Magufuli angekuwepo sio tu vitu vingepanda bei, vingeadimika kabisa

Magufuli angekuwepo sio tu vitu vingepanda bei, vingeadimika kabisa

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Wakuu, kwema

Kama mnavojua kuna inflation kubwa kila nchi duniani nimeweka screenshot chache kuonyesha hilo.

Sasa watu wasioelewa wanasema inflation imesababishwa na Samia na Magufuli angekuwepo bidhaa zingekuwa chini sana

Kanuni ya msingi kabisa kwenye uchumi ni kuwa bei za vitu zinakuwa determined na demand vs supply au uhitaji vs upatikanaji.

So uhitaji wa bidhaa fulani ukiwa mkubwa ila upatikanaji wake ukawa mdogo lazima hiyo bidhaa itapanda tu bei hata rais angekuwa nani

Mfano mavuno ya mahindi mwaka huu yamekuwa kidogo kutokana na ukame lakini uhitaji wa mahindi ni mkubwa, so matokeo yake lazima ni bei ya mahindi kupanda, simple as that

Sasa hebu tuangalie historia ya Magufuli katika ku deal na matatizo ya kiuchumi yalivyokuwa na tutajua kama angeleta unafuu katika hali ya sasa au ndio angeogeza balaa

Sakata la sukari: Kama mnavyokumbuka mwaka 2016 Magufuli kwa papara alipiga marufuku sukari kutoka nje ya nchi, matokeo yake ni sukari kuwa adimu hence bei yake kupanda, ila cha ajabu kwa uelewa mdogo wa Magufuli, alianza kusema wafanyabishara ndio wanafanya hujuma kupandisha sukari na akaagiza sukari kusakwa na jeshi, matokeo yake sukari ikapanda zaidi.

Sakata la korosho: Kuna muda korosho zilinunuliwa kwa bei nzuri sana huko Mtwara, watu wakafaidi, hii ni kwa sababu bei katika soko la dunia ilikuwa nzuri, so hata wafanyabishara watanunua kwa bei nzuri kutoka kwa wakulima, ila misimu uliofuata bei ikashuka, kwenye soko la dunia, so hata wafanyabishara nao wakatoa bei ndogo huku, Magufuli kwa akili zake pia akasema ni wafanyabishara wanamhujumu, akaagiza jeshi kununua korosho wazibangue hata kwa mabomu, matokeo yake ni korosho zile zilishindikana kubanguliwa na zikawa zinaozea kwenye maghala na watu wengi waliporwa korosho zao bila kulipwa.

Sasa kwa mifano hiyo michache tu inaonyesha jinsi gani Magufuli alivyokuwa akifanya vitu kwa impulse, (kwa hasira bila kufikiri)

huyo mtu angekuwa rais kipindi hiki ambacho dunia ina struggle na inflation unajua angefanya situation kuwa mbaya zaidi, pengine angeagiza jeshi lifanye biashara ya mafuta ili yashuke bei.

Screenshot_20220803-192254.png
Screenshot_20220802-080103.png
screenshot_20220721-072018-png.2369426
 

Attachments

  • Screenshot_20220721-072018.png
    Screenshot_20220721-072018.png
    19.5 KB · Views: 24
Kwa watetezi wa Magufuli najua mna hisia kali sana, lakini hebu jaribuni kujibu hoja kwa hoja, sio matusi

Hebu niambieni ni mambo gani Magufuli angefanya au alishafanya ambayo yangeshusha bei za vitu
Wanaongozwa na hisia hasi muda wote akitajwa mzee wa "Intaplinywaa"!Ni vimbwenerehi wanaovaa mavazi ya binadamu.
 
Umeamua kupuuza kabisa umuhimu wa serikali kwenye uchumi wa nchi.

Umeegemea supply na Demand.

Wakati wa Magufuli tulikuwa na nchi ya maziwa na asali.

Mtizamo wako ni assumption tu wala hauna mashiko.

Acha waendelee kulamba asali huku maisha yakiwa magumu kila kukicha.

Swala la Sukali: Ni kweli aliingilia na bei ilipanda lakini badae ilishuka.

Swala la Korosho ilikuwa ni mabadiliko ya sheria yaliyohitaji usimamizi. Wanasiasa wenzako wakaingilia kati, wakawa wananuanua kwa wakulima afu wanaficha na kuichonganisha serikali na wanachi. Badae mambo yalikaa mwenye msitari na maisha yakasonga.

Sasa unambie; Serikali yako ya TOZO, Imefanyia kazi jambo lipi ilikuleta unafuu kwa wananchi?

Kila kitu kimepanda bei na mambo ni magumu mno kwa wananchi.
 
Umeamua kupuuza kabisa umuhimu w serikali kwenye uchumi wa nchi.

Umeegemea supply na Demand.

Wakati wa Magufuli tulikuwa na nchi ya maziwa na asali.

Mtizamo wako ni assumption tu wala hauna mashiko.

Acha waendelee kulamba asali huku maisha yakiwa magumu kila kukicha.
Nchi ya maziwa na asali kwa lipi?
 
Umeamua kupuuza kabisa umuhimu w serikali kwenye uchumi wa nchi.

