Mafuriko ya kuku wa nyama Dar es salaam na bei kushuka nini chanzo?

Mafuriko ya kuku wa nyama Dar es salaam na bei kushuka nini chanzo?

Jack HD

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
851
Reaction score
1,168
Habari wanajukwaa,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nimekuwa mfugaji wa kuku wa nyama kwa miaka kadhaa na nimefikia wakati nimenotice soko la kuku kutokuwa zuri hususani kuelekea mwishoni mwa mwaka hasa mwezi november tofauti na kasumba tunayoijua ya mwishoni mwa mwaka kuna high demand ya kuku.


Kumekuwa na sababu mbalimbali kutoka kwa wafugaji ambazo zinaenea kwa kasi katika mwezi huu tu, ikiwamo serikali imeruhusu vifaranga kutoka nje kuingia nchini. Kuna vifaranga vya Zambia vinasemekana vimeingia na wanafungwa maeneo mbalimbali kwenye jiji la Dares Salaam. Pili, kuna taarifa ya Waziri ilitolewa kuhusu kuwashirikisha wenzetu kutoka Uholanzi juu ya kutatua Uhaba wa Kuku nchini, kibaya taarifa hii imefika kwa wakulima kuwa Uholanzi imeanza kusupply kuku waliochinjwa kuja Tanzania na kupelekea soko la Kuku Kushuka. Miezi iliyopita mpaka kufikia mwezi wa kumi ilishuhudiwa Kuku kuuzwa kati ya Tshs. 5300-5800 Kulingana na ubora wa kuku.

Leo hii soko la kuku huyo huyo limefikiwa wastani wa Tshs 4500 - 5000 na bado kuku hawauziki kwa kusemekana kuku wamekuwa wengi na ni wakubwa kuliko kipindi cha nyuma. Nini Tatizo? Nafahamu JF ni kijiji kilichokusanya watu wa kada na kutoka kwenye taaluma mbalimbali, hivyo jibu litapatikana.

Nawasilisha!!

Jack HD
 
Kweli bei imeshuka sana, wanunuzi sasa hivi wanataka kununua kuku mwenye uzito zaidi ya kilo moja, hiyo kuhusu kuku wa uholanzi sikuwahi isikia, so it means kama hao wa uholanzi wataendelea kuleta soko litakuwa hivi hivi?? Basi ufugaji utakuwa mgumu sana.
Mimi nina kuku 800 nategemea kuwauza next week hapa tumbo joto!!!
 
Mie mlaji nataka ifike hata 500 kila siku mnatupiga tu

Ila hawa kuku Wa muda mfupi ni kuuana tu bora ukafuga wako nyumbani
Ikishuka zaidi watu wataacha kufuga, wachache wanaobaki watapandisha bei, back to square one! Lakini on a more serious note, ufugaji kwetu hapa una changamoto nyingi, kuu ni vyakula vya mifugo kuwa ghali sana zaidi ya nchi nyingine. Hivyo without protection, wafugaji wetu hawawezi ku-survive! Lakini protection nayo inatakiwa iwe temporary wakati mitigation measures zinafanyika. Mojawapo ikiwa kuwepo na mkakati wa ku-encourage mass production ya feed ingredients ikiwemo Soya na mahindi, CHEAPLY. CHEAPLY. HOW DO WE PRODUCE FEED CHEAPLY IN TANZANIA? Tafakari!
 
Hii nayo kaz,sasa kila mtu anafuga,itabidi serikal iangalie kwa undani chakufanya hapa kwan nao wanalipa kodi
 
Habari wanajukwaa,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nimekuwa mfugaji wa kuku wa nyama kwa miaka kadhaa na nimefikia wakati nimenotice soko la kuku kutokuwa zuri hususani kuelekea mwishoni mwa mwaka hasa mwezi november tofauti na kasumba tunayoijua ya mwishoni mwa mwaka kuna high demand ya kuku.


Kumekuwa na sababu mbalimbali kutoka kwa wafugaji ambazo zinaenea kwa kasi katika mwezi huu tu, ikiwamo serikali imeruhusu vifaranga kutoka nje kuingia nchini. Kuna vifaranga vya Zambia vinasemekana vimeingia na wanafungwa maeneo mbalimbali kwenye jiji la Dares Salaam. Pili, kuna taarifa ya Waziri ilitolewa kuhusu kuwashirikisha wenzetu kutoka Uholanzi juu ya kutatua Uhaba wa Kuku nchini, kibaya taarifa hii imefika kwa wakulima kuwa Uholanzi imeanza kusupply kuku waliochinjwa kuja Tanzania na kupelekea soko la Kuku Kushuka. Miezi iliyopita mpaka kufikia mwezi wa kumi ilishuhudiwa Kuku kuuzwa kati ya Tshs. 5300-5800 Kulingana na ubora wa kuku.

