Magufuli aliahidi kuboresha mafao ya Wafanyakazi. Badala yake kavuruga maslahi yao, na ametumia fedha za mafao yao kujipaisha zaidi

Magufuli aliahidi kuboresha mafao ya Wafanyakazi. Badala yake kavuruga maslahi yao, na ametumia fedha za mafao yao kujipaisha zaidi

Moja ya simulizi za kusikitisha katika utawala wa awamu ya Tano, ni kisa cha wafanyakazi wa Tanzania. Zipo kada nyingi zilizoumizwa sana na utawala huu, mojawapo nyingine ni wakulima. Hawa wote wametumika kama nyenzo tu ya kufanikisha miradi ya awamu hii, huku wao wenyewe na familia zao wakiachwa kwenye mateso na lindi la ufukara. Nachelea kusema kinachofanyika kinakaribia mfumo wa utumwa haswa.

John Joseph Pombe Magufuli, wakati anajinadi 2015, aliahidi, kati ya ahadi nyingi, kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Na baada ya bajeti yake ya kwanza, alitamka kwamba ataanza kuyaboresha "baada ya mwezi mmoja au miwili", akidai kwamba haiwezekani kuboresha maslahi kabla ya kukamilisha zoezi la kuhakiki WAFANYAKAZI HEWA. Hilo lilionekana ni busara iliyo wazi kabisa. Wafanyakazi wakavuta subira.

Kusema kweli uhakiki ulifanyika, watu walihakikiwa zaidivya mara 4, lakini mishahara haikupanda, ila bei mbalimbali na gharama za maisha, ziliendelea kupanda.

Miezi haigandi, ikasonga mbele, ukawa mwaka, na zaidi. Baada ya kuachana na kisingizio cha uhakiki wa wafanyakazi, Serikali ya JPM ikabuni kibwagizo kingine: maboresho ya wafanyakazi yapo ndani ya maboresho ya maisha ya watanzania wote. Barabara zinazojengwa, ujenzi wa reli ya SGR, mradi mkubwa wa umeme wa Stigler, fly over, ununuzi wa ndege, na mengine mengi.

JPM aliridhishwa sana na hoja hii, kiasi kwamba baada ya hapo, akisikia kilio cha kuboresha maslahi ya wafanyakazi, alikuwa anajibu kwa ukali: kama unaona mshahara hautoshi, nenda kalime! Hapo JPM aliridhika kabisa kwamba ametekeleza ahadi yake ya kuboresha maslahi yavwafanyakazi.

Na kwa kweli, kuna wakati aliahidi kwamba kabla ya kumaliza awamu hii ya miaka 5, atatekeleza ahadi yake. Mpaka hivi sasa keshavunja bunge, kwa hiyo keshawahadaa wafanyakazi kwa mara nyingine.

Inafaa kukumbuka kwamba kama mishahara ya wafanyakazi haiongezwi, basi maana yake vipato vyao vinashuka, kwa sababu gharama za maisha zimepanda sana kipindi cha Magufuli, ili kugharimia miradi mingi aliyoianzisha bila kuzingatia uwiano katika sera za uchumi. Kwa hiyo maana yake ni kwamba kiuhalisia, badala ya kuboresha maslahi ya wafanyakazi, ameyadunisha kwa kiwango kikubwa sana. Hii ni pamoja na maisha ya watanzania wote kwa ujumla wao, wamefukarishwa zaidi.

Lakini Magufuli hakuishia hapo katika mradi wake mkubwa wa kufukarisha wafanyakazi. Ameingilia pia Mafao na Pensheni za wafanyakazi wastaafu, na kuzipiga.

Mbali ya kurithi madeni ya serikali, ambapo serikali ilikopa toka mashirika ya hifadhi za jamii, Magufuli badala ya kupunguza madeni hayo, ameyaongeza zaidi na zaidi.

Ili kuficha " uporaji" huu, serikali ya JPM imetumia njia kadhaa, hapa nitaje njia mbili: kwanza kuunganisha mashirika. Hapa kuna manufaa mengi kwa serikali. Kwanza kujipatia muda zaidi kwa kisingizio cha " mchakato", pili "uhakiki", na kuficha udhaifu wa mashirika yaliyokuwa hoi zaidi kutokana na uporaji huo wa serikali.

Pili ni kwa "kurekebisha" vikokotoo.

