Magufuli kutowalipa mshahara makocha Taifa Stars

Magufuli kutowalipa mshahara makocha Taifa Stars

Hio mada imepotoshwa.
Usahihi ni kwamba makocha wote wa Starz hulipwa na TFF isipokuwa Marcio Maximo ambapo kwa utashi wa JK kupenda mpira aliamua alipwe na serikali.
Na makocha waliowahi kuikochi starz tangu JK aingie madarakani ni Marcio Maximo, Jan Paulsen, Kim Paulsen, Mart Nooij na sasa ni Boniface Mkwassa. Ila ni Maximo ndiye aliyepata zali la kulipwa na serikali ya JK.
 
Safi sana Magufuli, akina malinzi walikuwa wanagawa na kocha hizi fedha
 
Serikali inalipa makocha wa timu ya Taifa na TFF majukumu yao ni yepi?
 
Nakubaliana na jpm anayempinga atuonyeshe mafanikio ya hao makocha toka serikali ianze kuwalipa karibu miaka kumi ya jk hata kombe la mbuzi hakuna.

Uamuzi sahihi
Jpm tuko pamojaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
TFF wanakusanya pesa nyingi sana hivyo walipe makocha kwa pesa zao. Serikali iwalipie makocha, TFF wakiboronga ati serikali haina nafasi ya kuwaingilia. Basi wajitegemee kwa kila kitu.
 
Hio mada imepotoshwa.
Usahihi ni kwamba makocha wote wa Starz hulipwa na TFF isipokuwa Marcio Maximo ambapo kwa utashi wa JK kupenda mpira aliamua alipwe na serikali.
Na makocha waliowahi kuikochi starz tangu JK aingie madarakani ni Marcio Maximo, Jan Paulsen, Kim Paulsen, Mart Nooij na sasa ni Boniface Mkwassa. Ila ni Maximo ndiye aliyepata zali la kulipwa na serikali ya JK.

wewe vp unapingana na ambao wapo juu serikalini, wao wamesema walikua wanalipa wewe unabisha?
 
Kila kitabu na zama zake JK alikuwa sahihi kwa wakati huo lakini timu linabutuliwa namna ile kuna haja gani ya kuendelea kutumia pesa za walipakodi kugharamia soka isiyo soka.
 
Mkwasa ana bahati mbaya,naona kambi za starz zitarudi tena jeshi la wokovu.
 
Habari kutoka gazeti la Mwananchi inasema kuwa makocha wa Taifa Stars watakuwa wanalipwa na TFF na wala sio serikali kwa kuwa hakuna ulazima wa wao kuendelea kulipwa na serikali badala ya TFF.

Ikumbukwe kuwa serikali ya awamu ya nne ilileta makocha wengi wa kigeni kuanzia Marcio Maximo na ilikuwa ikiwalipa mshahara

Muache Malinzi aisome NAMBA maana Mara baada ya JPM kuteuliwa na CCM alimualika kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kombe la kagame (Kujipendekeza)
 
Muache Malinzi aisome NAMBA maana Mara baada ya JPM kuteuliwa na CCM alimualika kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kombe la kagame (Kujipendekeza)

hahaaaaa kumbe unakumbukaeeee jamaaa alinoboa kichiz, alafu baade mashabiki wakaja kumzomea January makamba, kuona hivyo akapiga siasa marufuku michezoni, jamaaa boya kweli lile
 
sijaona kosa la Kikwete hapa. maana alikuwa na nia nzuri tu ya kuinua michezo nchini. kupeleka punda mtoni ni suala moja lakini punda huyo kunywa maji ni suala lingine kabisa. je, taifa stars ingechukua kombe la dunia/afrika kule brazili/west afrika ungeyaandika haya? ama kweli binaadam nio mtu.


Ninyi ndiyo mlikuwa mkimsifia JK kwa kuleta makocha na kuwalipa! Wabongo ni shida!
 
Back
Top Bottom