Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Watu wengi wanaweza kuwa wamesahau, wakati Serikali ya awamu ya tano inaingia madarakani ilikuta shirika la umeme nchini(TANESCO) wanakata 7000 kila mwezi kama gharama ya kuhudumia laini. Ilikuwa pesa flani ya mtelezo kwa Serikali na shirika la umeme, 7000 ukizidisha na wateja wote wa kawaida nchini zilikuwa ni pesa nyingi sana. Watu walilalamika kiasi, pitia uzi huu wa 2012: Tujadili makato ya LUKU katika manunuzi ya Umeme (Service Charges). Changamoto ilikuwa kubwa zaidi kwa nyumba ambayo ilibaki tupu kwa muda mrefu.
Pamoja na malalamiko hayo Tanesco ilikuja na ufafanuzi huu; Maelezo kuhusu gharama za huduma "service charge" ambapo ilijitetea ni gharama za kuhudumia laini ikiwemo kukata miti, kubadili nguzo zilizooza na kadhalika.
Mungu si Athumani, April 2016 Serikali kupitia Ewura waliondoa makato ya 'Service Charge' baada ya Tanesco kupeleka maombi ya tozo hiyo kuondolewa ambayo awali waliitetea uwepo wake na hadi sasa tozo hii haikuwahi kurudi. Pia tozo ya aina hiyo iliondolewa na mamlaka ya maji ya Dawasa.
Serikali ya awamu ya sita ilipoingia madarakani March 2021, miezi mitano baadae walitambulisha tozo mpya kupitia mfumo wa umeme wa Luku na tozo hii ilikuwa ni 'Flat rate' kwa kila mita ambapo ilitakiwa kulipa 12,000 kwa mwaka ikiwa ni wastani wa 1,000 kila mwezi. Wadau walilalamika wakidai hii ni tozo kama tozo nyingine zinazotambulishwa awamu ya sita, soma: Kodi ya Jengo au Kodi ya Mita ya LUKU?
Baadae tozo hii ikaanza kubagua majengo ambapo ya ghorofa yalitakiwa kulipa zaidi ambapo kila floor ilitakiwa kulipia 60,000.
Tangu jana vilio vimeanza huku tozo hii ikiwa imeongezwa isivyojulikana, watu wameandikiwa 'debt collected' pesa nyingi na kila mtu akiwa na bei yake. Ni kama Serikali imeamua kutumia luku kukusanyia tozo yao mpya na wanairekebisha karibu kila mwaka, inapoelekea itafika/itazidi 7,000 ambayo ilikuwa inalipwa zamani na tukaipa jina la 'Service Charge' ilhali ya sasa tumeipa jina la 'kodi ya jengo'
Tozo lukuki na mikopo mingi iliyotia fora, Serikali ya awamu ya sita inapeleka wapi fedha zote hizi inazonyonya kwa wananchi wake?
Pamoja na malalamiko hayo Tanesco ilikuja na ufafanuzi huu; Maelezo kuhusu gharama za huduma "service charge" ambapo ilijitetea ni gharama za kuhudumia laini ikiwemo kukata miti, kubadili nguzo zilizooza na kadhalika.
Mungu si Athumani, April 2016 Serikali kupitia Ewura waliondoa makato ya 'Service Charge' baada ya Tanesco kupeleka maombi ya tozo hiyo kuondolewa ambayo awali waliitetea uwepo wake na hadi sasa tozo hii haikuwahi kurudi. Pia tozo ya aina hiyo iliondolewa na mamlaka ya maji ya Dawasa.
Serikali ya awamu ya sita ilipoingia madarakani March 2021, miezi mitano baadae walitambulisha tozo mpya kupitia mfumo wa umeme wa Luku na tozo hii ilikuwa ni 'Flat rate' kwa kila mita ambapo ilitakiwa kulipa 12,000 kwa mwaka ikiwa ni wastani wa 1,000 kila mwezi. Wadau walilalamika wakidai hii ni tozo kama tozo nyingine zinazotambulishwa awamu ya sita, soma: Kodi ya Jengo au Kodi ya Mita ya LUKU?
Baadae tozo hii ikaanza kubagua majengo ambapo ya ghorofa yalitakiwa kulipa zaidi ambapo kila floor ilitakiwa kulipia 60,000.
Tangu jana vilio vimeanza huku tozo hii ikiwa imeongezwa isivyojulikana, watu wameandikiwa 'debt collected' pesa nyingi na kila mtu akiwa na bei yake. Ni kama Serikali imeamua kutumia luku kukusanyia tozo yao mpya na wanairekebisha karibu kila mwaka, inapoelekea itafika/itazidi 7,000 ambayo ilikuwa inalipwa zamani na tukaipa jina la 'Service Charge' ilhali ya sasa tumeipa jina la 'kodi ya jengo'
Tozo lukuki na mikopo mingi iliyotia fora, Serikali ya awamu ya sita inapeleka wapi fedha zote hizi inazonyonya kwa wananchi wake?