Matokeo yake, wafanyakazi wengi hivi sasa wanacheleweshewa mafao yao na Pensheni.

Miaka ya hivi karibuni kulikuwa na uboreshaji mkubwa katika utendaji wa mashirika ya hifadhi ya jamii, na kuwezesha wafanyakazi wanaostaafu kulipwa mafao yao mapema. Magufuli badala ya kuboresha zaidi alipoachia Kikwete, ndio amezidi kuvuruga zaidi.

Hapo juu nimetumia neno "UPORAJI" badala ya "UKOPAJI" kwa sababu, mstaafu halipwi pensheni ya kila mwezi, mpaka hapo atakapolipwa mafao yake. Hebu fikiria mtu katumikia miaka yote hiyo, anastaafu, hapati malipo yoyote mwezi baada ya mwezi. Kama atalipwa mafao baada ya miaka 2, maana yake muda wote huu hana kipato chochote. Kwa kuzingatia mstaafu ni mtu mwenye umri mkubwa, ana hatari ya magonjwa nyemelezi kibao, mateso kama haya hayawaachi salama baadhi yao wanafariki bila kupokea malipo yao. Na hata kama hajafariki, atakuwa ameathirika sana, yeye na wategemezi wake, kiasi hata akija kulipwa hayo mafao, kuna athari ambazo hazitawezekana kuponeshwa.
Hapo hakuna uporaji kweli?

Kwa hiyo JPM amewanyima wafanyakazi ile nafuu aliyowaahidi, badala ya kuwapa mkate akawapa UPUPU.

Pia hata kile kidogo kilichohifadhiwa kwa ajili yao wanapostaafu, amekipora pia.

Magufuli hakuishia hapo.
1) kwa mujibu wa sheria, mfanyakazi ana haki ya kupata nyongeza za kila mwaka (increments ) ambazo humwezesha kupanda ngazi za mshahara na madaraja. Miaka yote hii haijawahi kuingiliwa, inaweza kusimama kwa muda tu lakini si kwa kiwango cha wakati wa Magufuli. Katika awamu ya Magufuli, increment imegeuzwa kuwa hisani ya rais, na inatangazwa kwa mbwembwe. Hii ni enzi ya utumwa haswa.

2) Licha ya increments, kuna nyongeza za mishahara za jumla. Hizi Magufuli ndio kabisaaa kafutilia mbali. Hizi zilisaidia sana kuongeza kiwango cha mshahara kinachotumika kukokotoa malipo ya mafao. Ndio kimbilio pekee kwa wale wafanyakazi waliofika kwenye "bar".

3) Kuna kituko au tuseme UMAFIA umefanywa na serikali hii haijawahi kutokea. Mfanyakazi anapata barua ya kupandishwa daraja kwa mujibu wa taratibu. Maana yake mshahara pia unapanda. Tuseme anaambiwa kapandishwa kuanzia tarehe mosi Julai 2017. Baadae analetewa barua mshahara utapanda kuanzia Novemba mosi 2017. Baadae tena anaambiwa atalipwa kuanzia Julai Mosi 2018. Danadana hizo zinaweza kuendelezwa bila kikomo, kuna ambao mpaka leo hawajaonja mshahara mpya, kwa mtindo huo.

Ni wazi Magufuli ameona wafanyakazi ni Mgodi wa kuutumia kutekeleza miradi yake ili kujiletea sifa kubwa, kwa gharama ya wafanyakazi .

Tusisahau kwamba wafanyakazi ni chanzo kikubwa cha makusanyo ta kodi, tena cha uhakika. Serikali inajipigia panga yenyewe bila mjadala wala makadirio.

Tumesikia Rais Magufuli katika ziara hivi karibuni akiwajibu wafanyakazi , kama unaona mshahara hautoshi, nenda kalime. Siku chache Baadae akiongea na walimu, aliwaahidi kulipa mafao yao yote wanaodai, kufikia mwezi wa 8. Swali, hakuwajibu waende kulima. Je, hiyo ni kwa walimu tu? Au wafanyakazi wastaafu wote? Na kama ni walimu tu, kawatenga kwenye kundi la wanaoteswa, ili iweje? UCHAGUZI MKUU 2020?
Acheni kulalamika sana. Kama mnaona hafai jitokezeni kwa wingi kwenye sanduku la kura mumkatae na kumchagua mtu mwingine
 
Tutafute mtawala ambae siyo muongo na awe mkweli. Uchaguzi umefika.
 
