Tunaenda taratibu, reli tayari, ATCL ina ndege kwa sasa.Magufuli kwa ustadi kabisa kaanza kwa kasi kutekeleza ilani ya chadema kama kukataa misafara, kufuta sherehe za kipuuzi na kuelekeza pesa kwenye jamii, kinachofata sasa Magufuli futa kile kibatari cha kichawi wakati tukisubiri ahadi yako ya
laptop kwa kila mwalimu
mil 50 kwa kila kijiji
ujenzi wa Reli
ufufuaji wa viwanda na ajira mil 1.5 kila mwaka.
naiona ilani ya magamba iko kabatini huku ikitekelezwa ya chadema
Yah haijalishi anatumia ya NCCR au CHAUMA cha msingi kazi ifanyike.yaan kwetu sisi wa tz iwe kaichukua ilani ya ACT...CCK...CDM au yoyote ile sisi maadam anapiga kaz hasa ya kupambana na ufisadi na mafisadi........tunampa big up sana kamanda wetu wa mapambano........all the best sir Pombe.
Hata mimi sikuwahi kuliona hapo kabla, suala la laptop lilikuwa Kenya huwenda wamejichanganya.Sikuwahi kusikia mahali popote Dkt Magufuli akitoa ahadi ya Laptop kwa kila mwalimu....Watanzania tuache mzaha. Tumepata mtu serious...tuache afanye mambo ambayo ni kipaumbele.
Sasa mwalimu kumpa Laptop ya kazi gani!? Badala mshauri tuweke desktop kwenye mashule...ili zifaidishe na wanafunzi pia...nyinyi mnaleta mzaha.
Kila kitu ambacho Magufuli anafanya kipo kwenye Ilani ya CCM....hilo la Laptop kwa kila mwalimu halimo. Tuache mzaha.
Aiseee[emoji15]kupunguza misafara ya kipuuzi ilikuwa kwenye ilani ya CCM...kufuta matamasha na safari za kipiizi ilikuwa kwenye ilani ya CCM....Magufuli endelea kutumia ilani ya Chadema na usione tabu kutuuliza namna ya kutekeleza...
Uliona mbali sana mkuu. Kunywa banana nakuja kulipa.Mm ukawa damuni lakini kwa Magufuli nimepiga breki,kwa staili hii ya Magufuli miaka mitani tumekwisha na kufutika katika ramani za siasa.
Kwanini?Nitaufufua huu uzi baada ya mwaka mmoja.
Viva Magufuli, president of Africa.Kenya wanamkubali Mshua JPM
kweli watanzania tumekuwa katika dimbwi la umaskini kwa zaidi ya miaka 50, huku vigogo na matajiri wacheche wakitumia ujinga wetu kutuambia Nchi yetu ya Tanzania ni Masikni, tangu Nyerere hatujawahi shuhudia rais mwenye Uzalendo na nia njema kwa watanzania, Nafikiri Mungu ametusikia yuko kazini. Tusubiri mambi mazuri na Makubwa zaidi, maana huyu Magufuli ana sifa zifuatazo:
1. Mzalendo
2. Mpenda watu kwa dhati
3.Mchapa Kazi kwa Bidii
4.Mwenye kutaka kwa shauku maendeleo ya Tanzania
kILA LA KHERI MAGUFULI WETU MUNGU YUPO PAMOJA NA WEWE, TUNAKUOMBEA SANA BABA. ILI ADUI ASIPATE NAFASI. HATA KIDOGO. DAMU YA YESU IKUFUNIKE, MALAIKA WENYE UPANGA ULAO KUWILI WAKUZINGIRE KIPEKEE SANA.
Tunasonga mbele mama kubwa lengo letu ni kuhakikisha kila mwananchi anafurahia kuishi Tanzania.Mie mtaani kwetu raha tupu vitu dukani vimeshuka bei, sokoni nyama bei ni kama bure kwa kweli maisha yamekuwa rahisi sana kweli hii ndio Tanzania tuliyoitaka.
Sure.Magufuli ni habari nyingine yaani hizo ni rasharasha tu bado mambo mengi yanakuja kuweni watulivu
Nasi tunapaswa kuwa wazelendo na watiifu ili kula mema ya nchi.Ukipata kiongozi mwenye upendo na watu wake mambo ndio uwa hivyo. Asante rais wetu Dkt Magufuli kwa upendo wako kwa Watanzania.
Amen.Tunaomba na kumwombea rais wetu kwa ajiri ya nchi yetu.
Make Tanzania Great #Viva JPM.Go go go mtumbua majipu ambaye hajawahi tokea katika sayari hii ya tanzania!!tumechoka na viongozi wazembe!!tumechoka na huduma mbovu!!tumechoka na ufisadi tufanyie surprise nyingine huko chamwino nasikia upo umejifungia ukikagua cv za wakuu wa mikoa na wilaya
Moto wa JPM umewazidi.Wanaisoma namba
Sio kweli, Jamaa alipigiwa kura na watu wengi waliokuwa neutral...!
Tatizo lenu mnaamini kila mtu anaendeshwa kwa misingi ya vyama..poor you!!
Watu washaanza kumkumbuka mzee wa maisha bora,alisema watamkumbuka nadhani alimaanisha wale watu wachache waliokua wanaitafuna nchi.Sasa tingatinga limeingia wanaisoma namba hakuliki wala hakuendeki.big up prezidaa piga kazi saidia sisi wanyonge malofa.
Siyo kufifia utakufa kabisa.Upinzani umefifia kabisa
Ulinzi upo wa kutosha na kazi atapiga bila shida.Me naomba watanzania tumuombee huyu dingi manake anavopiga kazi kuna vigogo wauza unga, wapiga madili, wezi wa kupindukia, mafisadi hawatampenda badala yake watamchukia. kumbuka John Kennedy wa usa alipingia ikulu moto wake ulikuwa like wa JPM but yaliyotekea wengi tunayajua na wahusika wakuu ni matajiri wakubwa wa nchi hiyo. so TUMUOMBEE SANA RAIS WETU MPENDWA JPM, NA AONGEZEWE ULINZI MARA DUFU. PIA NA YEYE ASIJIACHIE KITAANI