Magereza yatumike kurekebisha tabia za Wafungwa sio kuadhibu pekee

Magereza yatumike kurekebisha tabia za Wafungwa sio kuadhibu pekee

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Wakuu, salaam, kuna mambo nimewaza hapa kuhusu Idara zetu za Magereza. Binafsi sikutarajia kuona au kusikia Wanaotoka Gerezani wakihusika na matukio ya uhalifu mitaani kwa sababu naamini moja ya kazi ya Magereza ni kurekebisha tabia za wahalifu na kuwafanya kuwa watu wema baada ya kutoka kifungoni.

Sasa kama Idara ya Magereza inatekeleza suala la urekebishaji Tabia, kwa nini bado wanaotoka kwa msamaha au kumaliza vifungo wanaendelea na uhalifu mitaani hata baada ya kukaa muda mrefu kifungoni?. Tafsiri ya haraka ni kuwa Magereza yetu yamejikita kwenye kuadhibu zaidi kuliko kubadili wafungwa kuwa watu wema.

Na hili linadhihirika wazi hawafanyi jambo hilo kupitia kauli ya Rais Samia aliyoitoa kwa Jeshi la Magereza August 29, 2022 Rais Samia: Magereza mrekebishe tabia za wahalifu

Nadhani Idara ya Magereza na Serikali ziweke msisitizo katika kuwarekebisha Wafungwa zaidi kuliko kuwapa adhabu pekee kwa sababu adhabu hazibadili tabia zaidi ya kuumiza na ndio sababu wengi wakitoka wanarudia uhalifu.
 
Magereza yamekua kama Jehanamu Wafugwa&Mahabusu wanateseka adhabu kali na kazi nzito bila chakula na malazi ya uhakika Wafugwa wakiumwa hawapati matibabu hadi vidonda vinaoza askari.
 
Tatizo siyo la magereza peke yake ambao wanapaswa kulalamikiwa kuhusu tabia za wahalifu kurudi gerezani. Jamii nzima inao wajibu wa kushughulikia na hilo jambo kwani malezi ya jamii, mitazamo ya jamii na hali za kijamii pia. Mtu anamaliza kifungo watu(jamii) ina mtazama kama mkosefu wa jumla. Kwa jamii zetu hatuna kitu kiitwacho "second chance" na huwa tunaamini mhalifu always ni mhalifu.
Na mara amalizapo kifungo watu ambao ni wafariji wakwanza kwake ni wale walio na mawazo yake kwani kwa utafiti mdogo inaonekana
 
Back
Top Bottom