Mahakama kanda ya Arusha yakubali kupokea taarifa ya CCTV camera toka Benki ya CRDB kwenye kesi ya uhujumu Uchumi ya Ole Sabaya

Mahakama kanda ya Arusha yakubali kupokea taarifa ya CCTV camera toka Benki ya CRDB kwenye kesi ya uhujumu Uchumi ya Ole Sabaya

seedfarm

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2020
Posts
260
Reaction score
2,655
Mahakama kanda ya Arusha jumatano oktoba 27, 2021 imekubali kupokea kielelezo namba 4 kama ushahidi toka kwa Afisa tehema wa CRDB tawi la kwa Mrombo bwana Geoffrey Abimiel Nko ambaye ni shahidi namba saba wa Jamuhuri Katika kesi ya uhujumu Uchumi inayomkabili Lengai Ole Sabaya.

Francis Mrosso analalamika kuwa aliporwa pesa zake alizotoa toka Bank ya CRDB tawi la kwa Mrombo huku wasaidizi wa Sabaya walisubiri mzigo huo wa pesa hapo Bank.

Hakimu mkazi wa kanda ya Arusha Bwana Kisinda alipinga pingamiza lililoletwa na upande wa utetezi wa Sabaya kuwa halina mashiko, Ambapo wakili wa Sabaya aliomba mahakama taarifa ya CCTV isitumike mahakamani kwa kuwa haina ubora na inaonyesha picha hafifu.

CCTV camera hiyo ilichukuliwa January 22 mwaka huu kuanzia 4:09 jioni mpaka saa 5:05 jioni ikionyesha Vijana wa Sabaya wakizikwapua pesa toka kwa Bwana Francis Mrosso hapo kwa Mrombo tawi la CRDB.
 
Yani sabaya na hao wapambe wake hawana akili kabisa... unafanyaje uporaji kama huo nje ya benki, mahali ambapo unajua kuna cctv cameras zinamulika wakati wote!!

Yale machozi aliyotoa mwenye msiba wa jiwe yalikuwa na sababu kubwa sana,
alijua kinga yake imeondoka na hakuna atakayemtetea kwenye haya maupuuzi yake aliyofanya....
 
binafsi mimi siwezi kuwa Mwanasheria.
ebu imejini wakili anatoa pingamiza la namna ilo mahakamani na anataka mahakama ili pokee!!!.
kuna hitaji akili za utoto na utu uzima kuwa wakili.
kila mtu ana talanta yake nashukru kutokuwa na hiyo talanta.
bila kuwaza kifala na kigirit thinka uwezi kuwa mwanasheria.
 
Hivi sabaya ilikuaje akaupata ukuu wa wilaya,naona mambo yake alikua anayafanya kishamba sana?
Huyo 7ya ni trela alomteua ndo muvi lenyewe lakutisha...stelingi kafa masaidizi yanaadhirika!!!
Tuendelee kuomba ili video za shambulio la lissu walizokwapua zivuje!! Mr. Wowowo naye atiwe nguvuni ale miaka 100 watu wajifunze
 
Yani sabaya na hao wapambe wake hawana akili kabisa... unafanyaje uporaji kama huo nje ya benki, mahali ambapo unajua kuna cctv cameras zinamulika wakati wote!!

Yale machozi aliyotoa mwenye msiba wa jiwe yalikuwa na sababu kubwa sana,
alijua kinga yake imeondoka na hakuna atakayemtetea kwenye haya maupuuzi yake aliyofanya....
Waswahili wanasema Bora Uibiwe na kupoteza Hirizi kuliko kufiwa na Mganga
 
Back
Top Bottom