Magufuli, Museveni wakubaliana kuufufua mradi wa Bomba la Mafuta

Magufuli, Museveni wakubaliana kuufufua mradi wa Bomba la Mafuta

Jamaa wa TOTAL walishajitoa kitamboo na Museven hawezi chukua hela za ndani kugharamia huu mradi kama afanyavyo Magufuli kwa kuwadhulumu wafanyakazi na wawekezaji stahiki zao. Huu mradi ni kama haupo labda Magufuli ampe Museven hela za ujenzi wake

Museveni ni tapeli, kisha kakutana na Magufuli asiyemjua vizuri Museveni. Wakati huo mradi unazinduliwa kwa mbwembwe, nilijua ni utapeli kama utapeli mwingine. Nakumbuka utapeli uliokuwa unafanywa na ccm kusema ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda ni sehemu ya mafanikio ya Magufuli, kitu ambacho hakikuwa kweli.

Tanzania hatutoi hata senti moja kwenye huo mradi, sisi tunasaka fursa zitakazotokana na huo mradi. Kibaya zaidi tulishapigia hesabu faida itakayotokana na huo mradi. Ni kama tuliandaa kachumbari kisha ndio tukaenda kuwinda swala! Na Magufuli hapa alipo hana hata kumi ya kuwezesha chochote kwenye huo mradi. Kumbuka hapa nchini Magufuli ana miradi miwili inayohitaji 15t+, na hakuna mradi wowote kati ya hiyo imefikia hata robo. Ni wapi atapata hela ya kusaidia chochote kwenye hilo bomba? Ni wazi kuwa ni kupaka rangi upepo.
 
Huu ni mradi mwingine bogus kabisa na ninashauri tusitupe fedha zetu kwenye mradi huu. Biashara ya mafuta inakwenda kutoweka miaka 15 hadi 20 tu ijayo kutokana na kukua kwa kasi kwa biashara ya magari ya umeme duniani. Hadi sasa bei ya mafuta imekuwa ikiyumba sana na ndio maana mmeona mafuta yakishuka bei kila siku. Laiti mtu angesikia na kuelewa nachosema. Miaka 20 ijayo magari ya petrol na dizeli yatakuwa machache sana barabarani. Ukitaka kujua zaidi fuatilia mambo ya renewable energy na yanayojiri nchi zilizoendelea.
Hapo ume argu kama mtu wa dunia ya ngapi!!?
Maana hayo magari ya kawaida tu bado tunayahitaji kama miaka 50 huku dunia ya tatu. Hivyo rudi kwenye uhalisia wa Bariadi sio Washington
 
kwani kafuta yanatunika kwenye magari pekee?
Huu ni mradi mwingine bogus kabisa na ninashauri tusitupe fedha zetu kwenye mradi huu. Biashara ya mafuta inakwenda kutoweka miaka 15 hadi 20 tu ijayo kutokana na kukua kwa kasi kwa biashara ya magari ya umeme duniani. Hadi sasa bei ya mafuta imekuwa ikiyumba sana na ndio maana mmeona mafuta yakishuka bei kila siku. Laiti mtu angesikia na kuelewa nachosema. Miaka 20 ijayo magari ya petrol na dizeli yatakuwa machache sana barabarani. Ukitaka kujua zaidi fuatilia mambo ya renewable energy na yanayojiri nchi zilizoendelea.
 
Naona leo 13 September, 2020 ndiyo wanasaini mkataba Ku resume, kazi hii.

Sisi wananchi tunasubili ajira tulizohaidiwa
 
July 31, 2020

Rais John Magufuli na mwenzake wa Uganda, Yoweri Museveni wamekubaliana kurejesha kwenye Ikulu zao mchakato wa kutandaza bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki.

Bomba hilo linaloanzia Hoima, Uganda na kuishia Chongoleani, Tanga nchini Tanzania, limekwama baada ya kuwepo kwa “vizingiti” ndani ya serikali zao na hata wawekezaji katika mradi huo.

Wawekezaji katika mradi huo mkubwa wa kusafirisha mafuta, ni Total, Tullow na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya China.

Chanzo: Magufuli, Museveni wakubaliana kuufufua mradi wa Bomba la Mafuta
Huu mradi ulikuwa umekufa kabla haukuwa umeanza?Kile kilichofanyika pale Chongoliani kilikuwa nini?Hivi Chato pia ni Ikulu ya nchi hii?Mradi wa kitaifa unahuishwa katika makazi binafsi ya Rais wetu?
 
Back
Top Bottom