Mahad Nur: Msomalia Wa City Mall na Victoria Plaza, Vijana wa Kitanzania tuko wapi?

Tembea maeneo yote ya starehe alafu angalia wasomali utawakuta wangapi baada ya hapo ndio utapata jibu kwa nini hawa watu wanatusua kuliko sisi!
Starehe ni sehemu ya maisha ya binadamu aliyefanikiwa kiuchumi &kiroho .....

.... km hufanyi starehe yoyote means umefanikiwa kiuchumi tu , kiroho bado ni fukara/masikini kupita kiasi + your life is meaningless.
 

Ni kweli kabisa unavyosema kwani dunia nzima na kila nchi ukiangalia matajiri wakubwa ni foreigners
Kwani zaidi ya biashara hawawezi kupasua
Ukiangalia foreigner hawezi kuja na kutafuta kazi serikalini au kuingia siasa maana inakuwa ngumu sana ku integrate
Lakini akipika chakula chao na kuuza lazima mtakipenda kwani hamkijui na ni kipya kwenu

Pia biashara wanaona opportunities nyingi ambazo wazawa hawazioni au hazipo kabisa na wao wanazianzisha

Kingine wengi wanajipa misaada ya hali na mali na wanakuwa na communities zao za kupanga mikakati ya kibiashara
 
Starehe ni sehemu ya maisha ya binadamu aliyefanikiwa kiuchumi &kiroho .....

.... km hufanyi starehe yoyote means umefanikiwa kiuchumi tu , kiroho bado ni fukara/masikini kupita kiasi + your life is meaningless.
Inategemea ni Starehe zipi! Ninazozungumzia mimi ni hizi Starehe za Kipuuzi.
 
Uyo Mahad ana kaka yake anaitwa Mohamed Nur aligombèa uraisi uko somalia na ànaishi hapa TZ amewekeza hapa ana kampun yaķe pale Airport cargö terminal. Hawa jamaa wanaspirit na asīli ingawa nchi yao haieleweki
 
Waswahili hamkosi sababu, Wasomali Kokote waliko na utakapowakuta ni wapiganaji.. kama ulikuwa hujui hata Europe na USA hadi Canada Wanakimbiza sana kwenye Biashara
Nmekaa nao Sana ndola
Mm nawajua in & out
Magumashi kwao lazima
Huko kote uliposema huwezi ona huasilia wao...
Ila nawasifu kwa kupeana michongo wao kwa wao

Ova
 
Network
Network
Network
Hawa jamaa wana network kali saana
msomali wa ilala leo ana network ya wasomali wenzie wa nje zaidi ya nchi 20 so wana Import BUSINESS IDEAS always money comes from ideas and experience
tofauti na mswahili wa kisukuma ana wivu kuvunjia wenzake nyumba na kutaka waishi kama mashetani
 

Masikini nao wanamaneno ya kujifariji ili waonekane wema ndio maana hawajawa matajiri. Basi imani yao wanawaambukiza na wengine ndio maana idadi ya masikni ni wengi.
 
Mtaji baba.
Unajua US walipo saidia kumpindua Rais wa Somalia Siad Barre,Uongozi uliparaganyika kwani utawala mpya haukutilia maanani baadhi ya clans kwenye uongozi. Rais Barre katika uongozi wake alihakikisha umuhimu wa kila clan unatiliwa maanani. Somalia bila kuzingatia hili nchi hiyo haitawaliki. Matokeo yake iligubikwa na ugomvi mkubwa kati ya hizi clans na kuanza kupigana wenyewe kwa wenyewe.
Matokeo hayo yalisababisha wasomali wengi wenye uwezo kukimbilia ulaya pamoja na familia zao kama wakimbizi. Watoto wa wakimbizi hao ambao wamepata elimu nzuri tu walijaribu kurudi nyumbani na kuwekeza lakini hali ya usalama iliwakimbiza.
Wenzetu hawa wana clan system kama wahindi ambapo wanasaidiana sana kupitia mfumo wa hawala ambapo mtu anasaidiwa mtaji na clan nzima ambapo baadaye kulipa naye inabidi asaidie wenzake kwenye clan yao kimtaji.
Baadhi ya clan, zilifaidika sana na ndugu zao walio somalia waliokuwa wanapata pesa nyingi baada ya kuteka meli za mafuta na mizigo kwenye pwani yao. Pesa hizi pia zilizunguka kwenye mtindo huo. Siri ya kuendelea ni kusaidia wengine kwenye clan popote pale walipo.
 
Katika maisha ya sasa jitahidi uwe wa mwisho kuamini. Kwani hata dunia imebaki kipande, there is a secret of unknown.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…