Elections 2015 Magufuli akutana na nguvu ya Umma Mbeya, azomewa, aambiwa wanamtaka Lowassa

Elections 2015 Magufuli akutana na nguvu ya Umma Mbeya, azomewa, aambiwa wanamtaka Lowassa

Mkuu,hao watu wa Magufuri mtaani hawapo pengine Lumumba tu.CCM mnategemea kukusanya watu kwa mara kutoka huku na kule ili mkutano uwe na watu.Hamuwezi kupata vijana hao kutoka sehemu moja.
Pia tambua ni tabia ya Magufuri kufanya mikutano ya barabarani walichofanya ni kumueleza tu kuwa hawamtaki aendelee na safari yake,hakuna hata jiwe wala chupa iliyorushwa mkuu.

Eti mikutano ya barabarani bora wameonyesha hisia zao.
 
ACT mnaendeleaje na kampeni?

Punguza mapovu....

Wako nyuma yangu wanafanya mikutano yao ya hadhara kunadi m-bunge na madiwani wao. Nikiwahesabu hawazidi 21 na vitoto ndio vingi kwani leo J'pili. Wamekodi vyombo vya matangazo na wanasikika vizuri sana. Wanachonishangaza toka waanze hotuba zao ni kuinanga ukawa haswa chadema na viongozi wao kuanzia taifa hadi diwani ni kuonyesha chuki tu mara ccm 'b' mara waelezee ufisadi na mapungufu ya mgombea uraisi wa ukawa yaani wanasahau kujieleza hata wenyewe na sifa zao na kujiombea kura.Yaonekana kuna semina kali walipewa ya kuwakashfu ukawa kwenye mikutano yote watakayoifanya.
 
Ustaarabu wako kamfunze kwanza Msukuma,

Baada ya jana Vincent kumjibu Msukuma kuwa mzee pusher ana mkono wa sweta leo mko kimya hata hamgusii matusi yenu.

Acheni kulialia dawa ya moto haijawa maji hata siku moja ni moto.
Kuna watu wana matusi humu JF kama Bavicha? Labda waambie wanaojiunga leo JF.
 
Kuiba ni dhambi lakini siasa zinazoweka maisha ya watu hatiani ni dhambi zaidi. Sasa mwizi na mtu anaependa siasa za fujo wakikutana ndio dhambi kubwa kwa bwana godi na sheria za nchi zinatueleza.

Nakushauri achana UKAWA kwa sasa jamaa ni hatari kwa taifa; tumia akili tu wala si kingine. Magufuli analengo la kuwanyoosha wote.

Mkuu Eric kuliko niwe ccm bora niwe maiti
 
bavicha bana sasa hapo nguvu ya ipo wapi hao wahuni wachache wanaopiga kelele?

Wapiga kura wametulia majumbani hawana fujo.

Endeleeni kujifariji mtakimbia humu baada ya uchaguzi.

mabadiliko
 
Ccm mmezoea kuwa vijana huwa hawaendi kupiga kura, Safari hii tunaenda kupiga lazma mtoke tu..
 
Hiyo siyo nguvu ya umma ila ni uhuni.

Uhuni mtu yeyote akiamua anaweza kuufaya, lakini matokeo yake ni kuvujika kwa amani.

Kama wao wameshaamua kuwa wanamtaka Lowassa nini kinawapeleka kwenye mkutano wa Magufuli?

Inaonekana kabisa kuwa kuna kundi lililojiandaa kufanya fujo na walishaandaa camera wapige hii picha ya video.

Ukawa badala ya kuchekelea vitu kama hivi inabidi mvikemee kwa sabau watanzania hawapendi vurugu, hawatamchagua mtu anayeandaa vikundi vya vurugu.

Afute kwanza kauli alioita Geita ya kutaka wagombea wa UKAWA wakirudi tena Geita wazomewe
 
# hapa ni kazi tu. Achana na warundi wenye majungu,umbea na fujo. Wamegawa chama kizuri kwa fisi. Mfungwa anaangalia mtu sio chama.

Kweli wewe ulivyo jitambulisha kuwa mfungwa ni kweli akili yako imefungwa haiwezi kufikiri kwa mapana na marefu na unapaswa kuondoa akili yako kifungoni.Badilika uwe huru kifikra.
 
