Mahakama imeamua. Je, ndo bandari yetu imekwenda, unasemaje?

Mahakama imeamua. Je, ndo bandari yetu imekwenda, unasemaje?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
1692143845213.png

Bila ushabiki. Kama ungeulizwa nini ushauri wako kwa mama kuhusiana mzozo wa bandari ambao mahakama kuu ilitolea uamuzi? Je, unashauri tuendelee hivi au tukate rufaa?

Je, akili na nguvu vinavyotumika kuhakikisha hii kitu inafanikiwa zinaonyesha maanguko au mafanikio huko tuendako hasa ikizingatiwa kuwa, kama taifa, tuna uzoefu mbaya na mikataba kama tutajikumbusha tulivyopigwa kwenye karibu mikataba yote iliyoingiwa baada ya Mwalimu Kambarage kuachia ngazi?

Ngoja Baba yenu nianze kumpasha mama yenu. Bi Mkubwa, kwa mwendo huu hatufiki. Kumbuka. Maulaji yana mwisho. Wakati mwingine ukiupiga mwingi, mwisho unaweza kuwa shubiri. Chonde chonde, mama punguza spiidi. Wasikilize hawa wenye nchi uliyopata baada ya waliyemchgua hata kama ni kwa kuchakachua kurudisha namba.

Je, nani hatakufa? Wayajua ya kesho? Waachie wenye bandari waamue badala ya kuwabambikizia maamuzi hata kesi binti yangu.

Sema na mama. Mwambie kupitia uzi huu unachotaka kumwambia mama bila woga wala kumung'unya maneno.
 
We! Umeharibu toka mwanzo, hakuna la kujjadiri hapo, uhalishe mwenyewe halafu utuuambie sisi tukuchambe ebo!
 
Bandari bye bye

Waangalie kingine pia wakibinafsishe

Nashauri,mlima,kilimanjaro wapewe wawekezaji wausimamie au mnasemaje

Ova
Ivi ile mwendokas hatuwezi kumpa DPW?
 
Bado Kuna ATC
MWENDO KASI
VYUO VIKUU
MBUGA ZA WANYAMA
FERI ZOTE
TANROADS
BOT
DAWASCO
vyote hivi vinahitaji wawekezaji.
 
We! Umeharibu toka mwanzo,hakuna la kujjadiri hapo,uhalishe mwenyewe halafu utuuambie sisi tukuchambe ebo!
Mwanangu kuwa na hekima. Umeona mchangiaji wa kwanza allivyonisuta bila kusoma between the lines kama wewe. Nisipofanya nilivyofanya nitaonekana mchochezi wa kawaida. Soma vizuri na utafakari kijana wangu nakuomba chonde chonde
 
Bila ushabiki. Kama ungeulizwa nini ushauri wako kwa mama kuhusiana mzozo wa bandari ambao mahakama kuu ilitolea uamuzi? Je, unashauri tuendelee hivi au tukate rufaa?
Watanzania wanahitaji kuelimishwa kuhusu IGA na HGA, uamuzi wa Mahakama ni kuruhusu IGA iendelee ili twende kwenye HGA. IGA ni makubaliano tuu na sio mkataba, HGA ndio mkataba, hakuna haja ya kukata rufaa, nilishauri Mwenye dada hakosi shemeji, IGA ni posa tu. Je, tuendelee kupiga kelele kuzozania posa, au tutulie tupange Mahari ya maana kwenye HGA?
Je, akili na nguvu vinavyotumika kuhakikisha hii kitu inafanikiwa zinaonyesha maanguko au mafanikio huko tuendako hasa ikizingatiwa kuwa, kama taifa, tuna uzoefu mbaya na mikataba kama tutajikumbusha tulivyopigwa kwenye karibu mikataba yote iliyoingiwa baada ya Mwalimu Kambarage kuachia ngazi?
Kwanza sii kweli ni tumepigwa kwenye mikataba yote baada ya Mwalimu, japo mingi tumepigwa ila pia, iko mingine mingi tuu na sisi tumefaidika, kula uliwe!.
Ngoja Baba yenu nianze kumpasha mama yenu. Bi Mkubwa, kwa mwendo huu hatufiki.
Tutafika tuu, IGA ni barua tuu ya posa, mahari ni HGA itakuwa nzuri!.
Je, nani hatakufa? Wayajua ya kesho?
Wajameni, maneno mengine tunayotumia, ni maneno mazito sana!. Tusitumie maneno mazito sana kama haya, maana kauli nyingine sio kauli tuu bali ni kauli umba! "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia
Waachie wenye bandari waamue badala ya kuwabambikizia maamuzi hata kesi binti yangu.
Naunga mkono hoja
P
 
Rudisha Nyara ya Taifa.
Ngorongoro na Serengeti haikuwatosha?

