Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

From The Bott6 Of My Heart: Binafsi Siamini Kua Wanaomkosoa Magufuli Wamekosa Ama Wanabaniwa Ulaji. History Is The Best Teacher. Magufuli Hakupata Urais From Heaven Angel, Ukweli Mchungu Ni Kua Miongoni Ya Waliompa Ni Wahujumu Uchumi Na Mafisadi. Tukitambua Ukweli Huo Mchungu. Yapo Maswali Ya Kadhaa Ya Ku-jiuliza Ufanisi Wake Katika Kudili Na Mafisadi + Wahujumu Uchumi. Iko Clear Kwamba Tutaacha Kuwa Washabiki Na Kuhoj?
 
Robot ya korosho utaijua tuu

Subiri abishe hodi nyumbani kwako ndio utajua anafanya nini maana nyie kina Tomaso mko wengi:decision:

cha ajabu alichofanya ni kusikiliza kilio cha watanazania na kufanya ambacho wengine hawajakifanya......

Kama wewe sio kichaa unaelekea kuwa kichaa.... Kama sio kichaa kwa sasa basi utakuwa kichaa shupavu pale milembe

Aisee...hapo wenyewe mmejipinda kweli kweli mkidhani mnaandika hoja za maana!!

Pole zenu!!
 
Ni kama nyie mliohubiriwa na DJ kuwa tatizo ni mfumo na si mtu, sasa Magufuli anafanya kazi kupitia mfumo upi? shame on you

Maskini elimu ya kata! imetuharibia kizazi cha sasa...ona utumbo huu hata hajaelewa nilichoandika maskini!
 
Umeme utashuka, subiri mradi ukamilike, mbona una kiherehere kijana.
aaaahhhh!!!! imebidi nicheke tu, naona umesahau yale niliyokuambia wakati ule. Kumbuka hata Songosongo walisema hayo hayo. Cha ajabu nawe unaimba kama kasuku wimbo huo huo. This is Tanzania Bibie, shamba la Bibi. Ndiyo maana Noran anatucheka sana
 
nimemskia aliekua mkuu wa taasisi ya kupambana na ufisadi nchini kenya akiponda utendaji wa marais wengne huku akimsifia magufuli
 
Kumekuwa namaneno yakijinga jinga ktk mtandao kumponda Magufuli au kumsema eti anawabeza viongoz walio pita mim nasema hivi, hili si kweli maana toka Mwinyi mpaka kikwete wote walipewa Nafasi ya uwamiri jeshi mkuu wa majeshi ya taifa hili na walicho kifanya ndio kitakacho ishi ata baada yakuondoka kwao. Magufuli amekuja na yake amejuwa siri yakuwa Rais na deni anadaiwa na Wa Tz. Even hayati baba wataifa anaona tumempata mtu ktk watu. Magufuli amekuja na staily za Nyerere na anataka kuuonyesha ulimwengu Rais nikuwajibika na sio kula,kuvaa vizuri,kupigiwa mizinga na kuish ktk majengo yakifahari. Magufuli atatuachia taifa jipya even watoto wetu watajivunia taifa hili. Mungu alie wapa hekima na maarifa viongoz wajuu wa taifa hil kutuletea Magufuli. Awape maisha marefu yenye heri na fanaka. Amen
 
Huyo atakuwa Lumumba. Anatisha ktk kuongea na kama amemkubali huyo. Pombe ametisha.
 
Magufuli ni mfano wa kuigwa kwa marais ote Africa....ingawa ni kwa muda mfupi kutoa tathimin Lakini huyu jamaa atatupaisha balaaaaaaaa!!!!!
 
Hongera Dr. Magufuli (PhD) ukienda kuhutubia EAC kama Mwenyekiti wanyooshe haswaaa, tena pale EAC Secretariat kuna ufisadi wa hali ya juu kapasafishe haswaaa
 
kama ni kweli kwa hayo unayo yazungumzia basi ili niamini naomba arudishe maduka ya ujamaa, na shule zote za watu binafsi apole ziludi serikalini, na kama hawezi naomba usimfananishe na mchonga, kwakuwa mchonga aliyaweza, nae hawezi kuvaa hicho kiatu.
 
Mwanzo wa magufuli sio mbaya ila mim kama mwananchi wa kawaida hajanifikia maana nna vilio vyangu vya kila siku kama vle huduma za afya rahisi na bora, vyakula vishuke bei, maji yapatikane na mengineyo..so aendelee na mambo yake ila mwisho wa siku mm wa dihimba nataka hayo. By the way big up rais wangu.
 
Baada ya 'warm up' (kupasha misuri) kazi itaanza. Itaanza ya 'push up', itafuata ya sarakasi na baadaye kazi zingine zitafuata.

Sasa nimeamini kuwa mafisadi ni waoga sana kwani tayari wengi wameanza kuweweseka kwa kuona 'warm up' tu! Kazi itakapoanza sijui itakuwa vipi?
 
Ukiwauliza maofisa serikalini wanakwambia...'moto wa mabua tu'..lakini mabosi wao Dsm matumbo joto. mi siwaelewi.
 
kama ni kweli kwa hayo unayo yazungumzia basi ili niamini naomba arudishe maduka ya ujamaa, na shule zote za watu binafsi apole ziludi serikalini, na kama hawezi naomba usimfananishe na mchonga, kwakuwa mchonga aliyaweza, nae hawezi kuvaa hicho kiatu.

Mchonga alisalimu amri na kukiri hawezi kuendesha uchumi hivyo. Hebu jaribu kujisogeza katika karne ya 21, mkuu!
 
Anakutana na wafanyabiashara sasa sijui itakuwaje maana mzee hatabiriki!
 
Kazi kaanza sema kasi ndio inaenda inaongezeka. sasa gari sasa yuko gia ya kwanza.
 
Back
Top Bottom