Mafundi Magari wa Kibongo hufanikiwa kujiinua kwa Promo halafu ukiwapatia kazi wanajiua kwenye kazi ya kwanza tu

Mafundi Magari wa Kibongo hufanikiwa kujiinua kwa Promo halafu ukiwapatia kazi wanajiua kwenye kazi ya kwanza tu

PakiJinja

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
11,689
Reaction score
25,848
Mafundi garage wa kitanzania wana mchango mkubwa sana katika kuyatia ubovu magari ya watu. Mafundi hawa ni wazuri sana kwenye kujipigia promo na kuwaharibia waliofanya uwekezaji mkubwa.

Utakuta fundi anawachambua yale magereji makubwa yakiwemo ya wachina na wakorea kwamba wale hamna kitu kabisa, hawatengenezi bali hununua na kufunga vifaa vipya.

Au wakati mwingine wanakuonyeshea jamaa anayepita kwenye hizo garage akiyza wiper, utasikia umemuona yule jamaa amepita na begi la waipa? Basi huyo ndiyo wachina wote hapa mjini wanamtegemea kusuka engine za magari yao.

Ukijichanganya ukawapa kazi hawa mafundi, basi tarajia gari kuua kifaa kingine, au vifaa kunyofolewa, gari kuanza kubadili milio n.k

Ukitaka kupaka rangi wataponda kwa nguvu zote watu wenye vifaa vya kisasa na kuanza kusifiana wao huku mitaani, paka rangi kwao sasa, miezi minne mingi gari imeshafubaa inaanza kukudai upya.

Wengine kwenda kutengeneza gari kwao inabidi uwe na fundi mwungine utakayekua una muuliza kama asemacho fundi huyu ni kweli na mara nyingi huishia kusagiana kunguni. Ukilaza gari ndiyo uhesabu umeisha. Kupaka rangi tu unalazimika kusubiria gari ikauke, ukiwaachia tu wanapita na masega.

Wito wangu kwa mafundi wa kibongo ni kwamba. Acheni gubu kwa wenzenu waliowekeza. Na nyie ikibidi unganeni muanze kufanya mambo ya kueleweka.

Mna mislead sana watu na kuwatia hasara. Mtu mpaka anahisi kuwa na gari isiyo na shida haiwezekani. Maana ukitengeneza kwao na gari ika misbehave wanakwambia gari yoyote ukitaka kujua kama ni nzima ni lazima iwe hivyo

Mpaka watu wanaogopa kununua gari isiyo na shida, wanahisi labda hiyo ndiyo feki.

Ifike mahali jifunzeni kuboresha mazingira ya kazi zenu. Pia muache udokozi wa vifaa kwenye magari ya watu.
 
Fundi anayechomoa vifaa kwenye gari namwona ni hamnazo tu, ni sawa na daktari aliyepelekewa mgonjwa kumtibu malaria aanze na kumwibia figo.
 
mimi sina gari lakini mafundi wengi wanarudisha watu nyuma kwanza kwa kutojifunza mbinu mpya na teknlojia inayobadilika inayoenda na wakati
 
Acheni kuendekeza anasa za kygynger wakati tuliumbwa na miguu. Kwani umelazimishwa kumiliki gari?

Kila mtu bongo ni mwizi katika nafasi yake.

Nunueni magari ya maana myapeleke DT Fobbie. Mnanua gari ya 1996 ina milage 600K + halafu mnabaki kulialia humu jamvin na kuwalaumu mafundi wetu wazawa.

Kuweni wazalendo nyie.
 
Siwezi kuwabeza pia siwezi kuacha kuwaambia ukweli kwamba kwa hali ya teknolojia tulipo fikia inahitaji pia kujifunza zaidi kwasababu kilio cha uharibifu ni kikubwa.

Japo wapo mafundi ninawafahamu wameenda shule vyema na wapo serious na hiyo kazi. Kwahiyo huwezi kuta anafanya jambo kwa kubahatisha.
 
Mafundi wa kweli hawanaga promo kabisa wao kazi kazi tu,mechanical wanaijua vyema
Sasa unampelekea gari uchebe sijui
Unategemea nini mkuu

Ova
Ila bongo yani kila fundi mpigaji kwaanzia wa cherehan, nyumba, magari halafu hayatajirik maisha yao ya kuungaunga tu.

Walishaniibiaga sement na nondo za kutosha yani nawamaindigi kichiz halaf maisha yao duniii. Moja linaitwa mamenooo nadhani wa kupuliza anaweza kumfaham.
 
Magereji yanayoji promo Instagram wengi ni matapeli na wezi. Ni hatari hatari kubwa! Binafsi kama si umakini na ufuatiliaji walikuwa wanilize vibaya! Deal na mafundi uliozoea na kama kuna kazi ya ziada mtumie fundi wako kupata fundi unayemtaka.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Mafundi body wanaotumia vifaa vya kisasa Dar wanapatikana wapi?

Nashida nao hawa
 
Wanatuamisha kuwa vifaa vikiwa vipya ni feki, hivyo inabidi kununua used, kumbe lengo ni ili wakuuzie vile walivyovichomoa kwenye magari mengine.
Mimi nikipeleka gari hiyo Siku sitoki hapo. Mpaka gari liwe sawa.
NB: kama halijapona, gari halilali Kwa fundi qumer ya kibuyu
 
Naunga mkono hoja, bongo mafundi ndio vinara wa kuyafanya magari yawe mabovu zaidi kuliko ubovu wa gari lenyewe, mafundi wanaamini kwenye kutumia nguvu kuliko logic, bahati mbaya hata kwenye garage kubwa matatizo ni yale yale
 
Zaidi sana mafundi wetu hawa nyundo mkononi ukipeleka gari make sure unasimamia
Bila hivyo
a. wataiba spea za maana
b. kazi watalipua! sana
c. hawagusi gari mpaka uwepo , ukiondoka anaanza mishmishe zingine
 
Mi kuna fundi 1 ndo nilikuwa namtumia kwa miaka 7 kabla ya kuanza tembea miguu.

Hadi nikawa fundi
 
Mi kuna fundi 1 ndo nilikuwa namtumia kwa miaka 7 kabla ya kuanza tembea miguu.

Hadi nikawa fundi

Jan motors ndio haohao jan international ltd? Bei zao mbona kama ziko chini kuliko kawaida,
 
Yaani, kaz kwelikweli af ukiwa na idea ya tatzo lako ndo anakudiss af anakuambia, vyombo vyote sisi tunafanya hivyoo.
Bongo ngum sana hasa ukiwa 'mdhungu'
 
Back
Top Bottom