Leo hii soko la kuku huyo huyo limefikiwa wastani wa Tshs 4500 - 5000 na bado kuku hawauziki kwa kusemekana kuku wamekuwa wengi na ni wakubwa kuliko kipindi cha nyuma. Nini Tatizo? Nafahamu JF ni kijiji kilichokusanya watu wa kada na kutoka kwenye taaluma mbalimbali, hivyo jibu litapatikana.

Nawasilisha!!

Jack HD
Cjaelewa unataka kujua nini, mbona sababu umeshazisema humo
 
In short sio kuku tu. We fatilia hata mazao ya wakulima wa tz kma matikiti, maembe, machungwa, vitunguu. Hivi vyote vimeporomoka bei.


Sababu ni kuwa watu hawana pesa. Sasa mfanyakaz mwaka wa 3 hajaongezewa mshahara mnatgmea nn?
 
In short sio kuku tu. We fatilia hata mazao ya wakulima wa tz kma matikiti, maembe, machungwa, vitunguu. Hivi vyote vimeporomoka bei.


Sababu ni kuwa watu hawana pesa. Sasa mfanyakaz mwaka wa 3 hajaongezewa mshahara mnatgmea nn?
Huyu ndio anetoa chanzo cha tatizo.
Watu hawana pesa mfukoni za kununulia hao mabroila.
Sio kwamba supply tu ndio imeongezeka ishu ni demand imepungua kutokana na purchasing power ya watu kushuka.
 
Habari wanajukwaa,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nimekuwa mfugaji wa kuku wa nyama kwa miaka kadhaa na nimefikia wakati nimenotice soko la kuku kutokuwa zuri hususani kuelekea mwishoni mwa mwaka hasa mwezi november tofauti na kasumba tunayoijua ya mwishoni mwa mwaka kuna high demand ya kuku.


Kumekuwa na sababu mbalimbali kutoka kwa wafugaji ambazo zinaenea kwa kasi katika mwezi huu tu, ikiwamo serikali imeruhusu vifaranga kutoka nje kuingia nchini. Kuna vifaranga vya Zambia vinasemekana vimeingia na wanafungwa maeneo mbalimbali kwenye jiji la Dares Salaam. Pili, kuna taarifa ya Waziri ilitolewa kuhusu kuwashirikisha wenzetu kutoka Uholanzi juu ya kutatua Uhaba wa Kuku nchini, kibaya taarifa hii imefika kwa wakulima kuwa Uholanzi imeanza kusupply kuku waliochinjwa kuja Tanzania na kupelekea soko la Kuku Kushuka. Miezi iliyopita mpaka kufikia mwezi wa kumi ilishuhudiwa Kuku kuuzwa kati ya Tshs. 5300-5800 Kulingana na ubora wa kuku.

Leo hii soko la kuku huyo huyo limefikiwa wastani wa Tshs 4500 - 5000 na bado kuku hawauziki kwa kusemekana kuku wamekuwa wengi na ni wakubwa kuliko kipindi cha nyuma. Nini Tatizo? Nafahamu JF ni kijiji kilichokusanya watu wa kada na kutoka kwenye taaluma mbalimbali, hivyo jibu litapatikana.

Nawasilisha!!

Jack HD
Mzunguko wa Pesa umekua wa hovyo sana.Pesa hakuna mtaani.Nani atakula chips kuku au mayai?hata mayai trei sasa hivi sh 5500
 
Hawa ni kuku wa kisasa eeh? Badili fuga wa kienyeji unatafuna mpaka mifupa
 
wafugaji wameongezeka
kila mtu anataka afanye biashara sasaivi kuongeza kipato
 
Hakuna pesa inayopatika kiulaini changamoto lazima ziwepo, nilitaka kusema kwa habari chanjo kwa kuku ni changamoto unaweza kuwachanja harafu wakafa hii hutokana huifadhi wa chanjo, chanjo inahifadhiwa kwenye ubaridi na tunajua changamoto ya umeme mara nyingi tunauziwa chanjo ambazo zishakufa kuwa mdadisi sana, kuwa makini sana kwenje ununuzi wa chanjo wiki iliyopita rafiki yangu kapata hasara ya kuku 200 akafuatwa muuzaji wa chajo anaomba msamaha na maelezomengi. Ninachota uelewe chanjo zake azikuexpire ila zilikufa kwa uhifadhi mbaya.
 
Back
Top Bottom