Watanzania hawajaridhika na uwekezaji wa bandari, serikali isione aibu kuachana nao​

 
View attachment 2718519

Bila ushabiki. Kama ungeulizwa nini ushauri wako kwa mama kuhusiana mzozo wa bandari ambao mahakama kuu ilitolea uamuzi? Je, unashauri tuendelee hivi au tukate rufaa?

Je, akili na nguvu vinavyotumika kuhakikisha hii kitu inafanikiwa zinaonyesha maanguko au mafanikio huko tuendako hasa ikizingatiwa kuwa, kama taifa, tuna uzoefu mbaya na mikataba kama tutajikumbusha tulivyopigwa kwenye karibu mikataba yote iliyoingiwa baada ya Mwalimu Kambarage kuachia ngazi?

Ngoja Baba yenu nianze kumpasha mama yenu. Bi Mkubwa, kwa mwendo huu hatufiki. Kumbuka. Maulaji yana mwisho. Wakati mwingine ukiupiga mwingi, mwisho unaweza kuwa shubiri. Chonde chonde, mama punguza spiidi. Wasikilize hawa wenye nchi uliyopata baada ya waliyemchgua hata kama ni kwa kuchakachua kurudisha namba.

Je, nani hatakufa? Wayajua ya kesho? Waachie wenye bandari waamue badala ya kuwabambikizia maamuzi hata kesi binti yangu.

Sema na mama. Mwambie kupitia uzi huu unachotaka kumwambia mama bila woga wala kumung'unya maneno.
Asirudi nyuma
 
Watanzania wanahitaji kuelimishwa kuhusu IGA na HGA, uamuzi wa Mahakama ni kuruhusu IGA iendelee ili twende kwenye HGA. IGA ni makubaliano tuu na sio mkataba, HGA ndio mkataba, hakuna haja ya kukata rufaa, nilishauri Mwenye dada hakosi shemeji, IGA ni posa tu. Je, tuendelee kupiga kelele kuzozania posa, au tutulie tupange Mahari ya maana kwenye HGA?

Kwanza sii kweli ni tumepigwa kwenye mikataba yote baada ya Mwalimu, japo mingi tumepigwa ila pia, iko mingine mingi tuu na sisi tumefaidika, kula uliwe!.

Tutafika tuu, IGA ni barua tuu ya posa, mahari ni HGA itakuwa nzuri!.

maneno mazito haya!.
P
Wakati mwingine tunalazimishwa kuyasema hata kama hayapendezi ila inabidi tuyaseme japo wahusika waelewe kuwa nasi tuna akili na hisia mbali na haki juu ya kile tunachoongelea. Rais si Malaika wala mwanafalsafa bali mtu wa kawaida tuliyemuamini madaraka iwe kwa kumchagua au kwa zali la mentali kama ilivyo kwa mama yenu
 