Yeye ndo aliwaambia wananchi wamzomeee sasa limemgeukia na hata sahahu siku ya leo
 
Uwongo wenu mwisho October 25. Leo magufuli yupo Iringa wilaya ya Mufindi pole Sana kajipange upya

Kabla ya kuja huko,alikuwepo Mbarali na alitokea Mbeya uwanja wa ndege,nipo Mbarali na nilienda kumsikiliza,mkutano wake Mbarali ilikuwa iwe tar 30 but wameurudisha nyuma na umefanyika leo.
 
Hilo la ugonjwa liko wazi wala si kumvunjia heshima Lowassa anaumwa.

Tukio la duni ni recently na kikubwa wananchi walitaka kusikia hoja sio matusi aliyoyaanzisha kwa CCM, either way sikubaliani na kuzomewa kwake sio ustaarabu hila viongozi wa CCM wamekuwa wakisema sana kwa wanachama wao kuacha kuzomea watu na kueshimu maamuzi ya wengine sijasikia UKAWA wakitoa matamshi ya aina hiyo tangia uchaguzi uanze.

kule geita kufuli alivyosema lowassa akirudi azomewe ulikuwa ustaarabu? kuhusu maradhi kumbuka hujafa hujaumbika, huenda ukatangulia kabla ya lowassa ata kesho, hujui siku yako.

View attachment 291841
 
Naziona siku 27 ngumu za kampeni. Naomba tuvumiliane, hivi nini kitatokea kama wafuasi wa CCM nao wakianza kuvuruga utulivu wa mikutano ya Lowasa kwa kuzomea?

Hivi usikii?? CCM wameshavuruga kampeni za Lowassa mnoo. Masaburi Dar kuwandaa vjn waandamane.msukuma kusema hadharani Lowassa kajinyea Bulembo kusema ccm haitaruhusu upinzani kwenda Ikulu kauli gani hizi? Si uchochezi huo? Mkuki kwa nguruwe. Lkn nakuhakikishia huyu msukuma alichosema kitawakosesha ccm kura haki yanani
 
Kuna watu wana matusi humu JF kama Bavicha? Labda waambie wanaojiunga leo JF.

Mkuu, kwenye jukwaa la complaints kuna thread vijana wa bavicha wakishirikiana na nyumbu wa ulipo tupo wanalalamika picha za Magufuli kuwekwa kwenye thread wanazoanzisha.

Cha kushangaza, watu haohao ndio wanaunga mkono wahuni kuvamia mikutano ya kampeni na kufanya fujo.

Hizi zote ni dalili za kushindwa. Watu wanaojiandaa kuchukua serikali hawawezi kufanya uhuni kama huu.
 
Halafu hizo video ndizo zinaonesha ni kwa namna gani UKIWA inaungwa mkono na watu wasiojitambua....
Sanduku la kura halina lebo kwamba anayejitambua aweke huku na asiyejitambua aweke kule!! what we need is changes.
 
Naziona siku 27 ngumu za kampeni. Naomba tuvumiliane, hivi nini kitatokea kama wafuasi wa CCM nao wakianza kuvuruga utulivu wa mikutano ya Lowasa kwa kuzomea?

ccm haina wafuasi, wasanii ndio wenye wafuasi. watu wanaenda fiesta. sasa hao wafuasi unaosema ni wa ccm ni kina nani? labda mnunue
 
Ha ha ha kwi kwi kwi akomeege kabisa vp NATAMAN AJE UWANJI KUOMBA KURA KAMA HAJATEGUKA MIGUUUU
 
Mkuu, kwenye jukwaa la complaints kuna thread vijana wa bavicha wakishirikiana na nyumbu wa ulipo tupo wanalalamika picha za Magufuli kuwekwa kwenye thread wanazoanzisha.

Cha kushangaza, watu haohao ndio wanaunga mkono wahuni kuvamia mikutano ya kampeni na kufanya fujo.

Hizi zote ni dalili za kushindwa. Watu wanaojiandaa kuchukua serikali hawawezi kufanya uhuni kama huu.
Wenyewe ndiyo mabingwa wa kulalamika lakini upuuzi wanaofanya wanaita nguvu ya umma.

Kwa akili yao wanadhani JF ni mali ya Chadema.

Wakati JF ni jukwaa huru wapo wenye vyama na wasiyokuwa na vyama.
 
Back
Top Bottom