Mafuriko Dar ushauri wa bure kwa vijana wanaotafuta maisha

Mafuriko Dar ushauri wa bure kwa vijana wanaotafuta maisha

Habari za jioni wakuu......straight to the point
Niwape ushauri vijana wenzangu ambao tumepanga huku mabondeni na ambao wanatarajia kupanga kuwa wasijaribu hiko kitu

Mafuriko yanarudisha sana nyuma hasa kwa vijana ambao tunahustle ili tuweze kutoboa

Leo asubuhi nlitoka kidogo ghetto kuna mishe nilikuwa naifuatilia sehem mida ya saa 10 napigiwa sim kuwa maji yamejaa vibaya mtoni nkajitahid kuwah chap nkakuta ndo yanagonga mlangoni kufungua mlango sekunde kadhaa tu maji tayar magotin nkafanikiwa kuliwah godoro.nguo na vitu kadhaa ila feni,subwoofer,kifridge.vyombo vidogo vidogo.na kisofa vyote chali

Aisee vijana wenzangu hata kam kodi ni ndogo huku mabondeni na kulingana na kipato chetu inatulazmu kuishi huku.....tuikatae hii hali mafuriko yanarudisha sana nyuma

Wasalaaam
Kataa umasikini, kataa vitu rahisi vinavyoweza kuharibu maisha yako
 
Wakazi wa dar Wana roho ya chuma, Kuna njia nilikua napita kipindi nipo chuo, msimu wa mvua kuna wakazi wa nyumba flani muda wote utakuta wanachota maji na ndoo ndogo kuyatupia barabarani, kiufupi nyumba ilikua inaingiza maji si mchezo

Baada ya muda kuna dada nikazoeana nae alikua anakaa nyumba Hio, kumdadisi akaniambia wale wote ni wapangaji pale, nikawa nashangaa kwanini hamuhami kama Kila mwaka maji yanajaa na mnajua, akawa Hana jibu

Aisee mpaka naondoka huko niliacha wote bado wapo nyumba Hio, Kuna watu ni kama hao mafuriko wmezoea wanaishi nayo kibishi
Ipo hi mkuu kuna jamaa wawili nakaa nao hapa....aisee wana miaka miwil na Wala hawana mpango wa kuondoka leo ama kesho wananambia ikitokea mara moja tu haijirudii Tena had mwakani
 
Habari za jioni wakuu......straight to the point
Niwape ushauri vijana wenzangu ambao tumepanga huku mabondeni na ambao wanatarajia kupanga kuwa wasijaribu hiko kitu

Mafuriko yanarudisha sana nyuma hasa kwa vijana ambao tunahustle ili tuweze kutoboa

Leo asubuhi nlitoka kidogo ghetto kuna mishe nilikuwa naifuatilia sehem mida ya saa 10 napigiwa sim kuwa maji yamejaa vibaya mtoni nkajitahid kuwah chap nkakuta ndo yanagonga mlangoni kufungua mlango sekunde kadhaa tu maji tayar magotin nkafanikiwa kuliwah godoro.nguo na vitu kadhaa ila feni,subwoofer,kifridge.vyombo vidogo vidogo.na kisofa vyote chali

Aisee vijana wenzangu hata kam kodi ni ndogo huku mabondeni na kulingana na kipato chetu inatulazmu kuishi huku.....tuikatae hii hali mafuriko yanarudisha sana nyuma

Wasalaaam
Matokeo ya mipango miji mibovu ndugu yangu tofauti na hapo hakuna sijui bondeni walq mlimani.
 
Nilichofundua watu wengi wamejenga kwenye njia za maji

Serikali haizibui mitaro
 
Dah sitasahau miaka ya 2000+ niliwahi kupanga kinondoni mkwajuni eneo la garden kule kama unataka kwenda mwananyamala bondeni.
Siku hiyo nimerudi home nimetoka mishe halafu usiku kuingia ghetto nakuta kapeti linaelea kutia mguu maji kwenye goti naenda kuchungulia dirisha naona taa za magomeni Ile lile blonde lote ni bahari maji kama yote nikawa najiuliza maji yameingilia wapi? kumbe maji yanachemkia chini kama kama chemchem. Kifupi nilihama baadae ila mabondeni hakufai ukienda kiangazi na wenye nyumba wanaringa ila masika utawaonea huruma
 
Someone told me watu wote JF wana nyumba nzuri na magari. na kwa ambao hawajajenga, they live in luxurious Appartments.
Pole sana mkuu kwa yaliyokupata
 
Back
Top Bottom