Mafuta ya kupikia yaadimika mitaani

Mafuta ya kupikia yaadimika mitaani

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Kuna watu wanamhujumu Mheshimiwa Rais na pengine yeye hajui hili. Kwa sasa huku mitaani mafuta ni adimu sana, na pale ambapo yanapatikana basi bei yake haishikiki. Dumu/Ndoo ya Lita 20 iliyokua ikiuzwa TZS 70,000/- mwezi wa sita mwaka jana leo inauzwa TZS 140,000/-

Aliekua Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda alipata kusema kua sababu ya kupanda huku ni kuadimika Kwa vibarua huko Malaysia sababu ya COVID-19. Kigoma inaongoza Tanzania Kwa kuzalisha chikichi, je wameweza kuchukua mazao yote yanayozalishwa pale mpaka yakaisha imebidi waagize Malaysia sasa?

Kwanini wasi encourage na ku facilitate kilimo hiki Kwa hapa Tanzania mpaka tulazimike kuagiza nje? Singida wanalima sana Alizeti, na mikoa ya kusini wanalima sana Ufuta, je mazao haya yamechukuliwa yote na bado kukawa na upungufu wa mafuta?

Haya maeneo (Singida na Mikoa ya Kusini) bado kuna mapori mengi tu, kama wanazalisha malighafi za mafuta na bado hazitoshi kwanini Serikali isiwawezeshe basi kuongeza zaidi maeneo ya kulima kwenye hayo mapori yaliyobaki ili kuongeza zaidi malighafi hizi?

Sasa kuna Hussein Bashe kwenye hii Wizara, nilidhani ni mtu Smart lakin naona nae mfumo umemmeza, amesha adopt tabia za mfumo alioko. Juzi nimemsikia akiwa mkali kweli kweli juu ya kupanda Kwa mbolea kutoka 108,000/- Kwa gunia mpaka 140,000/-, lakini nimkumbushe tu hata hiyo 108,000/- bado tunapigwa, kwani hapo kabla ilikua haizidi 60,000/-

Mafuta Sasa hayako tena mitaani, wenye vigenge/duka wanasema Kwa yalivyopanda bei hata wakiyaleta hawajui watauzaje. Mafuta yanagusa kila mtu, isije ikawa ni bomu linategwa kwenye most consumable products ili likilipuka liguse sehemu kubwa ya watu. Zama hizi za "Kazi Iendelee" tunashuhudia mfumuko mkubwa wa Bei.
 
Si mnamshabikia Putin?

Tanzania inazalisha 45%ya mahitaji yake ya mafuta ya kula na huagiza 55% toka Malaysia, India na Uturuki.

Duniani mzalishaji mkubwa wa mafuta ni Ukraine, sasa baada ya uvamizi wa Urusi, Ukraine amestop uzalisha na Rassia anaemfuatia amewekewa vikwazo hivyo mafuta ya Uturuki saivi yanaenda ulaya na ya Malaysia yanaenda Japan na Korea ili kuziba pengo la mafuta ya Urusi na Ukraine ambapo hayapo sokoni. Na Korea na Japan wananunua Bei nzuri kuliko sisi

Mungu ajalie mvua Ifike mwezi wa 4 nivune alizeti yangu ni jenge.
 
Hatuna watunga sera wazuri;
Kwa ukubwa wa ardhi ya Tanzania; serikali inashindwa kutengeneza mazingira bora kwa wakuli wa mazao muhimu kama alizeti na chikichi kwa ajili ya uzalishani wa mafuta ya kula?
Wizara imejaa maandiko na mipango lakini hakuna utekelezaji. Kila siku ni maneno ya ''tutafanya'' na wala husikii waziri wa kilimo akisema ''tumefanya''
Tunaishi tu bila mipango endelevu.

Lakini wanasiasa hawaishi kusema kuwa tunajitosheleza.

Tumekabidhi hatma ya taifa kwa watu wasio na mipango ila wana maneno mengi mazuri.

KIla kinachotokea duniani kinaongeza ugumu wa maisha kwa mtanzania.
 
Tupo vizuri ndugu zangu tutatumia nazi kupikia ubwabwa na rosti la kuku
 
Nchi kama malaysia walijikita kwenye kilimo cha chikichi ambapo mbegu walitoa kigoma, leo hii wana export kwenye soko la dunia mafuta ya chikichi kama hawana akili nzuri, pale kigoma waha wanazubaa na michikichi yao..........bongo kufanya initiatives zenye maslahi mapana na ya kudumu ni mtihani.
 
Alizeti ya singida na kwingineko haitoshi tuu kutumika katika uzalishaji/ matumizi ya nchi.

Mawese ya kigoma na kwingine neko viwanda vya kuprocess kupata mafuta safi bongo ni havipo ah vichache. Kuna kiwanda kilijaribu hawakufanikiwa kutengeneza katika viwango( harufu na kuganda)

Pamba ambayo ingeweza tupa mafuta na rahisi kuzalisha nayo bodi ya pambana imechangia kuua kilimo chake. Kilimo cha kutegemea mvua pia. Tuombe isije anzishwa bodi ya zao la mawese au alizeti tutakwisha
 
Nchi kama malaysia walijikita kwenye kilimo cha chikichi ambapo mbegu walitoa kigoma, leo hii wana export kwenye soko la dunia mafuta ya chikichi kama hawana akili nzuri, pale kigoma waha wanazubaa na michikichi yao..........bongo kufanya initiatives zenye maslahi mapana na ya kudumu ni mtihani.

Tatizo pia serikali yetu si wezeshi linapokuja swala la kuplan kwa ajili ya muda mrefu utasikia sera sera za miaka 20 lakini hakuna cha maana.

Tuweze niche ndogo za kilimo tuwatoe wanaolima hekari chache kua wakulima wa hekari nyingi.
 
Back
Top Bottom