Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Unadhani hivyo viwanda anavyopigia kelele kila siku ni kwa ajili ya ajira ya Jesca? vijana wengi watapata ajira humo au ulitaka awaajiri vijana wapi kwa mfano, kama huna sifa utaajiriwaje, kucha kutwa mnabeti mnatoka na GPA za 32 nani akuajiri.
Wape makavu Aisee
 
Katika Historia ya Dunia toka iumbwe Tanzania ndio Taifa lililowahi kuwa na Watumishi hewa wengi....Walikua 20,000, Walikua wakilipwa mshahara wa wastani Bilioni 226 kwa mwaka Tunaposema Hewa ni watu ambao hawapo, ni Majina aidha Feki au ya Waliofariki lakini yapo kwenye Payroll, Fedha zinaingia Mifukoni mwa Makanjanja wachache, wanapiga, Achilia Mbali Mshahara, hizo Hewa zilikua zikilipwa mpaka Fedha za Likizo, House Allowances, Overtime, Posho za safari n.k

NOTE : Utasikia Nyumbu inasema Namchukia Magufuli kweli, Maisha yamekuwa Magumu".View attachment 858398
Unamtetea kichaa mwenzio ?
Ndio maana mnahamia dodoma ili muwe karibu na milembe
 
Eideed,

..sera za uchumi za Mwalimu na Sokoine zilifeli.

..Sasa badala ya wao kukubali kuwajibika, walitafuta KISINGIZIO.

..kisingizio ilikuwa uchumi wetu umeporoshwa na WAHUJUMU UCHUMI na WALANGUZI.

..Lakini ukweli ni kwamba Walanguzi na hao walioitwa Wahujumu Uchumi walikuwa ni matokeo ya sera uchumi zilizoshindwa na siyo chanzo.

..Mwalimu Nyerere na Sokoine waliunda mahakama ya wahujumu uchumi.

..Lakini watuhumiwa wengi waliofikishwa ktk mahakama hiyo walikuwa wamekamatwa na kusota mahabusu kabla bunge halijapitisha sheria ya uhujumu uchumi.

..Tawala zinazozingatia haki za binaadamu na utawala bora, hupitisha kwanza sheria, halafu baada ya hapo hukamata wale watakaovunja sheria hiyo.

..Kipindi ambacho Sokoine alikuwa Waziri Mkuu hali ya uchumi na maisha kwa ujumla ilikuwa ngumu kuliko kipindi chochote kile ninachokikumbuka mimi.

..Watanzania wa leo hawawezi kuvumilia shida tulizovumilia sisi wakati wa Sokoine.

Cc chige, Pascal Mayalla
 
Nyie hamjaelewa kitu kimoja.
Magufuli anaongea hiki ila anafanya kile.

Kama hujaelewa hutokaa uelewe mpaka yakukute
 
Eideed,

..sera za uchumi za Mwalimu na Sokoine zilifeli.

..Sasa badala ya wao kukubali kuwajibika, walitafuta KISINGIZIO.

..kisingizio ilikuwa uchumi wetu umeporoshwa na WAHUJUMU UCHUMI na WALANGUZI.

..Lakini ukweli ni kwamba Walanguzi na hao walioitwa Wahujumu Uchumi walikuwa ni matokeo ya sera uchumi zilizoshindwa na siyo chanzo.

..Mwalimu Nyerere na Sokoine waliunda mahakama ya wahujumu uchumi.

..Lakini watuhumiwa wengi waliofikishwa ktk mahakama hiyo walikuwa wamekamatwa na kusota mahabusu kabla bunge halijapitisha sheria ya uhujumu uchumi.

..Tawala zinazozingatia haki za binaadamu na utawala bora, hupitisha kwanza sheria, halafu baada ya hapo hukamata wale watakaovunja sheria hiyo.

..Kipindi ambacho Sokoine alikuwa Waziri Mkuu hali ya uchumi na maisha kwa ujumla ilikuwa ngumu kuliko kipindi chochote kile ninachokikumbuka mimi.

..Watanzania wa leo hawawezi kuvumilia shida tulizovumilia sisi wakati wa Sokoine.

Cc chige, Pascal Mayalla
Laki je,
Hatustahili kuwa na Maendeleo mithili ya Korea ya Kusini?
 
Eideed,

..sera za uchumi za Mwalimu na Sokoine zilifeli.

..Sasa badala ya wao kukubali kuwajibika, walitafuta KISINGIZIO.

..kisingizio ilikuwa uchumi wetu umeporoshwa na WAHUJUMU UCHUMI na WALANGUZI.

..Lakini ukweli ni kwamba Walanguzi na hao walioitwa Wahujumu Uchumi walikuwa ni matokeo ya sera uchumi zilizoshindwa na siyo chanzo.