Rais anafanya mazur lkn hapo naona alijisahau anapaswa kukumbushwa na wasaidizi wake badala ya kumuimbia mapambio
Baba mwenye watoto hata uwe na maghorofa 10 lakini watoto kila siku wanakula ugali mrenda hakuna haja ya kuwa na hayo maghorofa.
 
Hakuna Mfanyakazi mwenye akili timamu kichwani mwake anaweza kumfagilia Magufuli kwa chochote kile. Mimi binafsi nikimuona tu kwenye tv, faster nabadili channel. Maana namuona hana msaada wala faida yoyote ile kwangu.

Haiwezekani niishi kwa mshahara ule ule tangu enzi za JK halafu eti mtu aniambie tuna Rais! Labda aseme tuna RAHISI! ila siyo Rais.
 
Kiuchumi ukiona watumishi mishahara haiongezeki maana yake ni kuwa hata mtaani hali ya uchumi lazima iwe mbaya,hiyo ni kanuni ya uchumi-maana matumizi makubwa ya serikali ni kupitia mishahara na miradi.
Kwa bahati mbaya kwa Tanzania Miradi yote mikubwa wakandarasai wanatoka nje hivyo mapato yake nayo yanaenda nje.kwa hiyo njia pekee ambayo hela inaweza kupatikana mtaani ni kupitia mishahara.
By the way,haya mambo yalimuondoa mbunge wetu kipenzi aliyokuwa akitetea masilahi ya watumishi mule bungeni.Upumzike rafiki wa kweli Kasuku Bilago aliyekuwa mbunge wa Kankonko.
 
Moja ya simulizi za kusikitisha katika utawala wa awamu ya Tano, ni kisa cha wafanyakazi wa Tanzania. Zipo kada nyingi zilizoumizwa sana na utawala huu, mojawapo nyingine ni wakulima. Hawa wote wametumika kama nyenzo tu ya kufanikisha miradi ya awamu hii, huku wao wenyewe na familia zao wakiachwa kwenye mateso na lindi la ufukara. Nachelea kusema kinachofanyika kinakaribia mfumo wa utumwa haswa.

John Joseph Pombe Magufuli, wakati anajinadi 2015, aliahidi, kati ya ahadi nyingi, kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Na baada ya bajeti yake ya kwanza, alitamka kwamba ataanza kuyaboresha "baada ya mwezi mmoja au miwili", akidai kwamba haiwezekani kuboresha maslahi kabla ya kukamilisha zoezi la kuhakiki WAFANYAKAZI HEWA. Hilo lilionekana ni busara iliyo wazi kabisa. Wafanyakazi wakavuta subira.

Kusema kweli uhakiki ulifanyika, watu walihakikiwa zaidivya mara 4, lakini mishahara haikupanda, ila bei mbalimbali na gharama za maisha, ziliendelea kupanda.

Miezi haigandi, ikasonga mbele, ukawa mwaka, na zaidi. Baada ya kuachana na kisingizio cha uhakiki wa wafanyakazi, Serikali ya JPM ikabuni kibwagizo kingine: maboresho ya wafanyakazi yapo ndani ya maboresho ya maisha ya watanzania wote. Barabara zinazojengwa, ujenzi wa reli ya SGR, mradi mkubwa wa umeme wa Stigler, fly over, ununuzi wa ndege, na mengine mengi.

JPM aliridhishwa sana na hoja hii, kiasi kwamba baada ya hapo, akisikia kilio cha kuboresha maslahi ya wafanyakazi, alikuwa anajibu kwa ukali: kama unaona mshahara hautoshi, nenda kalime! Hapo JPM aliridhika kabisa kwamba ametekeleza ahadi yake ya kuboresha maslahi yavwafanyakazi.

Na kwa kweli, kuna wakati aliahidi kwamba kabla ya kumaliza awamu hii ya miaka 5, atatekeleza ahadi yake. Mpaka hivi sasa keshavunja bunge, kwa hiyo keshawahadaa wafanyakazi kwa mara nyingine.

