Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Schwulen-Jagd in Tansania: »Menschenrechte werden eingehalten

Rais Magufuli naomba kukuuliza mabalozi wetu wa Germany, Belgium na Uholanzi wako wapi? Na wanafanya nini? Mbona siwasikii wakikanusha habari hizi ambazo zinaipaka matope serikali yako?

Ina maana hao mabalozi hawana watumishi wanaojishughulisha na mitandao ya mataifa huko waliko kiasi kwamba ubalozi ukakanusha yanayo andikwa?

Kuna tatizo serikali kuinadi Tanzania nje? Au ndiyo tuseme, watendendaji wa serikali kama hao mabalozi hawajui umuhimu wa wao kuwa representarives wa watanzania katika mataifa wanayo tuwakilisha?

Hii hali inawasikitisha na kuwafanya watanzania walioko nje wasijisikie vizuri kwa taarifa ambazo sio za kweli ambazo mitandao ya wazungu ina publish kuhusu nchi yetu na serikali yake. Watanzania wamekuwa harassed na marafiki na majirani zao kuhusiana na taarifa kama hizo. Kwa hali hii ingekuwa kitu cha busara kama serikali ingechukua hatua kuhusiana na upotofu wa hizi habari. Ni mani anajishughulisha na vitendo viovu hivyo vya kupotosha taswira ya nchi yetu?

Naomba serikali isimwache RC Makonda aendelee na ujinga wa kuwasaka mashoga, yeye aelewe kuwa sio Mungu hata yeye ana upungufu wake, na ndiyo maana haja weza mpa mimba mkewe akamzalia mtoto. Maamuzi kama hayo yana sababisha ionekane kuwa Tanzania inatawaliwa na Rais ambaye ni dikteta na hivyo kuwafanya wadau kuogopa kuwekeza nchini kwa kuhofia mapinduzi ambayo yatawafanya wao mwishowe wapoteze Investments zao.

RC Makonda anatakiwa aelewe kuwa kila binadam ana vitu vyake maalum vya kumpa nguvu ili aendelee kuishi na kufanya kazi kulingana na uwezo wake ambao mwenyeezi Mungu amemjalia. Kama ushoga kwake ni faraja, basi hatuna budi sisi kumzuia au kumharass kama hamdhuru binadam mwenzake. Si mwili wake na starehe yake kwa mapenzi yake na mungu wake? Kama binadam nani katupa sisi mammlaka ya kumwingilia mtu maisha yake?

Rais Magufuli wewe ni mwana sayansi tena wa chemistry na unajua fika kuwa binadam yeyote yule anakuwa controlled na hormones, na hormones sio kitu kingine mbali na chemistry, kwanini sasa unashindwa kutambua kuwa hormones ndiyo zina wafanya hao mashoga ku-behave kama walivyo?

Rais Magufuli naomba utambue kuwa hakuna mtu ambaye yuko parfect na hata wewe una mapungufu yako mengi, ambayo yanaonekana dhahiri kwa mfano, huwezi zungumza kiingereza vizuri na hata kiswahili chenyewe hukiwezi vizuri japo kuwa umezaliwa na kukulia Tanzania na vile vile una handcape katika mahusiano na watu, huja jaliwa kuwa na kipaji cha kuwa diplomat, kwa kusema ukweli, lakini pamoja na hayo watanzania wamekupenda na kukuchagua wewe kuwa kiongozi wao kwa sababu kuna vitu ambavyo unavitenda vizuri sana kwa watanzania na nchi yako kwa ujumla, kiasi kwamba watanzania wakawa na imani na wewe na kukuchagua kuwa Rais wao.

Tukiwa wakweli kama wewe mwenyewe kila mara unavyo dai kuwa mkweli, basi ujue kuwa wewe pia kama binadam huna sifa nzuri za kuwa kiongozi wa nchi kwa tabia na mwenendo wako, lakini upendo wako kwa binadam wenzako na matendo yako ni thamani kubwa sana kwa watanzania na ndiyo ni vigezo vikubwa vinavyo kupa sifa na kukufanya wao wakuone kama mwokozi wao.

Mwambie Makonda aache tabia ya kuwa harass binadam wengine. Mawazo hayo ya kuwa nyanyasa homosexuals ni mawazo ya kinyama ni mawazo ambayo yanarudisha nyuma maendeleo yetu. Makonda asitafute kiki kwa kuwanyima binadam wenzake amani na kuwapa hofu ya kimaisha. Ni vizuri akatambua kuwa binadamu tuna maumbile tofauti. Kuna binadam ambao wamezaliwa wakiwa na mwili wa kiume lakini wana viungo vya kike. Kuna watu wana penis, vagina na anus vyote pamoja, sasa watu kama hawa wafanye nini wakati huyo mwenyeezi Mungu ambaye RC Makonda na wewe Rais Magufuli mnamwabudu amewaumba hivyo? Ina maana wao sio binadam? Je, hawastahili kuishi? Kwani wao wanatofauti gani kati yao na Albino? Au sisi na Wazungu?

