanya niwe Mnafiki na
kuuficha Ukweli.
Kipindi ambacho tuliteseka na kusaga meno hakuna aliyetujali, ni kipindi
ambacho Korosho ilikopwa na ikalipwa kwa awamu 3 mpaka 5, kilikuwa
ni kipindi kichungu sana sio tu CCM hata wapinzani wenzetu hawakuona
umuhimu wetu. Nikumbushe tu Tumewahi kukopwa Korosho na mpaka
leo hatujalipwa, wanaokumbuka wanakumbuka.....................
Leo wenzetu wengine naona munamsifia na kumpongeza Kikwete kuwa
alikuwa Bora, sawa ni haki yenu kwa sababu muliona manufaa yake.
Leo hii Tandahimba Tumemsimamisha Mbunge wa Upinzani Ndg. Katani A Katani
cha ajabu huyu ndiye Kinara wa ununuzi wa KANGOMBA tena mbaya zaidi ana
kashfa ya kununua korosho mbovu kutoka mkoa wa pwani....... sitaki kulizungumzia
hilo, wanaotuangusha na kutuletea matatizo kwa sasa ni viongozi wa vyama vya Msingi,
ushirika na viongozi wengine wa Halmashauri ambao wakibanwa vizuri matatizo
yatakwisha.......................... Mbunge wa CCM aliyepita ni mbovu, huyu wa upinzani hamna
kitu tena alikuwa na ushirikiano mkubwa kabisa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa
wa Mtwara ambaye muda huo alikuwa Kiongozi wa Chama kikuu cha ushirika. Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Mtwara na Mbunge wa Tandahimba CUF wameshirikiana sana kutuhujumu
Rais Dr.John Pombe Magufuli umeanza vizuri sana kwenye zao hili la Korosho
najua sio mtu wa kuokea Ovyo Ripoti za Kupikwa, KANGOMBA inahusisha baadhi
ya Vigogo. Kuwa SERIOUS na eneo hili la KANGOMBA ndio kwenye chanzo cha
matatizo yote haya ambayo yamebaki.
WAKULIMA WA KOROSHO TUNAKUKUBALI SANA, kipindi chako kifupi mabadiliko ni
makubwa sana.
YAANI UMEMGRADE MKOLMIJE KWA BEI YA KODO(KOROSHO)? NIKISEMA NA WEWE UNA AKILI KAMA BASHITE NITAKUWA NIMEKOSEA? HIVI UMEANGALI KADA NYINGINE ZINAVYOTESEKA? ENZI ZA KIKWETE PPF/NSSF ULIKUWA UNAPATA NDANI YA MWEZI,SASA HIVI UNAZIENYEA MWAKA MZIMA NDIO UNAKUJA KUPEWA NA MHUTU KASHAPITISHA KWAMBA KWA SASA HAKUNA KUTOA TUNASUBIRI ADONDOKE WINO TU.
UMEFIKIRIA MAKAMPUNI/WAFANYABIASHARA WALIOFUNGA BIZNESS ZAO? VIPI UMEFIKIRIA AJIRA ZILIZOPOTEA HAPO?
UMEFIKIRIA UNUNUZI WA MELI BOVU LA BILIONI 8 AMBALO NI SCREPA NA LIJAWAHI KUTUMIKA? BILIONI 8 ALIZOPIGA MUHUTU VIPI?
UMEFIKIRIA HASARA TULIZOPATA KWA KUNUNUA BOMANDIA NA HASARA YA ATCL? HIYO MITRILLIONI ILIYOPOTEA KWELI ISINGEWEZA KUFANYA JAMBO LINGINE?
UMEFIKIRIA HARASSMENT WALIYOFANYIWA WAFANYABIASHARA WAKUBWA KWA SABABU ZA KISIASA? ONA SOKO LA MBAAZI LILIVYOSHUKA,ONA GHARAMA ZA UJENZI ZILIVYOPANDA,ONA WAFANYABIASHARA WALIVOONDOKA TZ KWA CHUKI/VISASI VYA KISIASA.
UMEFIKIRIA WAKAZI WA KIMARA WALIOBOMOLEWA MAJUMBA YAO? UMEFIKIRIA WALIOFUKUZWA KWA VYETI FEKI NA KUDHULUMIWA MAFAO YAO? UMEFIKIRA KWELI AU UMEANGALI BEI YA KOROSHO TU? HILI SWALA LA VYETI WATU WALIOFUKUZWA TUPO NAO MTAANI,UKIMTAJIA MUHUTU ANAWEZA KAUPA KERBU,WANATESEKA SANA,UMEWAFUKUZA BASI WAPE MAFAO YAO BASI.
UMEFIKIRIA WAZAZI,NDUGU WALIOPOTEZA WAPENDWA WAO KWA AWAMU HII YA 5? BEN,AZORY,MADIWANI WAMEUAWA KIPINDI HIKI,UMEFIKIRIA UMINYWAJI WA HAKI YA KUJIELEZA/MAONI? UMEFIKIRIA UKANYAGWAJI WA KATIBA? HIVI UMEFIKIRIA KWELI AU UMEWAZA KOROSHO KAMA MUHUTU NA PDH FEKI YA MAGANDA YA KOROSHO?
KUUUA WAPINZANI SIO SOLUTION,UKIUA MMOJA ANAIBUKA MWINGINE TENA WANAIBUKA KWA KASI YA AJABU,MMEMPOTEZA BEN,LEO KUNA MDUDE,KUNA MALISA,KUNADWASON,KUNA NONDO,KUNA MTATIRO,KUNA ETC LIST NI NDEFU,JE MTAWAMALIZA WOTE HAO?