Inafaa kukumbuka kwamba kama mishahara ya wafanyakazi haiongezwi, basi maana yake vipato vyao vinashuka, kwa sababu gharama za maisha zimepanda sana kipindi cha Magufuli, ili kugharimia miradi mingi aliyoianzisha bila kuzingatia uwiano katika sera za uchumi. Kwa hiyo maana yake ni kwamba kiuhalisia, badala ya kuboresha maslahi ya wafanyakazi, ameyadunisha kwa kiwango kikubwa sana. Hii ni pamoja na maisha ya watanzania wote kwa ujumla wao, wamefukarishwa zaidi.

Lakini Magufuli hakuishia hapo katika mradi wake mkubwa wa kufukarisha wafanyakazi. Ameingilia pia Mafao na Pensheni za wafanyakazi wastaafu, na kuzipiga.

Mbali ya kurithi madeni ya serikali, ambapo serikali ilikopa toka mashirika ya hifadhi za jamii, Magufuli badala ya kupunguza madeni hayo, ameyaongeza zaidi na zaidi.

Ili kuficha " uporaji" huu, serikali ya JPM imetumia njia kadhaa, hapa nitaje njia mbili: kwanza kuunganisha mashirika. Hapa kuna manufaa mengi kwa serikali. Kwanza kujipatia muda zaidi kwa kisingizio cha " mchakato", pili "uhakiki", na kuficha udhaifu wa mashirika yaliyokuwa hoi zaidi kutokana na uporaji huo wa serikali.

Pili ni kwa "kurekebisha" vikokotoo.

Matokeo yake, wafanyakazi wengi hivi sasa wanacheleweshewa mafao yao na Pensheni.

Miaka ya hivi karibuni kulikuwa na uboreshaji mkubwa katika utendaji wa mashirika ya hifadhi ya jamii, na kuwezesha wafanyakazi wanaostaafu kulipwa mafao yao mapema. Magufuli badala ya kuboresha zaidi alipoachia Kikwete, ndio amezidi kuvuruga zaidi.

Hapo juu nimetumia neno "UPORAJI" badala ya "UKOPAJI" kwa sababu, mstaafu halipwi pensheni ya kila mwezi, mpaka hapo atakapolipwa mafao yake. Hebu fikiria mtu katumikia miaka yote hiyo, anastaafu, hapati malipo yoyote mwezi baada ya mwezi. Kama atalipwa mafao baada ya miaka 2, maana yake muda wote huu hana kipato chochote. Kwa kuzingatia mstaafu ni mtu mwenye umri mkubwa, ana hatari ya magonjwa nyemelezi kibao, mateso kama haya hayawaachi salama baadhi yao wanafariki bila kupokea malipo yao. Na hata kama hajafariki, atakuwa ameathirika sana, yeye na wategemezi wake, kiasi hata akija kulipwa hayo mafao, kuna athari ambazo hazitawezekana kuponeshwa.
Hapo hakuna uporaji kweli?

Kwa hiyo JPM amewanyima wafanyakazi ile nafuu aliyowaahidi, badala ya kuwapa mkate akawapa UPUPU.

Pia hata kile kidogo kilichohifadhiwa kwa ajili yao wanapostaafu, amekipora pia.

Magufuli hakuishia hapo.
1) kwa mujibu wa sheria, mfanyakazi ana haki ya kupata nyongeza za kila mwaka (increments ) ambazo humwezesha kupanda ngazi za mshahara na madaraja. Miaka yote hii haijawahi kuingiliwa, inaweza kusimama kwa muda tu lakini si kwa kiwango cha wakati wa Magufuli. Katika awamu ya Magufuli, increment imegeuzwa kuwa hisani ya rais, na inatangazwa kwa mbwembwe. Hii ni enzi ya utumwa haswa.

2) Licha ya increments, kuna nyongeza za mishahara za jumla. Hizi Magufuli ndio kabisaaa kafutilia mbali. Hizi zilisaidia sana kuongeza kiwango cha mshahara kinachotumika kukokotoa malipo ya mafao. Ndio kimbilio pekee kwa wale wafanyakazi waliofika kwenye "bar".

3) Kuna kituko au tuseme UMAFIA umefanywa na serikali hii haijawahi kutokea. Mfanyakazi anapata barua ya kupandishwa daraja kwa mujibu wa taratibu. Maana yake mshahara pia unapanda. Tuseme anaambiwa kapandishwa kuanzia tarehe mosi Julai 2017. Baadae analetewa barua mshahara utapanda kuanzia Novemba mosi 2017. Baadae tena anaambiwa atalipwa kuanzia Julai Mosi 2018. Danadana hizo zinaweza kuendelezwa bila kikomo, kuna ambao mpaka leo hawajaonja mshahara mpya, kwa mtindo huo.