Umeegemea supply na Demand.

Wakati wa Magufuli tulikuwa na nchi ya maziwa na asali.

Mtizamo wako ni assumption tu wala hauna mashiko.

Acha waendelee kulamba asali huku maisha yakiwa magumu kila kukicha.
Ni situation imebadilika dunia nzima, sio Tanzania tu kwa sababu eti Magufuli kafa
Ni kweli serikali inaweza kushusha kwa kiasi bei za vitu kwa kutoa ruzuku, lakini Magufuli hakuwa na uelewa huu, yeye ilikuwa ni mabavu kwenye kila kitu
 
Naongezea Mama mbali ya mzigo mkubwa miradi mikubwa na kimkakati aliyo rithi kapambana kupata mikopo nafuu na wahisani huko duniani kwa diplomasia ya uchumi.

JPM mbali ya kumaliza kukamua akiba mfano mifuko hifadhi na Watanzania wengine Hadi kufilisika na mauti, alianza kukopa mikopo ya kibiashara kwa riba kubwa!

Angefanya Nini kwa mtetemo huu ulioikumba Dunia?

Tumshukuru Mola kwa yote.
 
Kwa watetezi wa Magufuli najua mna hisia kali sana, lakini hebu jaribuni kujibu hoja kwa hoja, sio matusi

Hebu niambieni ni mambo gani Magufuli angefanya au alishafanya ambayo yangeshusha bei za vitu
Mimi sio mtetezi wa Magufuli, umezunguzia historia ya Magufuli ya nyuma, hujatuambia ni kwa namna gani kwa sasa inflation ingekuwa kubwa kwa sababu ya mafuguli, maana nijuavyo angezuia mahindi kuuzwa nje hii ingesaidia kutopanda na pia angeagiza mafuta kutoka Russia hii ingepunguza ahueni kidogo ya mafuta kuwa juu
 
Huyu Magufuli naanza kuona licha ya kutawala kwa muda mfupi, lakini anaonekana ndie ataongoza kutawala vichwa vya wengi zaidi ya marais waliopita.

Ukiuliza kwanini anasemwa hivi, utajibiwa lazima asemwe kwa mabaya yake, naona wajinga siku hizi wanajificha kwenye kivuli cha ubaya wa Magufuli, ili wao waonekane/wajione watakatifu, huku ni kujidanganya tu.

Magufuli hakuwa malaika, lazima kama mwanadamu wa kawaida alikuwa na mazuri na mabaya yake, lakini kwa baadhi hili hawalioni, wao kwao Magufuli alikuwa ni shetani tu, this is insanity & mental slavery.

Nikitizama vizuri hoja za mleta mada, naona ameamua kulaumu kwa kujua/kutojua, ili aendeleze tu kasumba ya kumsema vibaya Magufuli.

Mfano, anazungumzia sakata la sukari 2016 lililosababisha bei ya bidhaa kupanda, analaumu uamuzi wa Magufuli kuzuia uagizwaji wa sukari toka nje, kwamba huo ndio ulisababisha bei ya sukari kupanda.

Kwangu haya ni mawazo ya mtu anayefikiria kwa upande mmoja tu, tena negatively; kwasababu kama angeamua kufikiria positively ule uamuzi wa Magufuli kuzuia sukari toka nje, naamini angepata jibu zuri tu, kwamba alikuwa ana promote viwanda vyetu vya ndani, na kukuza ajira.
 
Jpm Kwenye utawala wake kumekuwepo na changamoto za hapa na pale na jitihada za kushughulikia zilionekana.

Basi kwa utawala wa mama tungependa kuona jitihada za kushughulikia changamoto mbalimbali zinazojitokeza l.
 
Umeamua kupuuza kabisa umuhimu w serikali kwenye uchumi wa nchi.

Umeegemea supply na Demand.

Wakati wa Magufuli tulikuwa na nchi ya maziwa na asali.

Mtizamo wako ni assumption tu wala hauna mashiko.

Acha waendelee kulamba asali huku maisha yakiwa magumu kila kukicha.


Swala la Sukali: Ni kweli aliingilia na bei ilipanda lakini badae ilishuka.
Swala la Korosho ilikuwa ni mabadiliko ya sheria yaliyohitaji usimamizi. Wanasiasa wenzako wakaingilia kati, wakawa wananuanua kwa wakulima afu wanaficha na kuichonganisha serikali na wanachi. Badae mambo yalikaa mwenye msitari na maisha yakasonga.

Sasa unambie; Serikali yako ya TOZO, Imefanyia kazi jambo lipi ilikuleta unafuu kwa wananchi?

Kila kitu kimepanda bei na mambo ni magumu mno kwa wananchi.
Ni nini cha pekee alichofanya Magufuli ambacho hakijawahi kufanyika huko nyuma?

Kama una akili na ufahamu na uwezo wa kufuatilia mambo, utagundua kuwa Magufuli alikuwa anaendesha siasa za uwongo kuwahadaa wajinga wamwone kuwa anafanya mambo makubwa sana ambayo hayajawahi kufanyika, wakati hakuna hata moja lililokuwa jipya
 
Back
Top Bottom