Magufuli - Katika mataifa ya Afrika, Kenya ndiye mwekezaji mkubwa Tanzania

Magufuli - Katika mataifa ya Afrika, Kenya ndiye mwekezaji mkubwa Tanzania

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Haya ameyasema rais Magufuli kwenye hotuba yake ambapo amesoma takwimu za uwekezaji wa Wakenya Tanzania. Amesisitiza umuhimu wa kudumisha undugu na kuendeleza ushirikiano kwa hali zote.
Akatoa mifano ya makabila ambayo yapo Kenya na Tanzania, wakiwemo Wajaluo na Wamaasai jinsi wanavyoishi bila kuchoreana mipaka hii ya mzungu.

Kuna mengi waliyokubaliana na rais Uhuru hususan kuhusiana na shughuli za baina ya nchi zote mbili, na wakaamrisha mawaziri husika kuratibisha kabla mwaka huu haujaisha. Watakutana Tanzania na kuanza mikakati ya kuboresha makubaliano yao.

Rais Magufuli amekaribishwa kirasmi na kupigiwa mizinga 21 ya heshima. Hii hapa video ya hotuba yake.

 
Hongera zenu wakenya. Je mmewekeza nini huku? Isijeikawa anawapa bichwa nyinyi hamjui.
 
geza hehehe ameanza kuhint kuomba msaada nlikuambia
Kupitia mitandao ya kijamii, kama wananchi, tunataarifiwa msafara wa rais wetu ulisimama ktk foleni, rais wetu akatoa maamuzi ya kutaka kutembea kwa mguu, sasa kama wananchi tunajiuliza
1. Suala la usalama na wanausala wa Kenya wanalichukuliaje kwa kiongozi mkubwa kama rais ambaye hupatikana kwa gharama kubwa kiuchumi?
2. Kwa kuzingatia sura ya matukio ya ugaidi yanayoikumba nchi yenu, je ni mpango mkakati gani ulikuwa unaendelea kwa msafara wa kiongozi wetu?
3. Licha ya tabia ya rais wetu kuwa na ziara za kushtukiza lkn kwa hili ilikuwa tofauti kwani taarifa mlizitoa wenye siku mbili kabla, je ni sehemu ya dharau kwa rais wetu?
Tafadhari, tungependa mtuoneshe upendo kama tunaowapa mkija kwetu.
 
Hadi leo haujui uwekezaji wa Wakenya huko. Basi utakua umefungiwa kijijini....
Yaani huoni Magufuli kawapiga changa la macho. Yaani uwekezaji wa 1.5 billions za unajisifia!!? Mbona pesa ndogo sana haifikii hata investment ya kampuni dogo kabisa la kibongo!!!

Ajira ya watu elfu 54. Yaani hata wauza ice cream wa azam hamuwafikii nchi. Huo ni uwekezaji mdogo sana. Na kuanzia leo msijisifu.
 
Haya ameyasema rais Magufuli kwenye hotuba yake ambapo amesoma takwimu za uwekezaji wa Wakenya Tanzania. Amesisitiza umuhimu wa kudumisha undugu na kuendeleza ushirikiano kwa hali zote.
Akatoa mifano ya makabila ambayo yapo Kenya na Tanzania, wakiwemo Wajaluo na Wamaasai jinsi wanavyoishi bila kuchoreana mipaka hii ya mzungu.

Kuna mengi waliyokubaliana na rais Uhuru hususan kuhusiana na shughuli za baina ya nchi zote mbili, na wakaamrisha mawaziri husika kuratibisha kabla mwaka huu haujaisha. Watakutana Tanzania na kuanza mikakati ya kuboresha makubaliano yao.

Rais Magufuli amekaribishwa kirasmi na kupigiwa mizinga 21 ya heshima. Hii hapa video ya hotuba yake.




Psiiiiii! Kuna watu watakufa kihoro na roho mbaya wakiskia hivi, sasa hivi watoto wa fisadi Lowasa na Mbowe wanaendeleza propaganda kwamba Magufuli wetu kadhihakiwa na Wakenya!
 
Kupitia mitandao ya kijamii, kama wananchi, tunataarifiwa msafara wa rais wetu ulisimama ktk foleni, rais wetu akatoa maamuzi ya kutaka kutembea kwa mguu, sasa kama wananchi tunajiuliza
1. Suala la usalama na wanausala wa Kenya wanalichukuliaje kwa kiongozi mkubwa kama rais ambaye hupatikana kwa gharama kubwa kiuchumi?
2. Kwa kuzingatia sura ya matukio ya ugaidi yanayoikumba nchi yenu, je ni mpango mkakati gani ulikuwa unaendelea kwa msafara wa kiongozi wetu?
3. Licha ya tabia ya rais wetu kuwa na ziara za kushtukiza lkn kwa hili ilikuwa tofauti kwani taarifa mlizitoa wenye siku mbili kabla, je ni sehemu ya dharau kwa rais wetu?
Tafadhari, tungependa mtuoneshe upendo kama tunaowapa mkija kwetu.

Wacheni kukuza mambo, hebu leta ushahidi kwa picha kwamba Magufuli alikwama kwenye foleni. Kinachofahamika ni kwamba mwenyewe aliamua kutembea kwa miguu kutoka hotelini hadi alikozikwa mzee Kenyatta ambapo ni umbali wa kama mita 100 hivi ambazo hazihitaji msafara wa magari.

