Magoli 10 ya kufungwa katika mechi mbili,Simba inabaki vipi kama ilivyo?

πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”
 
Ndio kila timu inafungwa lakini siyo goli 10 kwa mechi 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkitwaa ilo kombe nakun*ya iringa mbeya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli ligi yetu sio bora.Hata pale mwaka 2003 simba ile ya Siang'a(Rip) ilipowatoa mabingwa watetezi Zamalek ligi yetu bado haikuwa bora!

Proffesional aliyekuwepo Simba kipindi kile ni Ramadhani Wasso pekee (kama sikosei).Kwa hiyo kukosekana proffesionals sahihi haiwezi pia kuwa sababu ya kufungwa 5 bila mechi mbili mfululizo ugenini.

Soura,timu ya Algeria ambayo simba iliwafunga 3 bila hapa Dar,wamekataa kufungwa na AS Vita (ugenini) na Al Ahly (nyumbani).Na wala simba isitegemee mteremko huko Algeria kwakuwa Soura wamejifunza makosa yao.

Pamoja na udhaifu wa soka letu ambalo wengi mmeliongelea.Pamoja na upungufu tulionao kama taifa kwenye mipango yetu ya mpira kuanzia kwenye grassroots...lakini kwa vipigo hivi vya simba hatuwezi kujificha kwenye sababu hizihizi za kila siku.Game approach.....Unapocheza na timu iliyokuzidi uwezo inabidi kuiheshimu tu na kucheza kwa tahadhari huku ukiviziazizia kushambulia.Simba hawajafanya hivyo mechi zote mbili za Vita na Ahly....Wanaenda kwenye mchezo as if wapo level moja na hizo timu.Kosa kubwa sana na ndomana wanapigwa vipigo vya ajabu..Ingewezekana kabisa kufungwa kwa heshima au hata kutoa sare kwenye hizo mechi mbili kama tu kocha wa simba angekuwa na approach sahihi na kuwatumia wachezaji sahihi kwenye hiyo approach.Kukomaa na 4-4-2 huku una Kagere na Okwi mbele,na Chama akicheza nyuma yao ni dhahiri hutaki kujilinda...ni kama unaenda kucheza na Mwadui tu!Hata ukiwapa majukumu ya kukaba hawa watu hawawezi...

Alikuwa ana option bora zaidi ya kuweka viungo watano na mshambuliaji mmoja tu ambaye anatumika kwenye counter akisaidiwa na Chama ambaye atakuwa anaunganisha kiungo na ushambuliaji na kusaidia attacking mnapokuwa na mpira.Kagere angeanzia benchi nafasi angechukua kiungo mkabaji labda Mzamiru na kucheza 4-5-1 mbele Okwi pekee.Hapa priority inakuwa ni kuwazuia waarabu wasikufunge na wala sio kushindana nao kufunga!Mkiwazuia dakika 45 wasifunge hata wao wanakuja a bit frustrated kipindi cha pili na watakuja wamechemka na mnaweza kutumia hiyo advantage kufanya counters kadhaa kipindi cha pili.Kwa kufanya hivi hata mkipoteza mchezo haiwezi kuwa kwa mabao mengi hivyo na ambayo yanawaharibia psychology wachezaji wenu.Na mnajiweka vibaya zaidi kwenye kundi kuruhusu magoli mengi itakapotokea mmelingana points!

Kocha akubali kuwa amekosea kwenye game plan na ajirekebishe kuliko kuanza kutoa visingizio vya ajabu eti sijui simba haina wachezaji wakuweza kucompete kimataifa!Angekataa hiyo kazi in the first place mpaka simba ipate hao wachezaji wa kimataifa anaowaongelea..Kukubali kukiongoza kikosi cha simba kwenye michuano hii ni uthibitisho kuwa aliridhika na kikosi....akubali makosa yake tusonge mbele,asilete blablaaa......
 
Kwa maelezo yako unakubaliana na shafii kuwa simba ni underdog
 
Hawa professional tunaokoteza tu ndugu, hatujawa makini na mashindano haya,
 
Spurs alimfunga Wigan 9 ndani ya dakika 90.. Man U alimfunga Arsenal 8 ndani ya dakika 90.

Ni mpira gani nyie huwa mnaangalia?
Kibaya ni timu kushindwa kukaba wkt hawana uwezo wa kushinda, sio mbaya tujifunze
 
Wa Misri wananunua wachezaji kutoka EPL, simba wananunua wachezaji kutoka Lipuli fc halafu mnataka matokeo mazuri like serious?
 
Kiongozi, thamani ya vikosi vya Vita na Simba kuwa karibia sawa sawa, lakini Vita kuwa juu, inaonyesha ligi ya Congo ni bora kuliko ya kwetu.
Ufumbuzi ni mmoja tu. Tuumize vichwa kuboresha ligi yetu iwe na ushindani wa kutosha.
Mkuu wenzetu wacongo kwao ni njaa kali na maisha ni magumu ndyo maana wachezaji wao wakipata nafasi ya kuchezea hizi timu kubwa wanajituma kweli kweli kwa sababu wanajua nje ya hpo mtaani hakukaliki na akizembea tu namba inachukuliwa na mwenye njaa zaidi tofauti na bongo mchezaji hta akipigwa benchi anapewa posho elfu themanini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenzetu walipoingia Makundi wakafanya usajii wa kufa mtu,Simba wanamchukuea Zana ambaye amekaa miezi sita bila kucheza,leo tena wanaleta wachezaji wa kuwafanyia majaribio,kweli?.

Juzi tena wamemsajili Mchezaji wa Timu ya Ndanda ,Vitalis Mayanga kutoka timu inayoshika nafasi ya 17 kwenye msimamo wa Ligi yetu ili akafanye maajabu gani Ligi ya Mabingwa Afrika wakati hata Mapinduzi Cup hajawahi kucheza kama si utani ni nini jamani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…