JPM NI ZAIDI YA TUMJUAVYO
Niungane na Watanzania Wengi kwanza Kumshukuru Mungu kwa Kutuinulia Ndugu John Pombe Magufuli, kama Mwenyekiti wa CCM Taifa, Sidhani kama katika Wakati Huu tunaweza Kuwa na Mtuwa Aina yake, Wengi wananielewa ninachomanisha.
TATU BOMBA
Katika Maisha ya Siasa nimejifunza kuwa UZOEFU ni Muhimu, lakini Hauwezi kuzidi Ubunifu , Uweledi, Uthubutu na Utashi wa Kisiasa.
Ingizo la Ndugu Mizengo Peter Pinda waziri Mkuu Mstaafu, na Ndugu Makongoro Nyerere sikuelewa Vizuri, ila alipopendekeza Jina la Ndugu Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM nilielewa huu utatu mtakatifu.
KWANINI HAWA WATATU
Tuanze na Ndugu Pinda , ukitazama viongozi wakuu wenye Umri, uzoefu na uadilifu ambae mienendo yake hata baada ya kumaliza kazi ya Uwaziri Mkuu utakubaliana na mimi kuwa Ndugu Pinda ni ingizo Sahihi ukiwaacha Marais wastafu, sisemi ni Bora kuliko wengine lakini Haiba yake inahitajika zaidi katika kushikilia Dhana ya Uzoefu kwenye Chama na Serikali, Uwepo wake utaisaidia CCM kwa miaka 10 ijayo.
Ndugu Makongoro Nyerere, wengi bado wanauliza Kaingia kufanya nini? Kwa wanaomjua Makongoro katika Siasa za UDAMBWIUDAMBWI, kama hunielewi Jiulize Kwanini Ndugu Wasira bado ana Nguvu kwenye CCM japo alikosa Ubunge kule Bunda, Sina maneno ya kuwaelezea hawa watu ila itoshe kusema kuwa CCM inahitaji watu wa Aina ya Makongoro ambao Wamezaliwa na kukulia ndani ya Misingi ya Chama cha Mapinduzi.
UJIO WA DKT. BASHIRU CCM
Ndugu Magufuli kama Ni kwenye Mpira wa Miguu amemudu kuucheza na kumaliza Dk 90 akiwa Nyota wa mchezo.
Ujio wa Dkt. Bashiru kama Katibu Mkuu wa CCM unasadifu Mambo Muhimu yafuatayo :-
1. Chama kimeanza kujenga safu ya Utendaji wa watu wenye Uweledi wa Modern Politics siasa za kisasa zinazohitaji Hoja na Sio kelele, Dkt. Bashiru kama wengi wakivyosema wamefundishwa nae Siasa pale Udsm na mimi nikiwa Mmoja wapo 2003-2006 , mbali na kuwa mwalimu wa Sayansi ya Siasa jambo zuri ni kuwa yeye ni Muumini wa Siasa za kumkomboa mtu Mweusi katika Umajumui wa Maendeleo.
CCM imeanza Kurudisha Misingi ya kuanzishwa kwake chama cha Wakulima na Wafanyakazi (hapa kwa Wafanyakazi ni pamoja na wafanyabiashara au mtu anaefanya kazi halali ya kumuingizia kipato) ambacho kinaanza Kuwavutia Wasomi wa Kati, kawaida na wale wa kiwango cha Juu.
2. Ccm Inaanza kuonekana kwa vitendo kuwa ni chama Cha Wote ili mradi uwe na Uweledi na Maarifa ya Kuongoza, haijalishi ulikuwa Nani Ccm Utapata fursa ya kusimama na Kuongoza, Hili limetimia kwa Dkt. Bashiru ambae mimi nimemjua mwaka 1998 akiwa mwenyekiti wa Tawi la Ccm Abiyani pale Ubungo, na zaidi ya Hapo wengi wamekuja kumuona akiwa Mwenyekiti wa Tume ya kuhakiki Mali za CCM , hakuwa mtu maarufu au Mashuhuri ndani ya CCM
Hii ni Karata nzuri katika Kuwaaminisha wananchi kuwa Ccm sio mali ya mtu au kikundi fulani Bali ni Bidii na maarifa yako tu, sasa naamini watu ambao ni Wasomi watagombea nafasi ndogo na za kawaida mfano kata z matawi, Wilaya na Mkoa.
3. Ujio wa Dkt. Bashiru unatoa fursa ya kuanza kushughulikia tatizo SUGU la matumizi mabaya ya RASILIMALI za Chama, yeye amezunguka Karibu nchi nzima ameona chama kikoje na kina nini, katika siasa za sasa suala la kujiimarisha KIUCHUMI ndio Agenda kubwa ambayo itaendelea kuleta Uhai wa chama mana uko mbeleni naona kila dalili ya kuondolewa au kupunguzwa kwa Ruzuku kwa Vyama vya Siasa mana zinatafunwa tu kama fedha za Capacity Charge kwa IPTL, Songas na Richmond.
HITIMISHO
Naomba nihitimishe kwa Kuwatazama watu wawili wakubwa kwanza ni Wana CCM wenzangu, na pili Dkt. Bashiru
Ndugu zangu wana CCM Tumepata Katibu Mkuu Mweledi, Mbunifu na Msomi najua wako *Majeruhi* baadhi waliofisadi Mali za chama najua hawa hawatamtaka kabisa Dkt. Bashiru watamkwamisha kila kona na kumuhujumu , mimi nasema hao mafisadi ni wachache sisi wanachama ni wengi hivyo mkae kimya kwa sasa muacheni Katibu Mkuu mpya afanye kazi, najua mtaibuka na Agenda zenu mfu kuwa Hakijui chama na Sio mzoefu, ila mjue siasa zimebadilika sasa ni siasa za hoja na Sio Matusi au kushambuliana, lakini mwenyekiti alishasema anataka kujenga Ccm mpya ndio hii sasa.
Kwako Dkt. Bashiru, wewe kwangu ulikuwa Mwalimu tuliona misimamo yako, hukuogopa na tunaamini uku utaendeleza zaidi.
Yako Mambo Mazuri unapaswa kujifunza kutoka kwa Mtangulizi wako Ndugu Kinana, yeye alikuwa kama Kisima Jangwani chukua Mazuri yake, endeleza pale alipoishia ila kubwa Endelea Kujenga Umoja , Mshikamano,UTII na uadilifu kwa Chama na wanachama, Wasaidie wenzako kufanya vizuri, na wale wanaofanya vizuri waendeleze wafanye vizuri zaidi na zaidi , Naamini katika Wewe, tutamuona Mwalimu Nyerere kwenye Chama, mana tumeshamuona Serikalini kupitia Dkt. John Pombe Magufuli.
Jua pia kuna wanafiki Wachache sana japo wana Vinguvu kwa Kiwango cha PhD
Usiyumbe Wala Kuyumbishwa
Wako katika Uzalendo
Jerry C. Muro