Mafunzo ya kutengeneza mkaa wa kisasa

Status
Not open for further replies.
Hii picha si ya shamba lako, mbona huko chini kuna maneno ya kiarabu?mtu poa 2013, mtoa mada, smart 2013, consolata2000, 3500 nadhani ni mtoa mada na ID zake tofauti


Hapana dada, hiyo nadhani ni kamera yenyewe maana imenunuliwa kutka doha. Mimi sio bwana biashara 2000
 
Hii picha si ya shamba lako, mbona huko chini kuna maneno ya kiarabu?mtu poa 2013, mtoa mada, smart 2013, consolata2000, 3500 nadhani ni mtoa mada na ID zake tofauti

ngoja ni post nyingine nzuri ambayo na mimi mwenyewe nipo ili unione ujue kuwa mimi sio biashara2000. maana biashara2000 watu kadhaa humu washamuona hivyo wata comfirm sio mimi
 
Hii picha si ya shamba lako, mbona huko chini kuna maneno ya kiarabu?mtu poa 2013, mtoa mada, smart 2013, consolata2000, 3500 nadhani ni mtoa mada na ID zake tofauti

Hata lotti masai, mwana ally, ladyfurahia, thegreat genius, mimi.mimi, husninyo, dolevaby, africando na yeyote yule katika hii thread ni biashara2000! This guy has a lot of time in his hands.

Mi nadhani cha muhimu hapa ni kuendeleza kile ambacho baadhi ya members waliochangia katika thread hii walioamua kujiunga pamoja na ku share uzoefu wao na kuamua kukutana na kuanzisha mashirikiano, watu wa dar na arusha nadhani. Hii ndio inayotakiwa ifanyike. Watu wameamua kuondokana na umaskini. Kila mtu amechoka kuishi maisha ya kutokujua kesho atapata wapi chakula, mavazi na nyumba. Conspiracy theories kama unazipenda kuna section ya intelligence ningeomba uwe una spend muda wako huko. Humu watu waachwe wajifunze na kuanzisha miradi yao ya kujiingizia kipato.
 

Kuhusu ku share uzoefu, biashara2000 naona ana hamasisha watu kushirikiana na kushare information. Katika vitu ambavyo unachanganya ili kuongeza ubora wa mkaa wakati wa kuutengeneza kama ambavyo biashara2000 anavyoshauri, juzi nilimpigia simu akasema pia unaweza changanya kiasi kidogo cha sodium nitrate au chemicals nyingine ambazo yeye aliniambia kuwa weekend iliyoisha alikuwa anafanyia majaribio. Nimeona ni share info hii kwa kuwa leo ndio nimechanganya chemical hii na baada ya mkaa kukauka ntaangalia kama kuna tofauti.
 

Wangu bado sijauchanganya na kitu chochote kipya naona uko vizuri tu. Ila kwa kuwa haiumizi kujaribu vitu vipya, ntajaribu ujanja huo mpya. Hiyo chemical inasaidia nini hasa?
 
Wangu bado sijauchanganya na kitu chochote kipya naona uko vizuri tu. Ila kwa kuwa haiumizi kujaribu vitu vipya, ntajaribu ujanja huo mpya. Hiyo chemical inasaidia nini hasa?

Mdau anasema kuwa sodium nitrate ni combustion agent, yaani inasaidia mkaa wako kuwaka haraka. Kuna chemical nyingine anasema anaijaribu bado ya kuongeza mkaa kuwaka muda mrefu zidi. Nadhani tumuulize
 
ni kweli kabisa hata mm na myamba mbepo juzi tulikua tunajadiiana kuhusu hizo chemicals cz tulipitia writtings mbalimbali tukakuta hivo vitu na wataalam wanasema kuna ya.kuongeza uwezo wa mkaa kuwaka kwa ukali,nyingne mkaa kuwaka muda mrefu hadi white chalk unatumija na wanasema una positive impact.
mm leo nitest sample yangu nyingne ambayo ni sample ya tatu baada ya ushauru wa bw 2000 na wadau wengne mtu poa na wengne na naona kuna dalili za kuwepo positive impact ksho kuanzia asubuhi ntautumia niendelee kuucheki
 

