Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Bangi mbaya sana,utakuta na wewe unalalamika hakuna uhuru wa kujieleza na kutoa maoni
 
Hahaha ngoja nicheke tu kwa pongezi hizi unafikiria uzi utaachwa ?
 


Kwa nini usianzishe thread yako? Unachanganya mada sasa
 
Mfyuuuu
 
Hahahaaa, Daaah watu wamepinda jamani, jiwe linapongezwa
 
Kwa akili zako mtoa mada, inaonesha bado una safari ndefu sana kujikomboa kifikra.
Hivi ni nchi gani unaweza toa upuuzi huu na ukaangaliwa tu?
 
Endelea kuogopa , kuna mijamaa mibabe imeanza kunyanganya chochote ulichonacho.
 
Nafurahi kusema kwa hakika kuwa Tanzania mpaka sasa ilishavuka vikwazo vyote. Tanzania ya sasa inajitambua. Wezi wote na mafisadi wanaogopa kuiba (siyo kama enzi zile). Nchi sasa imetulia. Vikundi vya kiharifu (vya kisiasa, dini etc) vinajitahidi kupiga kelele ili inchi irudi kwenye mfumo wa kifisadi, ila serikali imekaza. Mungu ambariki sana Dkt Magufuli.
 



Ni sawa,maoni yako ni oni la mtu mmoja tu kati ya watu milioni 60 kwenye hii Jamhuri!

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jana tarehe 02/04/2018 tumeshuhudia ndege yetu aina ya Bombadier Q400 Dash 8 iliyokuwa imeshikiliwa nchini Canada ikikanyaga ardhi ya Tanzania baada ya kuachiwa kutokana na Kampuni ya Stirling Civil Engineering Limited kutokuwa tayari kuendelea na kesi iliyokuwa imefunguliwa dhidi ya Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo kufikia maamuzi ya kuondoa kesi hiyo mahakamani.

Baadhi ya watanzania ambao ni watetezi wa madhalimu kwa maslahi yao binafsi na bila kutanguliza uzalendo kwa taifa lao, mara kadhaa tumeshuhudia wakitafuta kila namna ya kuikwamisha serikali inayoongozwa na Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isifanikiwe kwa kile ambacho tumeona ikipigania kutafuta uhuru wa kiuchumi wa taifa letu la Tanzania.

Tumeona kazi iliyofanywa kulinda rasilimali zetu za madini, tumeona jitihada za kufufua shirika letu la ndege, miradi ya ujenzi wa reli ya standard gauge (SGR), mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa Stigglers Gorge, kuziba mianya ya upotevu wa fedha za serikali, kubana matumizi yasiyo ya lazima, kuboresha utendaji kazi serikalini na mengine mengi ambayo siwezi kutumia siku mmoja kuyataja. Mheshimiwa Rais anapaswa kuungwa mkono na kila mtanzania bila kujali itikadi za vyama. Na huu ndio uzalendo.

Tumeona baadhi ya wanasiasa wanaopinga kila kitu wakijiita eti wapinzani, wakikosoa kila jema linalofanyika na hata kutafuta njia za kutukwamisha. Niwaeleze tu hawawezi kuzuia mkuki kwa mkono!

Wanasiasa hawa walitamani kuona na walifanya kila jitihada kuhakikisha ndege yetu haiachiliwi ili wapate cha kuwalaghai wananchi, wameshindwa! Wapinzani hawa uchwara kwa sasa hawana sehemu ya kupumlia, wamebanwa, mbavu zinawauma!

Nimemsikia ndugu Humphrey Polepole, Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi Taifa (CCM) wakati akitoa salamu zake za chama katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la usimikaji wa rada, pamoja na mambo mengine, alitanabaisha kuwa nchi yetu ilikuwa imejaa madhalimu na wanyonyaji wa wanyonge, na akipatikana mtu mmoja kwa ajili ya kuwatetea wanyonge hao lazima atapingwa na madhalimu na watetezi wa madhalimu kwa kila namna.

Niwaombe watanzania tusimame pamoja na Magufuli

Mimi nasimama na Magufuli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…