Sasa mkijipoteza ufahamu na kujadili mambo yasiokua na maana ilhali marais wamekutana na kujadili mengi ya muhimu kuhusu nchi zetu, mnadhihirisha mlivyo na matatizo. Kesho anazindua barabara, sasa sijui mtaandika nini hapo.
 
Yaani huoni Magufuli kawapiga changa la macho. Yaani uwekezaji wa 1.5 billions za tsh unajisifia!!? Mbona pesa ndogo sana haifikii hata investment ya kampuni dogo kabisa la kibongo!!!

Ajira ya watu elfu 54. Yaani hata wauza ice cream wa azam hamuwafikii nchi. Huo ni uwekezaji mdogo sana. Na kuanzia leo msijisifu.
Huwa napenda mtu mkweli...Anael wew ni wa arusha/kaskazini..usijifanye hujui pilikapilika za wakenya kanda hiyo na pia 1.5b sio ndogo ukilinganisha na sisi tulivyowekeza kenya. Tuna jambo la kujifunza kwani wenzetu wamethubutu na kuweza
 
Hapa Prezidaa kateleza, ktk Afrika anayeongoza kwa uwekezaji hapa Tz ni South Africa, au hii si nchi ya Afrika?
 
Huwa napenda mtu mkweli...Anael wew ni wa arusha/kaskazini..usijifanye hujui pilikapilika za wakenya kanda hiyo na pia 1.5b sio ndogo ukilinganisha na sisi tulivyowekeza kenya. Tuna jambo la kujifunza kwani wenzetu wamethubutu na kuweza
Ndugu 1.5b ni ndogo sana ukilinganisha na mali ghafi wanazochukua kwetu.
Unajua uchumi wa kenya umekamatwa % kubwa na wazungu. Na hilo ni swala la kihistoria.

Mapato ya vodacom ya mwezi ni zaidi ya 10b. Sasa nchi nzima ya kenya kuwekeza 1.5b ni pesa ndogo sana zaidi ya kuiba mali ghafi.
 
Wacheni kukuza mambo, hebu leta ushahidi kwa picha kwamba Magufuli alikwama kwenye foleni. Kinachofahamika ni kwamba mwenyewe aliamua kutembea kwa miguu kutoka hotelini hadi alikozikwa mzee Kenyatta ambapo ni umbali wa kama mita 100 hivi ambazo hazihitaji msafara wa magari.

Sasa mkijipoteza ufahamu na kujadili mambo yasiokua na maana ilhali marais wamekutana na kujadili mengi ya muhimu kuhusu nchi zetu, mnadhihirisha mlivyo na matatizo. Kesho anazindua barabara, sasa sijui mtaandika nini hapo.
Mbona wewe hujaleta ushahidi alivyotembea kwa mguu kutokea hotelini?
 
Ndugu 1.5b ni ndogo sana ukilinganisha na mali ghafi wanazochukua kwetu.
Unajua uchumi wa kenya umekamatwa % kubwa na wazungu. Na hilo ni swala la kihistoria.

Mapato ya vodacom ya mwezi ni zaidi ya 10b. Sasa nchi nzima ya kenya kuwekeza 1.5b ni pesa ndogo sana zaidi ya kuiba mali ghafi.



get this straight

529 kenya comapanies
investment of $ 1.7 billion sio fedha za tz ni us dollars. kama ulienda shule kafanya hesabu.
employed 56, 290 tanzanians.
 
Wacheni kukuza mambo, hebu leta ushahidi kwa picha kwamba Magufuli alikwama kwenye foleni. Kinachofahamika ni kwamba mwenyewe aliamua kutembea kwa miguu kutoka hotelini hadi alikozikwa mzee Kenyatta ambapo ni umbali wa kama mita 100 hivi ambazo hazihitaji msafara wa magari.

Sasa mkijipoteza ufahamu na kujadili mambo yasiokua na maana ilhali marais wamekutana na kujadili mengi ya muhimu kuhusu nchi zetu, mnadhihirisha mlivyo na matatizo. Kesho anazindua barabara, sasa sijui mtaandika nini hapo.
Kiongozi acha majibu yenye mihemko, rejea hoja yangu na chanzo cha taarifa, kuwa tumepata kupitia mitandao ya kijamii,... Ilitosha kusema si kweli Bali uharisia ni moja, mbili na tatu, kuliko kuanza kutoa majibu yenye mtazamo hasi kwa watz wote, kimsingi, tunahaki ya kufuatilia kila kinachoendelea nawe unawajibu wa kukanusha kwa lugha ya staha pale unapoona pana chembe za upotoshaji.
 
Bwana yule si mtu wa mchezo kabisa,anaomba misaada hadi Kenya![emoji1]
 
Ndugu 1.5b ni ndogo sana ukilinganisha na mali ghafi wanazochukua kwetu.
Unajua uchumi wa kenya umekamatwa % kubwa na wazungu. Na hilo ni swala la kihistoria.

Mapato ya vodacom ya mwezi ni zaidi ya 10b. Sasa nchi nzima ya kenya kuwekeza 1.5b ni pesa ndogo sana zaidi ya kuiba mali ghafi.
$1.5 b ni Tshs 3 trillion. Najua hesabu kidogo imekupiga chenga lakini ningependa kukueleza kua kampuni za Tz zote pamoja haziwezi fikisha profit ya Tshs. 3 trillion.
 
Back
Top Bottom