..Mwalimu Nyerere na Sokoine waliunda mahakama ya wahujumu uchumi.

..Lakini watuhumiwa wengi waliofikishwa ktk mahakama hiyo walikuwa wamekamatwa na kusota mahabusu kabla bunge halijapitisha sheria ya uhujumu uchumi.

..Tawala zinazozingatia haki za binaadamu na utawala bora, hupitisha kwanza sheria, halafu baada ya hapo hukamata wale watakaovunja sheria hiyo.

..Kipindi ambacho Sokoine alikuwa Waziri Mkuu hali ya uchumi na maisha kwa ujumla ilikuwa ngumu kuliko kipindi chochote kile ninachokikumbuka mimi.

..Watanzania wa leo hawawezi kuvumilia shida tulizovumilia sisi wakati wa Sokoine.

Cc chige, Pascal Mayalla
Umeingia deep sana mkuu.... Nimepata kitu
 
Rais John Magufuli ameingia kwa kishindo mkoani Mara, aking’aka baada ya kubaini mradi wa maji Bunda, haujakamilika tangu ulipoanzishwa miaka minane iliyopita.



Hilo lilimfanya Rais amkumbuke Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere na kusema, angetokea leo, basi hata yeye angeshangazwa kusikia mradi huo haujakamilika.
Rais Magufuli ambaye alianza ziara yake Mara, akitokea Mwanza, amewataja mawaziri waliosimamia wizara ya maji katika kipindi cha miaka minane iliyopita na kusema:



“Wakati kuna mawaziri walikuwepo tangu wakati huo zaidi ya watatu, Lwenge, Magembe, Kamwelwe na sasa Mbarawa,”alisema.
Aliongeza: “Inashangaza, Nyerere atamshangaa hata huyo mkandarasi, wanabebana si ndiyo, wanabebana si ndio, wataachiana. Nasema wataachiana, naomba hilo mniachie hili nalibeba mimi mwenyewe. Kama mkandarasi mshenzi, mimi mshenzi zaidi, kama ni kufukuza watu wafukuze, kama ni kuwatumbua, watumbue.”



Magufuli aliyasema hayo baada ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, Simona Mayaya kumuomba Rais kuingilia kati tatizo la ukosefu wa maji linaloukabili mji huo.
Rais Magufuli alimtaka mkuu wa mkoa kufanya kazi na wakandarasi na ameahidi kumtuma waziri wa maji na katibu mkuu wizara hiyo kusimamia suala hilo.



“Nataka kuahidi maji Bunda lazima mpate. Hamuwezi kunichagua bure, halafu mimi nisiwasaidie,” alisema.
Mradi wa kupeleka maji kwenye mji wa Bunda kutoka ziwa Victoria katika eneo la Nyabeho ulisanifiwa mwaka 2006 na ulikuwa unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha za maendeleo.



Mayaya alipoulizwa ni kampuni gani ya ukandarasi inayohusika na ujenzi wa mradi huo aliomba kusaidiwa na mkuu wa mkoa.
Jibu hilo lilimfanya rais Magufuli amuite Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima ambaye alieleza kufahamu kuhusu sakata hilo na kueleza kuwa hatua zimeanza kuchukuliwa.



Alieleza kuwa hata Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika wilayani humo alikuta sintofahamu hiyo na ikaamuliwa kuvunjwa kwa bodi ya Mamlaka ya Maji safi ya Musoma (Muwasa) na aliyekuwa mkurugenzi wake Mhandisi Gantala Said akikamatwa na kuhojiwa na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Ruswa (Takukuru).



Baada ya kusikia maelezo hayo Rais Magufuli akahoji sababu za mradi huo kutoendelea na kama mkandarasi ana uwezo wa kuukamilisha.
“Kwa hiyo siku zote hizo mnaendelea kuchunguza, kwanini msihakikishe mradi unakamilika na watu wanapata maji. Kwahiyo na wewe mkuu wa mkoa unachunguza? Haya sasa niambie mkandarasi ana uwezo wa kukamilisha mradi huo ndani ya muda gani,”alisema



Aliongeza: “Mkandarasi alikamatwa ila ametolewa nje kwa dhamana na jinsi ninavyomuona hawezi kumaliza mradi huu na fedha zote alishalipwa hivyo tumemuomba waziri tuvunje mkataba.”




Kutokana na maelezo hayo rais Magufuli aliagiza waziri wa maji na katibu mkuu kwenda wilayani humo na kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo ili maji yaweze kupatikana.



Rais Magufuli pia alizungumzia sakata la mwekezaji anayefahamika kwa jina la Magoma anayewataka wakazi wa kijiji Kinyabwiga kuhama kwa kile anachodai ana leseni ya kuchimba madini.