Ni wazi Magufuli ameona wafanyakazi ni Mgodi wa kuutumia kutekeleza miradi yake ili kujiletea sifa kubwa, kwa gharama ya wafanyakazi .

Tusisahau kwamba wafanyakazi ni chanzo kikubwa cha makusanyo ta kodi, tena cha uhakika. Serikali inajipigia panga yenyewe bila mjadala wala makadirio.

Tumesikia Rais Magufuli katika ziara hivi karibuni akiwajibu wafanyakazi , kama unaona mshahara hautoshi, nenda kalime. Siku chache Baadae akiongea na walimu, aliwaahidi kulipa mafao yao yote wanaodai, kufikia mwezi wa 8. Swali, hakuwajibu waende kulima. Je, hiyo ni kwa walimu tu? Au wafanyakazi wastaafu wote? Na kama ni walimu tu, kawatenga kwenye kundi la wanaoteswa, ili iweje? UCHAGUZI MKUU 2020?

Posti bora ya wakati wote hiii
 
Moja ya simulizi za kusikitisha katika utawala wa awamu ya Tano, ni kisa cha wafanyakazi wa Tanzania. Zipo kada nyingi zilizoumizwa sana na utawala huu, mojawapo nyingine ni wakulima. Hawa wote wametumika kama nyenzo tu ya kufanikisha miradi ya awamu hii, huku wao wenyewe na familia zao wakiachwa kwenye mateso na lindi la ufukara. Nachelea kusema kinachofanyika kinakaribia mfumo wa utumwa haswa.

John Joseph Pombe Magufuli, wakati anajinadi 2015, aliahidi, kati ya ahadi nyingi, kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Na baada ya bajeti yake ya kwanza, alitamka kwamba ataanza kuyaboresha "baada ya mwezi mmoja au miwili", akidai kwamba haiwezekani kuboresha maslahi kabla ya kukamilisha zoezi la kuhakiki WAFANYAKAZI HEWA. Hilo lilionekana ni busara iliyo wazi kabisa. Wafanyakazi wakavuta subira.

Kusema kweli uhakiki ulifanyika, watu walihakikiwa zaidivya mara 4, lakini mishahara haikupanda, ila bei mbalimbali na gharama za maisha, ziliendelea kupanda.

Miezi haigandi, ikasonga mbele, ukawa mwaka, na zaidi. Baada ya kuachana na kisingizio cha uhakiki wa wafanyakazi, Serikali ya JPM ikabuni kibwagizo kingine: maboresho ya wafanyakazi yapo ndani ya maboresho ya maisha ya watanzania wote. Barabara zinazojengwa, ujenzi wa reli ya SGR, mradi mkubwa wa umeme wa Stigler, fly over, ununuzi wa ndege, na mengine mengi.

JPM aliridhishwa sana na hoja hii, kiasi kwamba baada ya hapo, akisikia kilio cha kuboresha maslahi ya wafanyakazi, alikuwa anajibu kwa ukali: kama unaona mshahara hautoshi, nenda kalime! Hapo JPM aliridhika kabisa kwamba ametekeleza ahadi yake ya kuboresha maslahi yavwafanyakazi.

Na kwa kweli, kuna wakati aliahidi kwamba kabla ya kumaliza awamu hii ya miaka 5, atatekeleza ahadi yake. Mpaka hivi sasa keshavunja bunge, kwa hiyo keshawahadaa wafanyakazi kwa mara nyingine.

Inafaa kukumbuka kwamba kama mishahara ya wafanyakazi haiongezwi, basi maana yake vipato vyao vinashuka, kwa sababu gharama za maisha zimepanda sana kipindi cha Magufuli, ili kugharimia miradi mingi aliyoianzisha bila kuzingatia uwiano katika sera za uchumi. Kwa hiyo maana yake ni kwamba kiuhalisia, badala ya kuboresha maslahi ya wafanyakazi, ameyadunisha kwa kiwango kikubwa sana. Hii ni pamoja na maisha ya watanzania wote kwa ujumla wao, wamefukarishwa zaidi.

Lakini Magufuli hakuishia hapo katika mradi wake mkubwa wa kufukarisha wafanyakazi. Ameingilia pia Mafao na Pensheni za wafanyakazi wastaafu, na kuzipiga.