Ijaribu hiyo kesho kama bado utakuwa unakutatiza nipigie tuendelee kushauriana na kurekebisha mambo mpaka utokee vizuri maana watu wengine wametoa vizuri tu
 
Yani mimi nishautengeneza na kuupikia several times..sijaweza bado kuwapa watu wengine wautest lakini uko poa.sana tatizo.kidogo ni kuwa majivu ni mengi na ukisha waka hautakiwi uguse guse jiko maana unavunjika. Vizuri uuongezee hapohapo. Nilimpigia Biashara2000 akanambia nikipata mashine kubwa kidogo nibadili ratio.. Sasa hivi niko na 5 kwa 10..NAJUA NTAFIKA TUU
 
Kuna kipindi nilikuwa Nairobi katika shughuli zangu za kutafuta maisha nikakuta katika maduka mengi wanauza huu mkaa wa kisasa ukiwa umepakiwa kisasa kabisa jambo ambalo lilinihamasisha sana. Nikaona hata mimi naweza fanya hivyo ingawa kwa sasa bado sijaanza kupaki kitaalamu. Ila nimeona ni idea nzuri kwa sisi watz nasi kuamua kufanya vitu kisasa zaidi kama wakenya. Kuna kampuni moja ya keny ainaitwa chardust Ltd ndo hao wanaotengeneza mkaa na kuupaki katika pakti ndogo ndogo za kilo 4 na kuuza kwa sh 200 ya kenya ambayo ni kama sh 3500 ya bongo. Cheki picha ya mkaa huo hapo



Hii ni changamoto ambayo inabidi tuweke mawazo yetu huko ili nasi tufanye mambo ya kisasa. Ila nimeona kampuni moja ya tz nao wameanza kupaki namna hii wanauuza mkaa wao pale shoprite mlimani city. Wamejitahidi. Na nikachunguza packaging yao nikagundua kuwa wanatumia mifuko flani hivi ya kaki inauzwa kwenye ma supermarket kwa ajili ya kubebea vitu na kuweka mkaa huko na kuweka nembo. Wanawekea nembo zao pale manzese darajani kuna jamaa wanachapisha nembo kwa bei nzuri. Nimeamua ku share info hii kama mchango wangu ktk jamii ya JF
 

changamoto kama hilo nilikuwa nalo ila nilitatua kwa kuacha kabisa kuweka maji katika hatua za utengenezaji wa mkaa kwa maelezo ya biashara2000. Alisema maji yanaua nguvu ya mkaa na kuufanya uwe na majivu mengi. Usiweke maji kabisa katika mkaa wako
 

Halafu kama mkaa wako unapikia vizuri tu usisubiri kitu. We anza kuuza ilimradi tu uwauzie watu kwa bei nzuri wakati huo ukiendelea kushughulikia tatizo la majivu liishe. Hakuna kitu perfect duniani, hiyo isiwe sababu ya wewe kukufanya usubiri kupata maendeleo
 

napenda kutokukubaliana nawe kidogo. Ninapenda kuwauzia watu bidhaa ambayo ni bora kadri iwezekanavyo. Kama bado haijawa bora usiwauzie. Ila kila kitu kinategemeana na mteja wako anaangalia nini zaidi katika bidhaa yako. Kuna wanao focus zaidi kwenye muda ambao mkaa wako utaweza kukaa wakati wa kupikia, wengine wanaangali zaidi bei na wengine wanapenda mkaa usiwe ntatizo lolote. Itategemea na wateja wako. Ningekushauri wakati unasubiria upate suluhisho la tatizo lako, hebu jaribu kuuza kidogo kwa wakaanga chipsi hapo mtaani kwenu uone feedback yao. Uone watauchukuliaje. Ila naamini utauza kwa kuwa wakaanga chipsi wengi wanaangalia faida zaidi hivyo tatizo la majivu kwao sio ishu, kwao cha msingi mkaa wako uwe unaweza pika tu. Hivyo point test zali. Uza sampe kama tuseme ndoo moja ya mkaa then uone feedback.

