Elections 2015 Magufuli akutana na nguvu ya Umma Mbeya, azomewa, aambiwa wanamtaka Lowassa

Elections 2015 Magufuli akutana na nguvu ya Umma Mbeya, azomewa, aambiwa wanamtaka Lowassa

Hapo mi Sijaona fujo hapo ni kumsaidia ndugu yetu magufuli kwamba hanachakuwaeleza Hao mabwana asipoteze nguvu zake achape lapa
 
hiv mnadhan CCM wao hawawez mzomea lowasa? hiyo n dalili ya kushindwa, mmekubali kushindwa mapema mmeanz akuzomea, haya wenye timamu hatuzomea tutampa kura huyo huyo 25 oct.....
Wataanzaje kumzomea wakati hata hao wana ccm maelfu kwa maelfu wanamkubali Lowassa
 
leo asubui Magufuli wakati akipita mbeya
kakutana na zomea zomea
eneo la mwanjelwa na uyole
kuna wana ccm walipangwa wamzuie ili ionekane wananchi wamemsimamisha azungumze
kibao kikageuka watu wakaanza kukimbia nakuanza kumzomea
ccm acheni maigizo leo yamewaponza

Mahala pengine Zomea zomea katika siasa ni silaha pekee ya mtu aliyeshindwa na ambaye siku zote kakata tamaa jambo ambalo ni tofauti sana kwa mji wetu wa mwanjelwa kwani wao wanashida ya kukosa uvumilivu wa hata kufikia hatua ya kutotoa nafasi sawa na haki ya upande mmoja, mfano kuchana nguo, mabango, na mambo mengine yanayoashiria uelewa mdogo kwenye siasa na hata ktk michezo kwani tumekuwa pia tukishuhudia ushabiki wa prison Vs mbeya city na hili limekuwa likichangiwa zaidi na hata aina ya viongozi tunaowapata kwa ngazi takribani zote kutokuwa taa kwa jamii kama vile tunavyoshuhudia uropokaji, na ushuhuda fitinishi majukwaani kana kwamba baada ya uchaguzi hakuna maisha tena
 
leo asubui Magufuli wakati akipita mbeya
kakutana na zomea zomea
eneo la mwanjelwa na uyole
kuna wana ccm walipangwa wamzuie ili ionekane wananchi wamemsimamisha azungumze
kibao kikageuka watu wakaanza kukimbia nakuanza kumzomea
ccm acheni maigizo leo yamewaponza

Ahahahaha naona mnajitekenya na kucheka wenyewe.... Mbona unaandika kama umekalia jiko la gesi?
 
sasa kuzomea hivyo ndo kushinda hata akili hamna hivi kama magufuri akaingia madarakani alafu hao walokua wanamzomea watasemaje acheni upumbavu kuzomea mtu ambae hata ujui kama atashinda au hatoshinda koo hao wanaozomea wamijiaminisha kabisa kura zao ndo zitamfanya lowassa ashinde alafu utaendaje kwa mtu ambae wewe humtaki ukaenze kumzomea ukipigwa na police unaanza kulalamika ooh police wanatuonea wakati umeyataka mwenyewe
 
Dodoma, Livingstone Lusinde
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imejadili kwa kina suala la kupanda kwa gharama za maisha nchini. NEC inakiri kwamba ni kweli lipo tatizo la kupanda kwa gharama za maisha nchini.

Tatizo hili pia limezikumba karibu nchi nyingi za Afrika Mashariki na kwakweli karibu sasa lipo dunia nzima.

Baadhi ya sababu za kupanda kwa gharama za maisha hapa nchini ni pamoja na;

1. Hali mbaya ya mavuno inayotokana na uhaba wa mvua au mvua kunyesha kipindi cha nje ya msimu katika maeneo mengi nchini.
2. Kuongezeka kwa bei ya mafuta duniani, hivyo kuongezeka kwa gharama za uzalishaji wa bidhaa na usafirishaji wa mazao.
3. Kuyumba kwa thamani ya dola ya Marekani.
4. Kuwepo kwa soko huria ambapo sasa mazao ya chakula yanapata soko nje ya nchi, na wakati mwingine kuuzwa nje kwa njia ya magendo na hivyo kusababisha uwepo wa ukubwa wa mahitaji na hivyo kuongezeka kwa bei ya chakula nchini.
5. kuongezeka kwa walaji wakati uzalishaji ukiwa mdogo.
6. kutofanikiwa (ikiwemo kuhujumiwa na wafanyabiashara wasio waaminifu) kwa baadhi ya mikakati ya kudhibiti mfumko wa bei.

Uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa.

1. Pamoja na Serikali kuendelea kuchukua hatua za muda mrefu na wa kati za kukabiliana na tatizo hili, CCM inaiagiza Serikali kuchukua hatua za haraka za muda mfupi ikiwemo kuangalia upya baadhi ya kodi katika vyakula pamoja na kodi ya ongezeko la thamani VAT katika sukari.

2. Utaratibu wa ruzuku ya mbegu na mbolea upanuliwe ili kunufaisha wakulima wengi.

3. Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa mpango wake wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi chakula nchini, hasa kwa kupitia Hifadhi ya Nafaka ya Taifa, ikiwa ni pamoja na kujenga maghala zaidi ya mazao ya chakula katika maeneo ya uzalishaji wa mazao, na kutenga fedha nyingi zaidi kwa ununuzi wa mazao hayo. Pamoja na hili, mipango ifanywe kuongeza uwezo wa wakulima kuhifadhi chakula chao wenyewe na kupunguza upotevu baada ya mavuno (post-harvest losses).

3. Serikali iendelee kupanua utaratibu wake wa kutumia Hifadhi ya Nafaka ya Taifa (SGR) kama nyenzo ya kudhibiti kupanda kwa bei za vyakula. Wakati wa uhaba wa vyakula katika maeneo ya mijini, kasi ya kupeleka chakula maeneo hayo iongezwe na utaratibu mzuri zaidi wa usambazaji wa chakula utumike ili walaji, na sio wasafirishaji na wasindikaji, wanufaike.

4. Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya kilimo nchini, hasa ASDP na SAGCOT, ambayo itasaidia kumaliza tatizo la chakula nchini na kuongeza ajira na kipato kwa Watanzania walio wengi.

5. Serikali idhibiti malipo ya huduma ya ndani kwa kutumia fedha za kigeni, hasa dola za kimarekani. Aidha, Serikali iongeze udhibiti wa Maduka na mahoteli yanayofanya biashara ya fedha za kigeni ili kuondoa hujuma kwa uchumi wa nchi inayofanywa kutokana na uhuru uliokithiri katika biashara hii.

6. Waajiri wahimizwe kupandisha mishahara na malipo mengineyo kwa wafanyakazi wao ili waweze kumudu gharama za maisha.

7. Serikali iweke jitihada zaidi za kudh ibiti ulanguzi wa bidhaa muhimu na upandishaji holela wa bei za vyakula, kodi za nyumba na usafiri.


Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary
Posted by CCM Blog
CCM mnadhani tatizo la kilimo chetu na wakulima kukosa Ruzuku?Mnadhani tatizo la mfumuko wa bei ni kutokana na wakulima wetu na wafanyabiashara wetu kupeleka mazao ya kilimo nje kihalali au kwa Magendo? Tatizo kubwa ni viongozi wetu kuwa wafanyabiashara/kuwa wawekezaji katika sector mbalimbali za nchi yetu ndo tatizo?nani hataki biashara yake ipate faida kubwa kwa kuuza bidhaa zake kwa bei ya juu?
 
Hiyo siyo nguvu ya umma ila ni uhuni.

Uhuni mtu yeyote akiamua anaweza kuufaya, lakini matokeo yake ni kuvujika kwa amani.

Kama wao wameshaamua kuwa wanamtaka Lowassa nini kinawapeleka kwenye mkutano wa Magufuli?

Inaonekana kabisa kuwa kuna kundi lililojiandaa kufanya fujo na walishaandaa camera wapige hii picha ya video.

Ukawa badala ya kuchekelea vitu kama hivi inabidi mvikemee kwa sabau watanzania hawapendi vurugu, hawatamchagua mtu anayeandaa vikundi vya vurugu.

Kama wali interfere huo ni uhuni na haikubaliki. Napenda mqbadiliko lakini uhuni haukubaliki! Lakini kama walitumia ujanja ujanja kuhadaa watu kuwa walisimamisha msafara ili wamsikilize ndo wameumbuka.

Yote kwa yote tuwe wastaarabu!
 
Natamani uchaguzi ufanyike leo, Tumweke LOWASSA, halafu tuendelee na mambo yetu!

....mkuu naumia sana nikiona Lowassa anaelekea kushinda halafu watu wanahujumu haki ya watanzania kwa maslahi yao binafsi....
 
Back
Top Bottom