Mbali ya kurithi madeni ya serikali, ambapo serikali ilikopa toka mashirika ya hifadhi za jamii, Magufuli badala ya kupunguza madeni hayo, ameyaongeza zaidi na zaidi.

Ili kuficha " uporaji" huu, serikali ya JPM imetumia njia kadhaa, hapa nitaje njia mbili: kwanza kuunganisha mashirika. Hapa kuna manufaa mengi kwa serikali. Kwanza kujipatia muda zaidi kwa kisingizio cha " mchakato", pili "uhakiki", na kuficha udhaifu wa mashirika yaliyokuwa hoi zaidi kutokana na uporaji huo wa serikali.

Pili ni kwa "kurekebisha" vikokotoo.

Matokeo yake, wafanyakazi wengi hivi sasa wanacheleweshewa mafao yao na Pensheni.

Miaka ya hivi karibuni kulikuwa na uboreshaji mkubwa katika utendaji wa mashirika ya hifadhi ya jamii, na kuwezesha wafanyakazi wanaostaafu kulipwa mafao yao mapema. Magufuli badala ya kuboresha zaidi alipoachia Kikwete, ndio amezidi kuvuruga zaidi.

Hapo juu nimetumia neno "UPORAJI" badala ya "UKOPAJI" kwa sababu, mstaafu halipwi pensheni ya kila mwezi, mpaka hapo atakapolipwa mafao yake. Hebu fikiria mtu katumikia miaka yote hiyo, anastaafu, hapati malipo yoyote mwezi baada ya mwezi. Kama atalipwa mafao baada ya miaka 2, maana yake muda wote huu hana kipato chochote. Kwa kuzingatia mstaafu ni mtu mwenye umri mkubwa, ana hatari ya magonjwa nyemelezi kibao, mateso kama haya hayawaachi salama baadhi yao wanafariki bila kupokea malipo yao. Na hata kama hajafariki, atakuwa ameathirika sana, yeye na wategemezi wake, kiasi hata akija kulipwa hayo mafao, kuna athari ambazo hazitawezekana kuponeshwa.
Hapo hakuna uporaji kweli?

Kwa hiyo JPM amewanyima wafanyakazi ile nafuu aliyowaahidi, badala ya kuwapa mkate akawapa UPUPU.

Pia hata kile kidogo kilichohifadhiwa kwa ajili yao wanapostaafu, amekipora pia.

Magufuli hakuishia hapo.
1) kwa mujibu wa sheria, mfanyakazi ana haki ya kupata nyongeza za kila mwaka (increments ) ambazo humwezesha kupanda ngazi za mshahara na madaraja. Miaka yote hii haijawahi kuingiliwa, inaweza kusimama kwa muda tu lakini si kwa kiwango cha wakati wa Magufuli. Katika awamu ya Magufuli, increment imegeuzwa kuwa hisani ya rais, na inatangazwa kwa mbwembwe. Hii ni enzi ya utumwa haswa.

2) Licha ya increments, kuna nyongeza za mishahara za jumla. Hizi Magufuli ndio kabisaaa kafutilia mbali. Hizi zilisaidia sana kuongeza kiwango cha mshahara kinachotumika kukokotoa malipo ya mafao. Ndio kimbilio pekee kwa wale wafanyakazi waliofika kwenye "bar".

3) Kuna kituko au tuseme UMAFIA umefanywa na serikali hii haijawahi kutokea. Mfanyakazi anapata barua ya kupandishwa daraja kwa mujibu wa taratibu. Maana yake mshahara pia unapanda. Tuseme anaambiwa kapandishwa kuanzia tarehe mosi Julai 2017. Baadae analetewa barua mshahara utapanda kuanzia Novemba mosi 2017. Baadae tena anaambiwa atalipwa kuanzia Julai Mosi 2018. Danadana hizo zinaweza kuendelezwa bila kikomo, kuna ambao mpaka leo hawajaonja mshahara mpya, kwa mtindo huo.

Ni wazi Magufuli ameona wafanyakazi ni Mgodi wa kuutumia kutekeleza miradi yake ili kujiletea sifa kubwa, kwa gharama ya wafanyakazi .

Tusisahau kwamba wafanyakazi ni chanzo kikubwa cha makusanyo ta kodi, tena cha uhakika. Serikali inajipigia panga yenyewe bila mjadala wala makadirio.

