Mahakama Kuu imetupilia mbali pingamizi la Serikali dhidi ya Mwanaharakati wa tozo

Mahakama Kuu imetupilia mbali pingamizi la Serikali dhidi ya Mwanaharakati wa tozo

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Mahakama Kuu imetupilia mbali pingamizi la awali Serikali dhidi ya maombi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya kibali cha kufungua shauri la kupinga tozo kwenye miamala ya simu.

Hata hivyo wakati mahakama hiyo ikitupa pingamizi la Serikali, pia imeyatupa maombi kama hayo yaliyofunguliwa na Mwanaharakati Odero Charles Odero baada ya kukubaliana na hoja moja ya pingamizi la Serikali kuwa hati ya kiapo chake kilichokuwa kinaunga mkono maombi hayo ina kasoro za kisheria.

Uamuzi huo wa umetolewa leo Jumatano, Septemba 8,2021 na Jaji John Mgetta.

Akitoa uamuzi wa pingamizi la Serikali, Jaji Mgetta ametupilia mbali hoja zote tatu za Serikali akisema kuwa hazina mashiko.
 
Sasa kwanini huyo jaji hakuwafundisha serikali wafanye nini kama yule wa Mbowe? kwani hiyo kesi ya tozo haina interest kwa jamii?

Mambo ya hovyo ni ya hovyo tu, siasa zisiachwe kuingilia mambo ya taaluma ili muhimili wa mahakama uheshimiwe.
 
Safi kabisa jaji na tayari umetengeneza precedence. Hati ikiwa ina makosa ya kisheria haina maana makosa yanayoshtakiwa hayakutendeka, ina maana kesi haiwezi kuwa hai!! Kesi inaweza kufunguliwa upya.

Ili haki itendeke lazima ionekane kutendwa! Jaji umetoa mfano!
 
Sasa kwanini huyo jaji hakuwafundisha serikali wafanye nini kama yule wa Mbowe?...
Hii kesi walimwachia jaji aamue, wakati ya Mbowe alipewa mmoja wa maafisa wa wasiojulikana waliopenyezwa mahakamani kwa lengo la kuhakikisha Serikali inashinda kwa baadhi ya kesi, hasa zile za kuwaonea na kuwakomoa mahasimu wao.

Na yule msajili ni miongoni mwa maafisa wasiojulikana, anaamua kesi ipi ipelekwe kwa jaji na ipi kwa ofisa wa wasiojulikana.
 
Double standard za kimahakama hapa nchini,pingamizi limetupwa kisa lilikosa mshiko wa kisheria wa kiapo fair enough, kesi ya Mr.Mbowe mashitaka yote yalikosewa means hayana mshiko wa kisheria ila my lady aliamua kuwapa muda serikali wakarekebishe mashitaka!nchi bado sana tena sana.
 
Duh!! Mahakama siku hizi ni kupitezeana tu muda
 
Back
Top Bottom