Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Nadhani kuna jambo halipo sawa. Maana naona hapo ewura ndio walitakiwa kupeleka research zao kwa waziri na kuonesha kwann wamekubali 8% na sio 18% . Au nchi hii hawaruhusiwi kutoa mapendekezo?? Maana ewura ndio katangaza ongezeko toka kwenye mapendekezo ya Tanesco
 
Nilitegemea Prof Muhongo atumbuliwe kwanza kisha wafuate wa chini yake.


Naona jamaa katolewa kafara
Hamna cha kafara wala nini...tulimpinga sana huyu mkurugenzi na EWURA juu ya kupandisha bei hawakusikia
 
..duh!

..tra alifukuza bodi akamuacha mkurugenzi mkuu.

..tanesco amefukuzwa mkurugenzi mkuu bodi ya wakurugenzi imeachwa.

..sasa tukisema nchi inaendeshwa kwa mihemko tutakuwa tumekosea?

..halafu anakwenda kuyazungumzia mambo haya
KANISANI!!

Yani akifuka Tanesco mkurugenzi
Lazima na TRA afukuze Mkurugenzi!!!
JokaKuu punguzeni Chuki
Haziwasaidii zaidi yakuumiza Nafsi yenu.
Kama Rais ndio huyo

Habadiliki kamwe
Mlie mtaka hakuwa
 
Ina maana kosa ni kuiomba EWURA kupandisha umeme?! Walisubiri EWURA wakubali ombi ndipo wamfukuze?! Sawa! Lakini Bukoba tunataka kusikia juu ya rambi rambi tu zilizoliwa na si habari ya Mramba. Ajenda za uchaguzi wa madiwani zinakosekana naamini mtawafukuza wengi mpaka ifikapo january 22.
 
Leo 1.1.2017 Prof. Muhongo amehojiwa na Radio One na kueleza sababu za kusitisha mpango wa EWURA wa kupandisha bei ya Umeme kwa 8.5% kama ifuatavyo: -
1. Kwenye mikutano ya 'public hearing' nchini kote wadau walipinga myongeza ya bei;
2. hadi jana 31.12.2017 EWURA, kinyume na matakwa ya sheria, haikuwa imepeleka ripoti ya uamuzi wake kwa waziri mwenye dhamana, kujadiliwa na kupitishwa/kuthibitishwa kabla ya kutangazwa kwa pendekezo la bei mpya;
3. Ufumbuzi wa matatizo ya kifedha (madeni) wa TANESCO hauwezi utatuliwa kwa kupandisha bei ya Umeme. TANESCO inatakiwa kuwa na mkakati wa ku-improve efficiency kwenye management yake badala ya kuongeza bei ya Umeme; na
4. Wakuu wa TANESCO hawawpaswi kulipana bonus kila mwisho wa mwaka kiasi cha kufikia Tzs. 60m/- kwa mtu mmoja wakati shirika linashindwa kujiendesha isipokuwa kwa kupandisha bei ya Umeme. Hii inamaanisha kuwa wananchi wakamuliwe ili ipatikane pesa ya mabosi wa TANESCO kulipana bonus! Prof. Muhongo amesema ameagiza hata hiyo bonus isilipwe au irudishwe kwa waliokwisha kulipwa.
Ndio maana tunasema kabla ya kufukuzwa bosi wa tanesco, bosi wa ewura anafanya nini hadi sasa?
Pia kumbuka hawa wametoa maombi tu, na ombi linaweza kukataliwa kwann haikufanyika hilo?
 
Dah Magufuli kumteua Mwinuka sijui kawaza nini? Kati ya sehemu ambazo hutakiwi kufanya majaribio ni Tanesco.. Kama ni kutafuta mtu pale UDSM basi Prof. Kimambo alikuwa anaweza sanaaa ila siyo Mwinuka!! Ila sasa ndo hivyo tena Kimambo anapitia Chalinze Mzee na huwa anakula pale Mombo.. humo hataki hata kuwasikia lakini Kimambo ni bonge la mbunifu!!
 
Huyu alikuwa mmoja wa watu waadilifu kwenye hii nchi. Na uchafu wa wakina muhongo nashangaa hawa watendaji wanawezaje kufanya kazi
Uko kinyume mkuu,hebu tujaribu kuunganisha hizi dots.
1. Sos alijiuzulu katika awamu ya nne,lakin ya tano akarudishwa wizara hiyo hiyo,,,kwanini???
2.JPM alilia sana mikataba ya tanesco,lakin ikawa ngumu kuivunja,,,wakati huo huo Mramba yupo wizarani,kwanini????
3.Ewura ilitangaza kupandisha gharama kwa 8.5%,,,SOS akakanusha haraka sana,,,kwanini???
4.Mramba katumbuliwa haraka sana,,,kwanini????

Mawazo yangu;
-Sos,alirudishwa wizarani kwa kaz maalum.
-Mramba alikuwa anavutiwa muda tuu.
-Tanesco inatakiwa kufa ili mikataba yake mibovu na wakina richmond ife.
 