Kama sisi hatupendi kufanyiwa vitu ambavyo vinatufanya tunyanyasike, basi nasi tusiwe wa kwanza wa kuwa nyanyasa wengine kwa mapungufu yao ya kimaumbile. Kama RC Makonda ana amua kuwa harass watu wenye maumbile na tabia ambayo ina wafanya wao wapate raha za dunia kwa namna ambayo ni kinyume na sisi wengine basi nasi tuanze kwake, kwani na yeye kwa denifinition ya mwanamme sio mwanamme, kwani mwanamme timilifu lazima ammpe mimba mwanamke ili amzalie mtoto. Sasa kwa vile yeye anashindwa kufanya hivyo toka aoe, basi na yeye pia ajitambue kuwa hajakamilika. Naye akapimwe kama anauume kweli.

Mimi nafikiri katika karne hii ya 21 wengi wetu tumepanuka mawazo kwa hiyo hatuna budi kupoteza mda, akili na nguvu zetu kwa mambo ambayo hayatusaidii kuondoa umasikini wetu. Ushoga sio umasikini na mashoga hawaifanyi Tanzania kuwa masikini.

Tuna hitaji nyenzo nyingine za kuondoa umasikini wetu ambazo zinajulikana na baadhi ya watanzania wenzetu, kama Malim Sefu wa Zanzibar na wengine wamejaribu kuzielezea kama, elimu ya vitendo, ufunguzi wa research Institutes katika mambo yanayo husu mali asili yetu na namna ya kuyatumia kwa maendeleo yetu sisi wenyewe, ufunguzi wa miradi mbali mbali na sio kujenga mabarabara, madaraja na flyovers tu na interchanges bali miradi ambayo kwa mda mrefu ita saidia kuleta ajira kwa wananchi wetu kama furnace ya kuoka chuma na steal na kadhalika.

Ninge mshauri Makonda kutilia mkazo katika kusimamia ubora wa majengo ya shule zote kwenye mkoa wake na kuona kama wanafunzi wana madawati ya kutosha na masomo yanayo tolewa ni ya kiufanisi na ambayo yatachochea kukua kwa uchumi wetu na hivyo kuboresha maisha ya jamii baadae badala ya kudili na mambo ya kanga kama wanawake wa uswahilini, kitu ambacho kina jenga chuki Kati yetu na umoja wa kimataifa.
Kitu kingine ni kutatua changamoto za maisha ya kila siku ya watu wake na kuwa mbunifu na sio kuendekeza ukilitimba ambao hauna tija kwa jamii yetu. Kuhakikisha kuwa barabara safi za waenda kwa miguu na waendeshaji wa baiskeli kando kando ya barabara za magari zinatengenezwa ili nao wa faidi matunda ya serikali yao.
 
Hingera JPM hata sisi tusio na pesa 2020 tutagombea nafasi za uongozi. Magufuli hataki maneno anataka utekelezaji kwa wakati tena bila kupindisha au kutafuta sifa tunapashwa tukimbie tulicheleweshwa mno. Sasa wewe kama siyo wehu mambo mnakubaliana kwenye vikao vya baraza la mawaziri boss wako anakupa go ahead wewe unaenda fanya ya kwako au kutumwa na mafisadi halafu ukitumbiwa unanungunika kweli?
JPM piga kazi tunakuombea.
 
Hingera JPM hata sisi tusio na pesa 2020 tutagombea nafasi za uongozi. Magufuli hataki maneno anataka utekelezaji kwa wakati tena bila kupindisha au kutafuta sifa tunapashwa tukimbie tulicheleweshwa mno. Sasa wewe kama siyo wehu mambo mnakubaliana kwenye vikao vya baraza la mawazili boss wake anakupa go ahead wewe unaenda fanya ya kwako au kutumwa na mafisadi halafu ukitumbiwa unanungunika kweli?
JPM piga kazi tunakuombea.
Kabla ya kubofya neno 'post' uwe unahariri(edit) kwanza!
 
Mkitaka kugombea njooni niwape nondo za kuvutia wapiga kura wenu.. kila mtu itakuwa tofauti mwanzo mwisho.. kutokana na vitu mbali mbali ambapo utajaza questionnaire kwanza..
Nitakupa nondo za uongozi/utendaji.. na kukusaidia utakaposhinda juu ya skills na uongozaje.. uweje.. ufanyaje.. ujiongeze vipi.. n.k.
😊

JPM atakupa/atawapa salute
As kila mmoja atapaa kivyake😎
 
Wakuu,

Kuna msemo unaosema Mnyonge mnyongeni, haki yake mpatieni. Nimejaribu kupita sehemu mbalimbali katika mitandao ya kijamii pamoja na magazeti mbali mbali hapa nchini na nje ya nchi utakuta mara nyingi mambo yanayoongelewa ni yale yanayokwamisha bidii na kuonyesha madhaifu ambayoo inasemekana kufanywa na serikali ya awamu ya tano.