Wakiwa na mabango yanayolalamikia kunyang’anywa ardhi, wananchi hao walidai kuwa hawana pa kwenda baada ya mtu huyo kuwataka kuondoka katika maeneo yao ndani ya siku saba.



“Huyo Magoma agome mwenyewe hakuna wa kumtoa mwananchi kule, RC, DC kama ulimleta wewe mwambieni atoke,”



“Akitaka kuwahamisha awalipe kwa fedha mnazozitaka ninyi hawezi kujiamulia kwas ababu ana leseni kwani hayo madini aliyazaa yeye,”alisema.



Wakati huo huo, Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, kumsimamisha kazi Kamishna wa Ardhi wa kanda, Bunda kwa kushindwa kumrudishia kiwanja anachodai kudhulumiwa, mwanamke mmoja mkazi wa Bunda.



Awali mkazi wa eneo hilo, ambaye hakujitambulisha jina alilalamika mbele ya Rais Magufuli kuwa alikuwa na viwanja viwili na kimoja, kimechukuliwa na tajiri mmoja.
Pamoja na kutoa maagizo hayo, pia Rais alimpa mkazi huyo, Sh 500,000 ili zimsaidie.



Katika hatua nyingine, akiwa eneo la Mwisenge, Musoma, Rais Magufuli alizungumzia mgogoro kati ya wakazi wa eneo hilo na mkandarasi wa kampuni ya Nyakinyang’ari wa kujenga mradi wa maji Bunda.
Rais Magufuli alisema ana taarifa kuwa mtu huyo amevikamata vyombo vya dola ndiyo sababu anafanya mambo yake anavyotaka.



“Nimepata taarifa ni mwana CCM na amevishikilia vyombo vya dola hapa sasa nasema uhalifu hauna chama sheria ichukue mkondo wake, haiwezekani ndani ya miaka minane mradi unasuasua halafu viongozi wangu niliowateua wapo tu wanamuangalia anadunda




“Sasa nitawageukia nyinyi ili wananchi wasiendelee kuteswa kwa kukosa maji, nitawatesa nyinyi,”
“Mliopa nataka mumnyang’anye apewe mwekezaji mwingine na ikiwezekana alipe fedha zote za miaka 10 ambayo amezuia hoteli kufanya kazi. Hivi huyu ni mtu wa aina gani alipewa mradi wa maji Mugumu akashindwa akafukuzwa,”alisema



Awali, mkazi wa eneo hilo, Edwin Wilson alisimama na kumwambia Rais Magufuli kuwa Hoteli ya Musoma ilikuwa inawasaidia kwa mambo mengi ikiwamo ajira lakini mwekezaji mpya aliyeinunua anazuia hata watu kuingia.
“Hoteli ya Musoma ilikuwa inatulisha pamoja na kutoa ajira lakini sasa tunazuiwa hata kuingia ziwani,’’ alisema.




Rais Magufuli alisema mwekezaji alipewa hoteli hii miaka kumi lakini hakuna alichokifanya.
Rais Magufuli pia aligusia suala la mkuu wa wilaya ya Musoma la kuwatishia kuwaweka ndani wanakijiji wa Mwisenge endapo wangebeba mabango wakati wa ziara yake.
Alieleza kuwa wananchi hao walikuwa wakilalamikia kitendo cha mmiliki wa hoteli ya Musoma kuzuia njia ya kwenda ziwani hivyo kuwalazimu kuzunguka umbali mrefu kufikia eneo la ziwa.



“Nina taarifa za tishio la Dc kwa wananchi, yani yeye yupo ndani ya ofisi ina bendera ya nchi sasa anataka kuwaweka wananchi ndani ili wasieleze kero zao, taarifa zote ninazo sitaki watanzanioa wateseke ninachowaambia sasa katizeni hapo hapo kwenye hoteli nendeni mkaogelee ziwani,”



“Ninyi ndio mmeniwezesha kuwa Rais msingenichagua nisingekuwa Rais, nawaagiza watendaji, wakuu wa mikoa, makamanda wa polisi na wakurugenzi kuanzia sasa hawa watu wasizuiwe kwenda ziwani, haiwezekani,” alisema.



Alisema eneo hilo lipo wazi na wananchi wanaweza kufanya shughuli zao hata wakitaka kuifanya fukwe.
Akizungumza katika uwanja wa Mukendo, Musoma, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima alisema katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, kero kubwa mkoani wilayani Musoma ni maji.