Tumesikia Rais Magufuli katika ziara hivi karibuni akiwajibu wafanyakazi , kama unaona mshahara hautoshi, nenda kalime. Siku chache Baadae akiongea na walimu, aliwaahidi kulipa mafao yao yote wanaodai, kufikia mwezi wa 8. Swali, hakuwajibu waende kulima. Je, hiyo ni kwa walimu tu? Au wafanyakazi wastaafu wote? Na kama ni walimu tu, kawatenga kwenye kundi la wanaoteswa, ili iweje? UCHAGUZI MKUU 2020?
Kama ni mpira una zako 3 points
Tatizo lipo hasa kwa waalimu hao watumishi wengine maisha yao angalau, yaani hiyo majuzi hapo Dodoma pambio na sifa kwenda kwa bw. Yule wacha wakome
 
Mateso bila chuki, utawala wa ovyo kabisa
Hali yetu wafanyakazi tulio punguzwa kazi ni ngumu kila siku yupo PSSSF lakini madai hayatolewi na tuna magonjwa nyemelezi kama kisukari, shinikizo la damu nk.sisi tumefungua madai yangu mwaka jana mwezi 12 lakini hakuna anayejali mapaka sasa tunahali ngumu ,labda hizo pesa hatatuzipata mpaka tumefika kaburini.
Majibu tunayopewa hayaridhishi kabisa,mtu unaumwa unaambiwa mpaka ufikishe umri wa kustaafu ndiyo upewe pesa yako.
 
Wazee Wastaafu wanasotea mafao yao mwaka wa 2 huu
Mifuko ukianza kudai inakuwa na visingizio mara mwajiri haijaleta michango yako miezi 3 imemiss kwahiyo ngoja tufuatilie! Kwani walikuwa wapi kufuatilia kabla ya mfafanya kazi hajaacha kazi ? Wameajiriwa kwa kazi ya kufuatilia michango ya mwanachama lakini wanasubiri uanze kudai mafao ndiyo wanakuambia tufuatilie mafao kwanza,nayo ni njia ya kuchelewesha malipo ya mwanachama
Pili wafanyakazi. wengi wa mifuko hawataki kutoa namba zao za simu wanataka kila siku wewe uende ofisini na ukifika unaambiwa neno lile lile kuwa tunashughulikia jibu ambalo lingeweza kujibiwa kwa simu
 
Acheni kulalamika sana. Kama mnaona hafai jitokezeni kwa wingi kwenye sanduku la kura mumkatae na kumchagua mtu mwingine
Eti watu proffesional hawalipi mafao yao mpaka wastaaafu ,ambapo mikataba yao imeisha na kazi hawana wasubiri tu mpaka wafikishe miaka 60 kwa sababu ni proffesional!! Watakula hiyo proffesional yao mpaka wafikishe miaka 60?
Wawape basi kazi wafanye kazi mpaka wafikishe hiyo miaka wanayotaka wao
 
Eti watu proffesional hawalipi mafao yao mpaka wastaaafu ,ambapo mikataba yao imeisha na kazi hawana wasubiri tu mpaka wafikishe miaka 60 kwa sababu ni proffesional!! Watakula hiyo proffesional yao mpaka wafikishe miaka 60?
Wawape basi kazi wafanye kazi mpaka wafikishe hiyo miaka wanayotaka wao
Chukua hatua
 
Ni hatari Sana ,

Sana....
Masikitiko haya Ni kila Kona, kila pembe ya nchi...

Hata hivyo udhaifu wa TUCTA kwa kukubali kununuliwa ndio unaleta hata yote
 
Hali yetu wafanyakazi tulio punguzwa kazi ni ngumu kila siku yupo PSSSF lakini madai hayatolewi na tuna magonjwa nyemelezi kama kisukari, shinikizo la damu nk.sisi tumefungua madai yangu mwaka jana mwezi 12 lakini hakuna anayejali mapaka sasa tunahali ngumu ,labda hizo pesa hatatuzipata mpaka tumefika kaburini.
Majibu tunayopewa hayaridhishi kabisa,mtu unaumwa unaambiwa mpaka ufikishe umri wa kustaafu ndiyo upewe pesa yako.
Pole sana mkuu, hela yako lakin unapangiwa jinsi ya kuitumia, so sad
 
Back
Top Bottom