Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Najua hilo ila niliona ujio wa gesi utaongeza uzalishaji wa umeme hivyo umeme wa maji ungeshuka kidogo badala yake wanapandisha
gift, acha kusikiliza kauli za wanasiasa!haya mambo ni ya kitaalamu sana. Kuchimba gesi baharini ni ghali usiombe. Anayewekeza huko kurudisha hela zake lazima gesi iuzwe gari and hence umeme. Mnadanganywa tu. I have been in Norway, Sweden where Statoil (Norway) is situated! Nimeongea na wao kama marafiki tu, sio kazi rahisi
 
"Wananchi wanyonge, walioumbwa kwa mfano wa Mungu".
Wananchi ambao sio "wanyonge" wao wameumbwa kwa mfano wa nani?
Hivi "wanyonge" nchi hii ni nani? Wako wapi? Unyonge wao umesababishwa na nani/nini? Hivi ni kweli baada ya miaka 55 ya uhuru bado tuna Tanzania ya "wanyonge"walioumbwa kwa mfano wa Mungu?
Hiyo ndio kauli mbiu yetu kwa sasa, tunawalinda "wanyonge walioumbwa kwa mfano wa Mungu"; wanaowanyanyasa wameumbwa kwa mfano wa shetani, ni kuwatumbua tu, hakuna namna nyingine!
 
Ila kuna jambo hapa ambalo sijaelewa... naomba wajuvi wanijuze! Hivi unachomoa vipi Mwalimu wa Chuo kuwa Managing Director wa shirika lenye changamoto lukuki?! Hivi PhD inaweza ku-solve changamoto za TANESCO pasipo na kuwa na uelewa kwa mapana na marefu ya changamoto za TANESCO na energy sector kwa ujumla?! Au Mheshimiwa Daktari alitokea private/public commercial sector kabla hajawa Mhadhiri?
Kweli kabisa. Na hili ndo linatokea ATCL. Japo MD wake siyo phd lakini kwa vile ni wa kuokotwa mambo hayaendi
 
Serekali inawasiliana kwa nyaraka...madokezo...paper trail sio kujitangazia tangazia
Unaweza kutoa flow ya how things need to be done kabla ya kutangaza bei mpya ya umeme?! Usiongee kwa maneno bali with reference manake EWURA wamesema wazi kwamba:
EWURA2.png

Hao sasa, wanadai walifuata taratibu kwa mujibu wa sheria na kanuni hizo hapo juu! Which means; kama taratibu hazikufuatwa; ina maana EWURA nao hawakufuata sheria na kwa kiburi tu wakapokea maombi ambayo hayakufuata utaratibu na hatimae kuidhinisha kupanda umeme wakati taratibu hazikufuatwa!!!

Kwanini basi serikali hawakuanza na hawa waliodhinisha upandaji wa bei ya umeme wakati serikali haijaarifiwa? Au hiyo EWURA ina mamlaka nyingine juu yake?!
 
nadhani kuna la ziada hapo maana kuna wahauri wanampotosha kiongozi wetu mbona wa ewura kaachwa????y mramba ???
Hapa naona kuna kitu, hata ingekuwa mimi ningependa shirika ninaloliendesha lipate faida kubwa! Lazima nilete mapendekezo ya kupandisha bei! Ila pia kuna mdhibiti anahakiki! Sasa Huyu Mramba kosa lake ni nini? Mimi sioni mdhibiti kakubali sasa ndio mwenye proposal ahukumiwe?
 
Kama mtu anamkamua mwananchi maskini mvuja jasho ili kujilipa bonus ya mamilioni kwa mwaka, sina huruma na mtu huyo bila kujali ametokea kusini au kaskazini. Koo za mafisadi zikalime kahawa zile jasho la halali kama tufanyavyo siye.
 
Mwaga uali wa Escrow.Bado gavana Ndulu zama mpya na mambo mapya timua wote hata watendaji wa kata.
 
gift, acha kusikiliza kauli za wanasiasa!haya mambo ni ya kitaalamu sana. Kuchimba gesi baharini ni ghali usiombe. Anayewekeza huko kurudisha hela zake lazima gesi iuzwe gari and hence umeme. Mnadanganywa tu. I have been in Norway, Sweden where Statoil (Norway) is situated! Nimeongea na wao kama marafiki tu, sio kazi rahisi
Mkuu kwa akili ya kawaida hata mtoto wa darasa la saba anaelewa kuchukua hiyo kitu baharini sio kitu kidogo teknolojia ya juu inahitajika.

Ila sioni sababu ya tanesko kupandisha umeme labda waseme wanashindwa kucontrol umeme wao wajanja wanaiba hivyo wanaingia hasara.

Ukishindwa kucontrol kinachotoka basii hata kinachoingia hutaweza. kuna sehemu nimeishi mambo yanafanywa bwana sio mchezo. sababu ya tanesko kupata bhasara ni kuibiwa umeme hivyo ni uzembe wao wala sioni sababu ya kupandisha bei bali walinde nishati yao isiibiwe na wezi
 
Hapa naona kuna kitu, hata ingekuwa mimi ningependa shirika ninaloliendesha lipate faida kubwa! Lazima nilete mapendekezo ya kupandisha bei! Ila pia kuna mdhibiti anahakiki! Sasa Huyu Mramba kosa lake ni nini? Mimi sioni mdhibiti kakubali sasa ndio mwenye proposal ahukumiwe?
ndio maana nikasema kuna la ziada yaan mtu aliyetoa ruhusa kaachwa aliyetoa wazo katumbuliwa maajabu zaidi yatatokea!!
 
