Maggid Mjengwa: Wazee wa Dar es Salaam ni akina nani na wana sifa zipi?

Kwa lugha nyepesi isiyo na kificho, kulingana na muandishi, wazee wa dar lazime wawe ni wawe ni wanaume wa kiislamu, wacheza bao na wasio na elimu ya kutosha
ni kweli lakini hivi kwa yanayoendelea huoni upuuzi unaofanywa na hao unaowamini kuwa ni wasomi?
 
Kama Wazee wa Dar huwa wanapata heshima ya kupiga story na Rais. Nawashauri wanawake waache kuwasema vibaya wanaume wa Dar maana wanapokuja kuzeeka huwa na heshima kubwa kwa viongozi wa nchi.
 
Sasa ulitaka na wale wa chadema wenye kushangilia ushoga nao wawemo?

Hiyo haikubaliki

Hata wakialikwa wao watawaza kumuangusha raisi na hayo ndio mawazo yao.
Hivi ni chama gani chenye katibu wa itikadi na uenezi mwenye tuhuma ya kuolewa mombasa?
 
Raisi wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan leo anaongea na wazee wa DSM

Niwakumbushe tu wazee wa DSM huu utaratibu ulikuwepo toka mwaka 1957 wakati TANU inazaliwa na kutafuta uhuru.

Wazee hawa kila mara walimuita kijana wao Nyerere kumpa miongozi namna ya kupambana na mkoloni na wengine walikuwa na ukwasi wa hela walikuwa hata wanampa msaada wa kipesa.

Kwenye picha hapo chini hao ni wazee wa DSM mwaka 1957 ninao wakumbuka hapo ni Mshumi Kiyate huyu mzee alikuwa ni mvuvi ndio alikiwa anasaidai familia ya Nyerere wakati alivyoacha kazi vile hakuwa na mshahara.

Siku moja alikutana na Nyerere pale fire akampa shillingi 200 wakati huo Nyerere anaishi Magomeni ili akailishe familia yake. Kumbuka shilling 200 ya wakati ule ulikuwa unaweza kujenga nyumba ya miti ya vyumba vitano.

Mwingine ni Jumbe Tambaza,Dossa Azizi,Suleiman Takadiri,Chaurembo,na wenginewe.

Utaratibu huu umekuwa ukiendelea hadi sasa maraisi wengi wanautumia utaratibu huu swali kwanini wazee wa Dar tu mkoani je.Jibu ni kuwa vuguvugu la kugombea uhuru lilianzia Dar ni vigumu kila mkoa raisi kwenda kuongea na wazee hawa wazee wa dar wanawakilisha wazee wa mikoani.

Ila ninachojiuliza kuwa mzee wa dar kuna kitambulisho au vipi maana sio kila mzee atakwenda huko.

Mama naona amefanya vizuri maana hao wazee hata yeye kwa umri wake ni baba zake

Namtakia hongera na maongezi mema

 
Existence of "Wazee wa mkoa" is it a something progressive? I mean do we have to expect "Wazee wa mkoa " after 50years. If its a progressive, Ni kwa namna gani somebody can became one of them?
 
Leo Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mh. Rais Samia Suluhu Hassan anatarajia kuongea na wazee wa Mkoa wa Dar es salaam. Tayari Rais ameshawasili Dar na bila shaka maandalizi yanaendelea. Ni kawaida kwa viongozi kufanya mazungumzo na makundi ya watu ama taasisi, utaratibu huu umekuwa desturi ya muda mrefu, japokuwa ni maarufu sana kwa viongozi kufanya vikao ama mazungumzo na wazee wa Dar es salaam.

Sio jambo geni kusikia kiongozi fulani, Rais ama Mkuu wa mkoa siku fulani atafanya mazungumzo na wazee wa mkoa wa Dar es salaam. Kabla ya leo siku zote niliamini utaratibu huu ni wa kawaida kwa kiongozi kufanya hivyo pale anapotaka kupata busara za wazee wa eneo lake analohudumu ama eneo ambalo makao yake yalipo, yaani mfano kwa Marais walikuwa wakiongea na wazee wa Dar kwakuwa IKULU ipo ndani ya Mkoa wa Dar. Sasa awamu hii jambo lipo tofauti kidogo japo si sana, sasa kwa tofauti hiyo ndogo imenifanya nitake kudadisi zaidi kuhusu hawa wazee wa Dar.

Naam! Hoja iko hivi, Rais aliyepita (JPM)alifanikiwa kuhamishia makazi ya serikali Dodoma. Na sasa Rais Samia anahudumu Nchi akiwa Dodoma ispokuwa pale tu anapokuja Dar. Sasa dhana ya kuongea na wazee niliamini huenda ingekuwa na mantiki kubwa zaidi kama ingekuwa Dodoma ambako ndiko yaliko makao rasmi ya Rais kuliko sehemu nyingine yoyote kwa sasa.

Au labda kuna nini cha mno kuhusu hawa wa kuitwa wazee wa Dar es salaam kiasi cha kumlazimu Rais kusafiri kuja Dar kuongea nao? Mbona kila mara wazee wa Dar.... Wazee wa Dar???
 
Ni rahisi kuwakusanya pamoja katika wingi wao. Ujumbe unawahusu wazee wa TZ, wao ni ishara tu.
 
Wazee wa Dar ni tunu kwani maarifa mengi na wameona mengi na pia wana weledi.
 
wa mkoani wapo busy na kilimo
wa mjini wanasubiri kodi hivyo wana muda mwingi
 
Wakati Mh.Rais anasema Atakutana na Wazee wa Mkoa wa Dar es salaam kwa Niaba ya Wazee wa Nchi nzima Binafsi niliamini Suala la ITIKADI za KISIASA halitakuwepo.Nimeshangaa na Kuona Mkutano wa Jana ni kama Uliandaliwa KICCM zaidi kuliko KISERIKALI.

Niliamini tunaposema Wazee Wangetafutwa Wazee kutoka Vyama vyote na kama Ingefaa kutoka Mikoa yote ili kuwawakilisha Wazee wenzao.

Kama Jana kulikuwa na Wazee 1000 na Tanzania ina Mikoa 30 basi Kila Mkoa ungetuma Wazee 35 na bila kuchagua Wazee wa Chama kimoja. Pia kama ule Mkutano ulikuwa wa Mh.Rais na Sio Mwenyekiti wa CCM basi Utitiri wa Viongozi wa CCM haukupaswa kuwepo.Mh Rais hebu tutoe kwenye siasa sana ili tuwe Wamoja Vinginevyo Ungeitwa Mkutano wa Mwenyekiti wa CCM na Wazee wa Ccm Mkoa wa DSM.
 
Huyu Mzee Tabu Mangala hakika Mungu alimjalia hekima na maono ya hali ya juu.

Ushauri aliompa Nyerere hakika ndio maisha yetu halisimtaani hadi hivi leo, wengi tuna madaftari ya mkopo kwenye maduka ya Mangi na Wapemba, hakika wanatustiri watu hawa, ukitaka kujuwa siri zetu waulize hawa Mangi na mpemba kama vile siku hizi ukitaka kujuwa siri za dada zetu wewe waulize bodaboda wa mtaani kwake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…