Ni obvious wale watu waliokuwa wanafaidika na mifumo ya serikali zilizopita huenda ndio wakawa wachochezi wakuu wa kusambaza habari zinazoendelea na kuzichapisha kwa bidii sana maana hamna tena nafasi za kufaidi ovyo ovyo

Nadhani ifike mahali watu tukubali kwamba awamu hii ya serikali imejitahidi saana kututoa sehemu moja hadi nyingine katika nyanja zoote zote za kimaendeleo... kiuchumi na hata kidemokrasia.

ina maana ni kwel hatuoni biodii za Mh Rais??

Elimu watoto wetu sasa wanapata bure na waalim wanafundisha kwa umakin ndio maana unaona hata shule za serikali sasa zinaingia katika shule bora za kitaifa katika mitihan mbali mbali.. kwa maana hyo sekta ya elimu imekaa mahala pake. hapa hapa kwenye elimu mikopo ya elimu ya juu inazidi kuongezewa bajeti yani kuonyesha jinsi gani serikali inaweka swala zima la elimu katika kipaumbele

kodi zinalipwa bila utani,na serikali inazidi kuweka bidii katika ukusanyaji wa kodi , sasa hapa wanaolalamika ni wale wamezoea tu kuendesha biashara zenye faida kubwa bila kulipa kodi, yan hivi tuwe na huruma jamn unadhan nchi itaendeleaje bila kuleta hizo kodi.. watu tumeumbwa kulalalama tu kwakweli

rushwa sasa hivi ni kwishney yan mambo yamekua mnyororo hakuna tena pinda pinda bila sababu za msingi.. imekomeshwa katika sekta nyingi sana

haya nani asiependa barabara nzuri.. hapa utasikia watu wanaulliza ooh barbara zitamsaidia nn maskini.. sasa tufikirie imagne hamna barabara nzur hapo kwako na ww n mfanyabiashara utumie masaa sita barabaran kufatilia tu mambo yako huon inachosha.. kusema kweli sekta hii piga ua Rais wa Awamu hii Dkt. JPM amefanya kazi kuubwa saana kupita kiasi..

usafiri wa anga umekuwa wa uhakika sana na imara na mzuri na ndege zetu bombastic kabisa zinazoruka kilaa siku iendaypo kwa Mungu kwa bei za kitanzania kabisa.. nani asiependa.. sasa hivi tumekua na ndege zetu ambazo zilikufa hapo nyuma na kiasi kwamba tumerudishwa katika soko la kimataifa kabisa yani kuonyesha n jinsi gani Rais JPM anapambana haswaa katkakutekeleza yale aliyoyaahidi kwa jaili ya nchi yake katika kipindi cha uongozi wake

ulinzi na usalama wa raia na mali zake uko konki kabisa ndio maana kila mmoja anafurahia kuzunguka masaa 24 bila kuwa na wasiwasi wa kukutana na mambo kama vita na vitu kama hivyo.. ulinzi uko konk kabisa umeimarika

nidhamu makazini imerudi sasa hivi watu wana nidhamu ya kazi maana kwa opareshesni ya kutumbuliwa hahah nani anataka.. watu wanafanya kazi kwa uzuri kabisa hakuna terna bla bla bla

miradi mikubwa ya mambomba ya maji yanazidi kusambazwa, umeme wa uhakika unapatikana tanzania nzima bila kuwa na mizengwe ya kukatika katik aovyo ovy..

mabomba ya mafuta kama tunavyojua.

yaan kwa ufupi mambo ya kuandika ni mengi mno.. bidii tunaziona na maendeleo tunayaona na tunayakubali kimya kimya hata kwa ubishi wa wazi kama tunavyoona watu wanaopinga wakikubali kimoyomoyoo..

viva serikali ya awamu ya tano na bidii zake
 
ina maana ni kwel hatuoni biodii za Mh Rais??
bidii zake tunaziona, watumishi wa umma watalipwa robo pesheni na hela zilizosalia wataendelea kulipwa kama mshahara wakifa kabla ya kulipwa fedha zao zote ni kiherehere chao hela zinapelekwa kwenye ujenzi wa zahanati.
 
Magufuli ataacha legacy kubwa sana ktk nchi hii, kinachonivutia sana kwake nikuwasaidia wanyonge ,asante sana Raisi wangu kwa kutupandishia bei ya Korosho kiukweli umeyagusa maisha ya sisi wakulima, natamani utawale nchi hii hadi utakapochoka mwenyewe, unalazimishwi kuamini ninacho amini Mimi
PSX_20181112_150206.jpg
PSX_20181112_150149.jpg
 
Misimamo mikali mwisho wa siku aliukumbia urais kwa hali ya uchumi kuwa mbaya ..naona na huyu unayemsadiki atatutumbukiza kwenye uchumi mbaya na huenda akaukimbia uraisi
 
Misimamo mikali mwisho wa siku aliukumbia urais kwa hali ya uchumi kuwa mbaya ..naona na huyu unayemsadiki atatutumbukiza kwenye uchumi mbaya na huenda akaukimbia uraisi
Huyu ni Raisi ambae amezungukwa na WASOMI WENGI SANA yote anayoyafanya nimatokeo ya ushauri mzuri anaopata kutoka kwa wataalamu
 
Back
Top Bottom