Hata hivyo amesema kutokana na utekelezaji wa ilani ya CCM, mradi wa maji wa Mugango utasainiwa katika wiki mbili zijazo.
“Umetupa bilioni 3 tumeboresha vituo vya afya saba wilaya za Tarime, Rorya Bunda, Serengeti na Butiama. Miradi ya Barabara ikimalizika itafungua fursa kiuchumi,”alisema



Alisema kuna mikakati ya kuboresha kilimo cha pamba kutoka kuzalisha tani 6000 hadi tani 60,000 na msimu uliopita mkoa umefanikiwa kuzalisha tani 20000.
Akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Musoma Vijijini, Sospeter Muhongo amemkumbusha Rais kuwa hii ni mara ya pili kwa Rais Magufuli kwenda mkoani humo katika kipindi cha miaka mitatu.
“Umekuja hapa tulipofanya kampeni na Mzee Warioba,” alisema.



Mawaziri wazungumza

Alipoulizwa kuhusu kukosekana kwa maji Bunda, aliyekuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge alisema waziri wa maji ndiye anaweza kuzungumzia suala hilo huku akihoji kama waziri anaweza kupeleka maji bila nguvu ya Serikali.



“Mtafute waziri wa maji ndiyo azungumzie hilo. Lakini waziri anawezaje kupeleka maji bila nguvu ya Serikali? Sasa si mtatafuta hata mawaziri waliokufa,” alisema Lwenge ambaye pia ni mbunge wa Wanging’ombe.



Kwa upande wake Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa alieleza kusononeshwa kwake na kusuasua kwa mradi wa maji wa Bunda na kuahidi kuchukua hatua kwa makandarasi wote wasio waaminifu.



“Mkandarasi huyu si mwaminifu na wala hana uungwana amekuwa akichukua fedha halafu hafanyi kazi, kuanzia sasa tutawachukulia hatua na kuhakikisha maji yanapatikana katika mji wa Bunda,”alisema.
 
Kwa kipindi cha miaka mitatu ya utawala wa Rais Magufuli ni dhahiri wazi kiongozi huyu ameonyesha ujasiri wa hali ya juu kama alivyokuwa Hayati Edward Sokoine.
Wakati Rais Magufuli alipoanza kasi ya kupambana na ufisadi wananchi wengi walitegemea ingekuwa ni vita vya muda mfupi lakini ni wazi Mheshimiwa Rais Magufuli amedhamiria kufuta ufisadi wote hapa nchini. Kwasasa nakubali Mheshimiwa Rais Magufuli amechukua hatua ama njia ambayo Hayati Edward Sokoine aliyotaka kuifuata wakati akiwa Waziri Mkuu kabla mauti haijamkuta mwaka 1984.
Uko sahihi kabisa mkuu.Ndio maana mauti ilimkuta Sokoine.Hata hivyo upinzani mkubwa anaokumbana nao Magufuli ni kwa sababu Watanzania walio wengi wamekulia kwenye mazingira ya kifisadi,kwa hiyo haya anayoyafanya ni mapya kwao na hivyo ni vigumu kuyakubali.
 
SUBHANNAH ALLAH....!!!!!!!

Mmevuka mipaka sasa!


Mungu huyu huyu huyu wa Isaka na Yakobo?
 
Wajiangalie tu wasijekuzua kesi nyingine na huyu mkandarasi tukanyang'anywa uwanja wa taifa.
 
Mambo mengine unatakiwa usikilize uache hapo hapo kwasababu yanakua na maswali mengi kuliko majibu na majibu hakuna kwasababu ni taarifa za upande mmoja.
 
Binafsi nimefurahishwa na kasi ya Dkt. Magufuli. Naamini wapo pia wengi wanaoungana nami katika furaha hii. Magufuli ameanza kwa kasi ambayo kama ataimaintain, Tanzania haimalizi miaka mitano itakuwa tayari ni nchi yenye kipato cha kati.

Hata hivyo wapo baadhi yetu ambao wanakejeli kasi hiyo. Hao kwangu ni watu waliozoea ubwete na bora liende!. Wanamwona Magufuli kuwa ni mtu atakayekuwa kauzibe kwao!

Wapigaji wote, wavivu wote na wazee Wa madili wote watamchukia Magufuli ila mi niseme na niwaombe tu kwamba tumpe support huyu jamaa kiukweli atatufikisha mahali Fulani!

Tuwafichue wote wanapanga kumhujumu (najua wanajulikana), tuwakatae kwani hawana nia njema na taifa letu.

Habari zaidi, soma =>Toka kwa Wananchi: Kero na Vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa...
Kichwa cha habari tu kimetosha kunichefua kama nikweli usemalo kwanini katoa bunge live na mikutano yasiasa basiingekuwa kila baada ya mwaka anaficha nini tusijuwe watz angalau ingekuwa ndani ya siku 7 zamwisho wa bajeti iliyopangwa kuisha tungejuwa niwapi tunakwenda tupo kama kwenyesanduku alafu tunasifu tu ila Mimi sinachama ninaipenda tz tu
 
Back
Top Bottom