Tatizo lako linaondolewa kwa njia mbalimbali mojawapo ikiwa ni kuhakikisha materials zako hazina mchanga kabisa wala maji, especially maji ya chumvi.
 

Nimeipata idea yako ya kuuza mkaa wako katika supermarket. Tuangalie tu katika muktadha wa kitanzania na wajasiriamali tuliowengi kwa sasa tunafikiria zaidi kuuza mkaa wetu mtaani kwanza au kwenye mashule na mahospitali na ma baa kabla hatujaingia supermarkets. Kwa wajasiriamali wa kawaida unaweza anza kwa kupackage mkaa wako katika njia ambayo ni rahisi kable hujaingia katika packaging complicated. Mfano hapa chini ni baadhi ya baadhi ya bidhaa za kitanzania ziuzwazo mtaani katika baadhi ya mitaa ya bongo.



Packaging za namna hii unaweza zifanya kwa urahisi kabisa na kwa gharama ya chini kabisa. Hivyo viroba vya kilo 50 unaweza beba pale kkoo sokoni kwa sh. 300 kimoja kutokana na idadi unayoitaka. Hivi ni viroba vya rangi tofauti tofauti mfano kijani, nyeupe au nyekundu na havina mistari ya pembeni kama vile vya unga. Pili unaenda maeneo ya mwenge karibu na nakiete kuna jamaa wana print viroba pale. Unaweza kukuta una kiroba chako kilichowekewa nembo yako kwa sh. 550 tu. Ukauza mkaa wako kisasa badala ya kujaza mkaa bila mpangilio kwenye viroba.
 
changamoto kama hilo nilikuwa nalo ila nilitatua kwa kuacha kabisa kuweka maji katika hatua za utengenezaji wa mkaa kwa maelezo ya biashara2000. Alisema maji yanaua nguvu ya mkaa na kuufanya uwe na majivu mengi. Usiweke maji kabisa katika mkaa wako
aisee nahisi cjui ndo nature ya huu mkaa ukishawaka hautakiwikuguswa unamomonyoka..ila nadhani matumizi ya maji yapo tu kwenye hatua ya kupika uji mimi sieki maji baada ya hiyo hatua ya kupika uji lain stil ina hiyo tatzo la kummomomyoka ikiguswq wakati limeshika moto.ila maji nayotumia kwenye lupioa uji niya chumvi,ila pia bado naendeleq kufanya testing kwq mkono.pia wazo la kuuza mkaa ukiwa bado una kasoro na mm naona itakua c wazo zuri..unaua soko kwqn uliemuuzia kuja kumcomvice kua saivi ni mzuri itakua shughuli pevu
 

Jaman naomba nielekez hio oven ya kukaushia mkaa maan hata. Huku arusha n majanga
 
Mi natamani kuuza ukiwa katika ubora unaofaa.. Unajua sisi watanzania ni rahisi sana kutangaza ubaya wa kitu.. Hawajui ni namna gani sisi( wajasiriamali watengeneza mkaa) tunakiu ya kuona tunafanikiwa..nawashauri tukaze buti tuu .tusirudi nyuma ni mwiko..ALUTA CONTINUA
 
kweli hakuna kurudi nyuma mpaka kieleweke..mkaa wangu leo umewaka lakin c kwq kiwqngo cha kuridhisha kwq sabb ulikua unainekana kupoa sana,ila bado naendelea kufanya marekebisho mpaka kieleweke
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…