Vitu vidogo sana hivi ndugu yangu! Inawezekana Richard ni baba wa familia tena mwenye madaraka kwenye serikali ya JPM!

Trust me, watu wa aina hiyo hawawezi kuvumilia criticism!! Na ni social factor kamwe huwezi kuwalaumu!

Sasa hebu pata picha Kamanda IGP Ernest Mangu anaingia JF kwa jina la chige... hivi unadhani atavumilia criticism? THUBUTU...! Hata kama anajiita chige but still yeye ni Mangu; baba wa familia na Mkuu wa Jeshi la Polisi!!!

Kwahiyo hilo la kutoka nje mara moja moja wala lisikupe shida; msisitizo uwe ni kwenye kutovuka mipaka!!!!

Nimekupata mkuu, kama wewe ungekuwa Mangu namfahamu vizuri na ule undugu wake na Tundu Lissu.

Usikute vetting yake imepitia mezani kwangu.

Nimepiga sana biashara za ujasirimali Singida.

JF ni sebule ya majadiliano tuondoe personal issues.

😀😀😀
 
Mkuu kwa akili ya kawaida hata mtoto wa darasa la saba anaelewa kuchukua hiyo kitu baharini sio kitu kidogo teknolojia ya juu inahitajika.

Ila sioni sababu ya tanesko kupandisha umeme labda waseme wanashindwa kucontrol umeme wao wajanja wanaiba hivyo wanaingia hasara.

Ukishindwa kucontrol kinachotoka basii hata kinachoingia hutaweza. kuna sehemu nimeishi mambo yanafanywa bwana sio mchezo. sababu ya tanesko kupata bhasara ni kuibiwa umeme hivyo ni uzembe wao wala sioni sababu ya kupandisha bei bali walinde nishati yao isiibiwe na wezi
Tuna ushahidi thabiti kuwa umeme unaibiwa kwa kiwango unachokisema cha kuleta hasara kubwa hivyo? Au ni wanasiasa? Mimi umeme unaniathiri ukipanda, sitaki bei ipande, ila siungi mkono the way we make decision on such important issues, victimizing people.
 
Daaaah yani hakuna watu wanafiki dunia hii kama UKAWA,nyie watu pepo hamtaiona kwa unafiki na uzandiki ulivoawakaa,mmepiga kelele hapa jf tangu jpm aingie madarakani kuwa tanesco ni jipu,tulitangaziwa kupanda kwa gharama za umeme mkasema jpm hana la kufanya tanesco imemshinda,jana kamtumbua mkaskazini mwenzenu mmeanza kumdhihaki jpm na mmekuwa upande wa tanesco,kweli hii mitandao izimwe nyie nyumbu tuwasikie kwa sauti zenu halisi
 
Nakubaliana na wewe kwa huyu D. Mhaiki. Huyu Bwana ni Engineer mzuri sana, alianzia SCADA huko mpaka kafikia hapo alipo, analijua vyema shirika hilo. Asingehitaji mda wa kujifunza uendeshaji na terminologies wanazotumia ndani ya hilo shirika! Wenyewe wanasema; he would have hit the ground running! Hilo la udini na ukabila I'm better than that. It's not my area of interest!
Udini maybe but be sure ukabila is real.
 
Unaweza kutoa flow ya how things need to be done kabla ya kutangaza bei mpya ya umeme?! Usiongee kwa maneno bali with reference manake EWURA wamesema wazi kwamba:
View attachment 453211
Hao sasa, wanadai walifuata taratibu kwa mujibu wa sheria na kanuni hizo hapo juu! Which means; kama taratibu hazikufuatwa; ina maana EWURA nao hawakufuata sheria na kwa kiburi tu wakapokea maombi ambayo hayakufuata utaratibu na hatimae kuidhinisha kupanda umeme wakati taratibu hazikufuatwa!!!

Kwanini basi serikali hawakuanza na hawa waliodhinisha upandaji wa bei ya umeme wakati serikali haijaarifiwa? Au hiyo EWURA ina mamlaka nyingine juu yake?!

Mkuu, EURA walitakiwa warudishe maombi hayo ya Tanesco mpaka ufafanuzi na makubalino na waziri Muhongo yatakapotokea.

Mramba alipaswa kumshauri waziri (ambae tayari walikuwa hawaivi kutokana na kauli yake kule bungeni kuhusu ufanisi mbovu wa Tanesco)

Hivyo utaratibu ni EWURA kurudisha maombi kwa Tanesco na kuwashauri wamwone waziri ambae ana mamlaka kisheria na kikatiba kuangalia hizo bei ya umeme na kutoa maamuzi ya mwisho.

Mtizamo wako wewe juu la hili ukoje?
 
argument ya msingi kuhusu kutenguliwa kwa Mramba ni kwamba hawakufuate procedure..
Hii sababu inaonekana siyo ya kweli maana kama sababu ni hiyo, board na mkurugenzi wa EWURA walistahili kuwa wa kwanza kuhojiwa.

Huenda sababu ya kufukuzwa kwake ni kulipana bonus lakini hata hiyo sidhani anayelipwa ni pekee yake. Kwa nini board iliyoidhinisha isiwe mhusika mkuu wa kwanza?
 
belive m ukinunua umeme wa buku unapata uniti 2.9 vat n kama 180 na points, kacm kangu hakawez ku2pia picha. ko 800 tugawe kwa unit 2.9 tutapata bei ya unit 1
 
Back
Top Bottom