Magori utulize wenge lako, kama mnamtafuta mchawi anza na bosi wako kisha wewe mwenyewe maana ndiyo mshauri wake

Magori utulize wenge lako, kama mnamtafuta mchawi anza na bosi wako kisha wewe mwenyewe maana ndiyo mshauri wake

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Nimeona bwana Crescentius Magori ametweet kwamba wamesalitiwa kwenye mechi ya leo na inaonekana kuna baadhi ya wachezaji wataangushiwa jumba bovu muda si mrefu kuwa wameisaliti timu.

Kitu ambacho bwana Magori na viongozi wenzake awataki kukubali ukweli kwamba timu waliyonayo kwa sasa ni tofauti na ile ya msimu uliopita, na bado wameuza Chama na Miquisone wakashindwa kutafuta wachezaji wa maana wakaenda kusajili wachezaji wa gharama nafuu ili wawatengeneze badae wawauze tena.

Sasa kwa mfumo huo ambao wanaenda nao simba kwa sasa ni ngumu kuupata tena ubora wake, leo Magori anasema wamesalitiwa lakini hapo hapo yule Babra alisema Manara ndio alikuwa msaliti akamuondoa ina maana hiyo timu kwa sasa imejaa wasaliti.

Timu imeonekana haijiwezi kuanzia mechi za ndani, sisi tunaojua mpira tulikuwa tunasema ni suala la muda tu simba itakata moto na ndicho kinachotokea msianze kuwaangushia jumba bovu wachezaji wakati timu iko hoi aieleweki inacheza mfumo gani uwanjani ni ilimradi tu bora liende!

Mnaposimamisha wachezaji na nyie viongozi mjitafakari
 
Sasa Magori anataka nini kama sio mitafaruku klabuni. Mambo ya ajabu sana, bodi ina wao wenyewe walioafiki kuwauza key players bila kuandaa mibadala yao.

Wakamuuza Chama kinafiki nafiki bila kuwataarifu mashabiki. Wakasajili akina Banda kwa mihemko, na mbaya zaidi wakatutengenezea mazingira kwa kushirikiana na mashabiki wa utopolo kumpamba Banda kuwa yanga wanammezea mate.

Banda ukiangalia uchezaji wake ni bora ya calinhos wa yanga, dogo hakabi ila kazi kupoteza mipira akajikuta anampa kazi nzito sana Kapombe na mashambulizi yakazidi upande wetu. Wakae bodi wahukumiane wao kwa wao kwa usajili wa kingese walioufanya.

Sasa wao wanajiweka pembeni wanatupa lawama kwa wachezaji ambao wao wenyewe ndiyo waliowasajili.

Mimi saa nyingine huwa nawaangalia Yanga hasa viongozi wao kama Eng Hersi, hanaga mambo ya kupanic kindezi ndezi, wakipoteza wanakaa wanapanga mikakati yao bila kelele na sasa wanakuja polepole huku wakiimalika, lakini sisi utaona kwanzia Dewji na kila kiongozi ni kuja na mihasira isiyo na maana.

Sasa hii ndo nini wakati tuna mechi dhidi ya polisi tena tarehe 27 na ni mechi dume pia. Tushukamane ku focus ubingwa wa ligi na kuangalia namna ya kusogea mbali shirikisho hizi lawama zinakuja kututoa relini
 
Japo mimi ni shabiki wa yanga ila Mechi ya leo benchi la ufundi ndio limezingua. Kocha anabeba lawama moja kwa moja

Why afanye sub half time huku timu inacheza vizuri. Kama timu inacheza vizuri why ufanye sub?

Pia hakuwa anawakumbusha wachezaji wake wasi relax

Simba leo wamefungwa magoli 3 yote kipindi cha pili.

Goli la kwanza naweza sema ni bahati mbaya.

Goli la pili ni uzembe tupu na lilipaswa liwe wake up call kwa wachezaji wa simba uwanjani wajue wanakaribia kutolewa wabadili mbinu ama wawe serious.

Ila hawakubadili mbinu wala kuwa serious waliendeleza uzembe uzembe mpaka wanafungwa goli la 3.

Kwa mtu yeyote anaejua mpira huwa anajua timu yoyote ikirudisha magoli mawili huwa inapata nguvu ya kutafuta goli la 3 na hata la 4. Simba walipaswa wajipange baada ya kufungwa goli la 2 tu maana lile lilikuwa ni dalili ya kuonesha goli la 3 linakuja
 
Ukishaona mapenzi na ushkaji kazini ujue hapo hakuna kazi ie mudy kamweka mskaji wake kuwa mwenyekiti wa bodi alafu mchepuko ndio mtendaji mkuu wa timu Chama aliuzwa kutokana na kutokukubaliana na namna utatuzi wa mgogoro wa mtendaji mkuu na msemaji
 
Kocha yupo jukwani mnategemea mshinde magoli au njaa?
 
Ule ni uzembe, Simba kuna wachezaji wasiojitambua na Manula akiwa miongoni mwao, lazima uchunguzi ufanyike naunga mkono hili 100%
 
Back
Top Bottom