Mafinga: Wafanyabiashara wagoma kufungua Maduka siku ya pili baada ya Halmashauri kuwapangia kodi kubwa ya pango

Mafinga: Wafanyabiashara wagoma kufungua Maduka siku ya pili baada ya Halmashauri kuwapangia kodi kubwa ya pango

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
IMG_0158.jpeg
IMG_0157.jpeg
IMG_0156.jpeg

Mgomo wa wafanyabiashara katika Soko Kuu la Mafinga lililopo Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa wa kufunga maduka, umeingia siku ya pili leo Agosti 24, 2024 ukisababisha adha kwa wananchi kukosa huduma.

Mwananchi limefika sokoni hapo na kushuhudia milango ya maduka hayo imefungwa huku baadhi ya wananchi waliofika kwa ajili ya kupata huduma wakiduwaa wasijue cha kufanya.

Wafanyabiashara wamedai kuwa hawatafungua maduka hadi malalamiko yao ya kupunguziwa kodi ya Sh80,000 yatakaposikilizwa.

Mwananchi ilimtafuta Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dk Linda Salekwa kuzungumzia hali hiyo lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda baada ya kutafutwa bila mafanikio.

Hata hivyo, Diwani wa Boma, Julias Kisoma lilipo soko hilo, amethibitisha wafanyabiashara hao kufunga maduka kwa madai kodi wanayolipa ni kubwa.

“Wafanyabiashara wanalalamikia kodi wanayolipa ni kubwa ambayo ni ya zaidi ya asilimia 200, lakini mimi kama diwani nitaendelea kuwasemea wafanyabiashara hawa hadi pale nafasi yangu ya uongozi itakapokoma,” amesema diwani huyo.

Wakizungumzia adha hiyo, baadhi ya wananchi wamesema hali hiyo imewasababishia adha kubwa ya kufika sokoni bila kupata mahitaji kutokana na mgomo huo.

“Nimetoka kijijini kwa ajili ya kununua mahitaji ya duka langu lakini nimefika hapa nimekuta maduka yamefungwa, hivyo nimepoteza nauli muda katika suala hilo,” amesema mkazi wa Mtili, Prisca Mlelwa.

Mlelwa ametoa ombi kwa Serikali kukaa meza moja na wafanyabiashara hao ili wafikie mwafaka na kuendelea na biashara zao.

MWANANCHI
 
watafungua wala haina shida

nafikiri wamesahau habari ya rejesho
 
View attachment 3078256View attachment 3078257View attachment 3078258
Mgomo wa wafanyabiashara katika Soko Kuu la Mafinga lililopo Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa wa kufunga maduka, umeingia siku ya pili leo Agosti 24, 2024 ukisababisha adha kwa wananchi kukosa huduma.

Mwananchi limefika sokoni hapo na kushuhudia milango ya maduka hayo imefungwa huku baadhi ya wananchi waliofika kwa ajili ya kupata huduma wakiduwaa wasijue cha kufanya.

Wafanyabiashara wamedai kuwa hawatafungua maduka hadi malalamiko yao ya kupunguziwa kodi ya Sh80,000 yatakaposikilizwa.

Mwananchi ilimtafuta Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dk Linda Salekwa kuzungumzia hali hiyo lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda baada ya kutafutwa bila mafanikio.

Hata hivyo, Diwani wa Boma, Julias Kisoma lilipo soko hilo, amethibitisha wafanyabiashara hao kufunga maduka kwa madai kodi wanayolipa ni kubwa.

“Wafanyabiashara wanalalamikia kodi wanayolipa ni kubwa ambayo ni ya zaidi ya asilimia 200, lakini mimi kama diwani nitaendelea kuwasemea wafanyabiashara hawa hadi pale nafasi yangu ya uongozi itakapokoma,” amesema diwani huyo.

Wakizungumzia adha hiyo, baadhi ya wananchi wamesema hali hiyo imewasababishia adha kubwa ya kufika sokoni bila kupata mahitaji kutokana na mgomo huo.

“Nimetoka kijijini kwa ajili ya kununua mahitaji ya duka langu lakini nimefika hapa nimekuta maduka yamefungwa, hivyo nimepoteza nauli muda katika suala hilo,” amesema mkazi wa Mtili, Prisca Mlelwa.

Mlelwa ametoa ombi kwa Serikali kukaa meza moja na wafanyabiashara hao ili wafikie mwafaka na kuendelea na biashara zao.

MWANANCHI

Hii ndiyo lugha pekee ambayo hata vyura viziwi huisikia
 
Hii tabia idhibitiwe haraka serikali ichukue hatua ya kuwafutia leseni mtu fremu sio zako halafu unataka wewe ndiyo upange bei! Mbona kwa watu binafsi wanalipa kodi kubwa kuliko hiyo! Siungi mkono upuuzi huu.
 
Back
Top Bottom