Mahakama Kuu Dar, imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa dhidi ya Spika Ndugai kwa kumtambua Mwambe kama Mbunge baada ya Kujiuzulu

Jamaa alishatangaza kwamba hakuna mahakama yoyote inaweza kutengua uamuzi wake...

Chezea mbunge wa Kongwa wewe!! Utakufwa siku si zako... na bado nyie wana harakati mnachokitaka mnakwenda kukipata come October 2020.
 
Katiba ya JMT, ibara ya 67(1) vifungu(a)-(c)Nukuu(b)
(b) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika Ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge iwapo:
(b) Ni Mwanachama na ni mgombea aliye teuliwa na Chama cha siasa.


Cecil Mwambe alijiuzulu Uanachama toka CHADEMA na hivo kupoteza sifa ya kuwa Mbunge kwa mujibu wa kifungu hiki. Iweje Spika Ndugai amrejeshe Bungeni kwa kukiuka kifungu hichi kilicho ndani ya Katiba???​
 
Sikutegemea kitu tofauti na hicho.
tindo sometime Ebu ujitahidi kuweka ushabiki wako pembeni alafu ujadili hoja itakusaidia Sana hapo kafuta kesi na kakuambia vifungu alivyotumia kuamua hiyo kesi na isitoshe akatoa pia ushauri kwa mleta kesi namna alivyotakiwa afanye wewe ulitakiwa umjibu kwa hoja kwa kutumia vifungu vya sheria Kama alivyofanya yeye badala ya kutumia hisia zako binafsi hii ndio maana ya great thinker.
 
Ok noted and thanks

Wanasiasa wanapotezea watu muda wa kufanya kazi

Kila mtu apambane na hali yake

Liwe Bunge au Mwambe kila mtu anaangalia familia yake

Kwa ufupi wananchi angalieni maisha yenu
Tunaangalia maisha yetu ila kumbuka kuna nguvu zetu zinaenda serikalini kilisha watu waliotumwa kazi
 
Ukiacha kufuatikia chombo cha kukutungia sheria kinaendaje, hujaendelea na maisha yako.

Umeacha wengine wakuamulie maisha yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nafahamu umedhamiria kitu fulani,

Tanzania watu waoga na wanahofu sana kutumia nguvu ya uma kudai haki

Nimekuelewa vizuri sana ,Kwa hali ya sasa bora watu waendelee na Maisha yao

Wanasiasa wote ni ndumilakuwili

Angalia waliohama wote wameacha majeraha kwa vijana
 
Huyo wakili Kaunda achunguzwe uraia wake sio mtanzania huyo

Umenikumbusha jina la Baba wa Taifa la Zambia Mzee Kenneth Kaunda.
Very likely the Advocate crossed the border from Kitwe to Mbeya and pretends to be a Nyakyusa from Ileje...!!
 
Kwa hasira zako sasa hakuna atakae kusikiliza iwe Bunge,Serikali au Mahakama

Hivi mfano wewe ndio Jaji ungefanya nini kwenye kesi hii,

Heshimu anayekupa chakula
 
Hata mtoto wa Darasa la pili alijua aliyefungua kesi hana hoja, labda anatafuta kiki.
Alafu bado eti ni "mwanasheria", tuna safari ndefu.

Hoja alikuwa nayo ila ameshindwa kujenga hoja kuitetea. Hivo Technicalities kwa lugha za Kimahakama zime mtoa TKO!!!
 
Tunaangalia maisha yetu ila kumbuka kuna nguvu zetu zinaenda serikalini kilisha watu waliotumwa kazi
Serikali hata wewe ni sehemu ya serikali

Walimu,Wanafunzi,Wakulima,Askari,wote ni sehemu ya serikali

Majukumu ndio yanatofautisha majina
 
Kwa hasira zako sasa hakuna atakae kusikiliza iwe Bunge,Serikali au Mahakama

Hivi mfano wewe ndio Jaji ungefanya nini kwenye kesi hii,

Heshimu anayekupa chakula

Wewe zuzu kwelikweli! Pole sana.
Hivi hujamsikia Rais wako Jiwe akisema kuwa Serikali hainaga shamba?
Au mwenzetu unapewaga chakula cha bure?
 
Dunia inaenda kasi sana wawe makini wasichukulie mambo poa muda wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…