Mafuta ya Safi na Korie yanatokana na Alizeti gani inayoganda?

Kaunara

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2013
Posts
249
Reaction score
452
Habari za mda huu!

Naenda kwenye mada fupi tu. Nimetaja mafuta hayo sababu common sana kwa wengi wetu. Ila kuna mafuta mengi yapo mtaani ambayo yanaganda.

Na uhakika wa haya mafuta kuwa yanaganda kwa asilimia 100. Na mafuta haya hutengenezwa na alizeti kwa mujibu wa watengenezaji, ila ukweli hamna mafuta ya alizeti yanayoganda. Pia mafuta mengi ya mimea huwa hayagandi.

Mafuta yanayoganda ni ya wanyama ambayo ni hatari sana kwa mlaji. Sasa nauliza hata kama ni wanyama wanapata wapi kiasi kingi hivi? Au ni ya nyangumi? Haya nimawazo yangu ila natamani sana kujua haya mafuta yanatokana na nini?
 
Kumbuka ni viwanda vya wahindi miongoni mwao wako kwenye mpango wa kuimaliza ngozi nyeusi, tafuta kuna uzi wa Mshana Jr humu
 
nilinunua hayo mafuta wanadai n alizeti ahsee nimekaa nayo kama mwez ivi nakuta kweny kidum yameganda yote kama baraf vile
Nikaon nigawe tu Maan duh hata kuyamimina kutok kweny dumu n kazi yan mpka uyaanike ahse!
 
Kwanza sijui kuhusu Safi ila Korie sio Alizeti....! Ila navyojua mafuta mengi wanaagiza na kuja kupaki kwene vibebeo tu hapa nchini so SIO ALIZETI..!
 
Serikali ifanye mchakato wa kuzalisha mafuta hapa hapa nchini haya mambo ya kuagiza mafuta ya kupikia wakati tuna alizeti na mawese ya kutosha ni miyeyusho matokeo yake binti mdogo anaonekana kama mshangazi.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…