Wakati mwingine tunalazimishwa kuyasema hata kama hayapendezi ila inabidi tuyaseme japo wahusika waelewe kuwa nasi tuna akili na hisia mbali na haki juu ya kile tunachoongelea.
Naunga mkono hoja ila tusitumie maneno makali sana!, kwasababu baadhi ya kauli za baadhi ya watu, sio kauli tuu kama kauli, bali ni kauli umba!, unalisema tuu jambo, linatokea!. "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia
Rais si Malaika wala mwanafalsafa bali mtu wa kawaida
Naunga mkono hoja na hili tumelisema Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda
tuliyemuamini madaraka iwe kwa kumchagua au kwa zali la mentali
Vyovyote iwavyo, ndio mpango wa Mungu, yeye ndiye mpangaji, Samia Mpango wa Mungu kwa Tanzania: Kwa Hili, Atabarikiwa!, Taifa Litabarikiwa!. Asante Mungu kwa Samia, Mungu Mbariki Samia, Mungu Ibariki Tanzania
kama ilivyo kwa mama yenu
Hili neno lako la mwisho, halijakaa poa!. Anayeweza kusema hivyo ni jirani tuu au mtu baki, lakini kwa Mtanzania, huyu ni Mama yetu wote, umkubali, usimkubali, Mama yako ni Mama yako tuu!, na Mama yetu ni Mama yetu wote!.
Hapa ninamaanisha mtu akiishakuwa ni rais wako, ni rais wa Watanzania wote popote walipo regardless wewe uko wapi, hivyo huwezi kusema rais wenu, ni rais wetu!.

NB. Hapa silazimishi watu wote kumpenda na kumkubali, that is a choice, lakini kumheshimu ni wajibu! Heshima kitu cha bure! Kwanini Rais Samia, japo sio lazima apendwe na wote lakini ni lazima aheshimiwe na wote? Akosolewe kwa staha na asitukanwe!
P
 
Watanzania wanahitaji kuelimishwa kuhusu IGA na HGA, uamuzi wa Mahakama ni kuruhusu IGA iendelee ili twende kwenye HGA. IGA ni makubaliano tuu na sio mkataba, HGA ndio mkataba, hakuna haja ya kukata rufaa, nilishauri Mwenye dada hakosi shemeji, IGA ni posa tu. Je, tuendelee kupiga kelele kuzozania posa, au tutulie tupange Mahari ya maana kwenye HGA?

Kwanza sii kweli ni tumepigwa kwenye mikataba yote baada ya Mwalimu, japo mingi tumepigwa ila pia, iko mingine mingi tuu na sisi tumefaidika, kula uliwe!.

Tutafika tuu, IGA ni barua tuu ya posa, mahari ni HGA itakuwa nzuri!.

Wajameni, maneno mengine tunayotumia, ni maneno mazito sana!. Tusitumie maneno mazito sana kama haya, maana kauli nyingine sio kauli tuu bali ni kauli umba! "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia

Naunga mkono hoja
P
Juzi TU ,umeshawazidi na akina prof shivji
 
Bandari bye bye

Waangalie kingine pia wakibinafsishe

Nashauri,mlima,kilimanjaro wapewe wawekezaji wausimamie au mnasemaje

Ova

Kabisa ,wabinafsishe ATC , TRC ,TRA ,MOF mapato yakiongezeka wachukue na MAGOGONI kabisa.
 

Bila ushabiki. Kama ungeulizwa nini ushauri wako kwa mama kuhusiana mzozo wa bandari ambao mahakama kuu ilitolea uamuzi? Je, unashauri tuendelee hivi au tukate rufaa?

Je, akili na nguvu vinavyotumika kuhakikisha hii kitu inafanikiwa zinaonyesha maanguko au mafanikio huko tuendako hasa ikizingatiwa kuwa, kama taifa, tuna uzoefu mbaya na mikataba kama tutajikumbusha tulivyopigwa kwenye karibu mikataba yote iliyoingiwa baada ya Mwalimu Kambarage kuachia ngazi?

Ngoja Baba yenu nianze kumpasha mama yenu. Bi Mkubwa, kwa mwendo huu hatufiki. Kumbuka. Maulaji yana mwisho. Wakati mwingine ukiupiga mwingi, mwisho unaweza kuwa shubiri. Chonde chonde, mama punguza spiidi. Wasikilize hawa wenye nchi uliyopata baada ya waliyemchgua hata kama ni kwa kuchakachua kurudisha namba.

Je, nani hatakufa? Wayajua ya kesho? Waachie wenye bandari waamue badala ya kuwabambikizia maamuzi hata kesi binti yangu.

Sema na mama. Mwambie kupitia uzi huu unachotaka kumwambia mama bila woga wala kumung'unya maneno.
WACHA IENDE Ukipinga utaungana na Dr.SLAA
 
La bandari halitaisha, samia hataweza kunyamazisha watu milioni 60
 
Back
Top Bottom