Leo 1.1.2017 Prof. Muhongo amehojiwa na Radio One na kueleza sababu za kusitisha mpango wa EWURA wa kupandisha bei ya Umeme kwa 8.5% kama ifuatavyo: -
1. Kwenye mikutano ya 'public hearing' nchini kote wadau walipinga myongeza ya bei;
2. hadi jana 31.12.2017 EWURA, kinyume na matakwa ya sheria, haikuwa imepeleka ripoti ya uamuzi wake kwa waziri mwenye dhamana, kujadiliwa na kupitishwa/kuthibitishwa kabla ya kutangazwa kwa pendekezo la bei mpya;
3. Ufumbuzi wa matatizo ya kifedha (madeni) wa TANESCO hauwezi utatuliwa kwa kupandisha bei ya Umeme. TANESCO inatakiwa kuwa na mkakati wa ku-improve efficiency kwenye management yake badala ya kuongeza bei ya Umeme; na
4. Wakuu wa TANESCO hawawpaswi kulipana bonus kila mwisho wa mwaka kiasi cha kufikia Tzs. 60m/- kwa mtu mmoja wakati shirika linashindwa kujiendesha isipokuwa kwa kupandisha bei ya Umeme. Hii inamaanisha kuwa wananchi wakamuliwe ili ipatikane pesa ya mabosi wa TANESCO kulipana bonus! Prof. Muhongo amesema ameagiza hata hiyo bonus isilipwe au irudishwe kwa waliokwisha kulipwa.
Majibu mazuri sana, yafungulie thread mpya then waambie mods wasiifute au kuiunganisha na thread nyinginezo.
Na Title iandike kwa herufi kubwa ili wadau wa JamiiForums waione kirahisi.
 
4. Wakuu wa TANESCO hawawpaswi kulipana bonus kila mwisho wa mwaka kiasi cha kufikia Tzs. 60m/- kwa mtu mmoja wakati shirika linashindwa kujiendesha isipokuwa kwa kupandisha bei ya Umeme. Hii inamaanisha kuwa wananchi wakamuliwe ili ipatikane pesa ya mabosi wa TANESCO kulipana bonus! Prof. Muhongo amesema ameagiza hata hiyo bonus isilipwe au irudishwe kwa waliokwisha kulipwa.
Kwa lugha hii basi amelipiza kisasi kwa mramba maana hiyo ishu ya bonus tanesco walinyanganya na baadae wafanyakazi kwa kushirikiana na TUICO walipigania hiyo bomus kwasababu ipo kisheria. Kwa maelezo hayo bus mimi naona ni matazam finyu sana kwasabau analipwa, na bunus ni shilingi ngapi kwenye upanuzi wa miundo mbinu ya TANESCO
 
Kosa ndio hilo LA umeme watupishe na serikal yetu,huu sio wakati wa kuumiza wananchi.GOOD ENOUGH MY PRESIDA
 
Rais Magufuli leo ametengua rasmi uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini(TANESCO), Eng. Felchesmi Mramba.

Aidha Rais amemteua Dkt. Tito Esau Mwinuka kukaimu nafasi hiyo. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Mwinuka alikuwa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM).


Ili tuendelee tunahitaji watu,ardhi,siasa safi,uongozi bora na kutumbua
 
Hujitambui were
Ajenge yeye fundi!!?

Mmeishiwa hoja
Huyu ndiye Rais wakweli
Huwa siwezi kumwelimisha mtu mwenye upeo mdogo wa kufikiri kama wewe siku nyingine usiwe unajipendekeza unarept coment zangu.
 
wakuu unajua nawaonea huruma sana watanzania wajinga wasiojua haya mambo Tanesco, Baada ya Muongo kuingia aliondoa bonus ya wafanyakazi wa tanesco kinyume cha sheria. Lakini kwasababu wafanyakazi wa tanesco wanajitambua walipiga kelele waziri akabadilisha msimamo wake. Hapa katikati kuna makampuni yamezima mitambo yake kushinikiza tanesco kuwalipa fedha zao, Tanesco wameshindwa kuwalipa wazalishaji. Leo kwa lugha za kusema unawatetea masikini, unaua shirika la umeme. Ngojeni tusubiri, wawekezaji wanakataa kuwekeza kwenye sectoor hizi kwasababu ya tanesco kuchelewa kulipa leo unakuja unajifanya unawatetea wananchi while mmnaenda kinyume ya mikataba .......................let us wait
Mkuu wawekezaji wa kitapeli kama IPTL hata wazime mitambo yao hakuna shida maana wanatuibia fedha zetu nyingi kwa mikataba wao wa kitapel
 
Ila mbona jamaaa namuonaga anapiga kaz kisomi sana mramba ...ila duh hizi drama ...
Na wa ewura nae mbona kaachwa
Kisomi vipi mkuu fafanua basi kiduchu.

Unapandisha bei ya umeme kwa wananchi bila kumwambi rais wala makamu wake unategemea nini.

Huyu jamaa alishageuza Tanesco mali yake.
 
Back
Top Bottom