Mahakama Kuu imewaruhusu Halima Mdee na wenzake 18 kufungua kesi ya kupinga CHADEMA kuwavua uanachama


Na hivyo ndio ishu ilipo
 

Chadema still haitambui uchaguzi uliopita,

I think now ilikuwa ni wakati mzuri sana kwao kupiga siasa mbadala, badala yake wamekosa hoja

Wapo kupambana na covid tu
 

Wakina Mdee hawajavunja sheria

Vile ni viti vya wanawake na wao wamekwenda ni wanawake
 
Unategemea Mnyika angekubali

..Mnyika hawezi kuwateua mwenyewe bila kupewa maelekezo na baraka za kikao cha kamati kuu.

..uwezekano mkubwa ni wamekwenda bungeni kwa MAAGIZO / MAELEKEZO na hawakuwa na nyaraka yoyote ile toka Chadema na Nec.
 
Amen
 
Ebu elezea na jinsi Mbowe na Mnyika walivyomtoa mahabusu Nusrat Hanje
usiku usiku na kumsafirisha toka Singida hadi Dodoma kwenda kuapishwa na Ndungai gereji.
Kwa nini unajitoa ufahamu?.
 
..Mnyika akizungumza toka viunga vya mahakama kuu.

 
Ngoja tuende kwenye kesi maana tume-miss yale maswali ya kibatala,mutobesya+malya ambapo majibu yaliwachanganya wenye kesi .......{Jaji naomba kwenda washroom}
 
Kama kweli wewe unao ushahidi huo, basi pamoja na kuchelewa peleka uwasaidie akina Mdee waachane na porojo za vijikesi kila uchwao.
 
..Mnyika akizungumza toka viunga vya mahakama kuu.

Mkuu JokaKuu

Katika club house moja Mwenyekiti Mbowe aliulizwa anakwendaje katika maridhiano wakati suala la COVID halijaisha?
Aliyeuliza swali alikuwa na maana moja, kwamba, huwezi kwenda kwenye meza ya mazungumzo bila ''bargaining chip''

Mbowe akajibu kwamba suala la COVID ni la kitaasisi na lihaitaji muda ili taratibu za kitaasisi zikamilishwe

Kauli hiyo ilinishtua sana kwasababu sikuitegemea kutoka kwake, sasa leo nashangaa Mnyika analalamika

Mnyika amuulize Mbowe huko kwenye meza ya maridhiano hili halimo?
 
Interesting. Kuna wakati mtu unashangaa tu vile CCM inavyohangaika kucheza shere na CHADEMA. Mara wanajipendekeza kwa Mbowe. Wanajipendekeza kwa kina Halima. Wamejipendekeza kwa Lissu. Wamezoa kina Lijualikali & co. What next?

Inawezekana ikitokea siku CHADEMA wakamtimua mtu mzito kama Lissu kwa kelele nyingi - kwa geresha tu, basi CCM watamkimbilia na ma-vieite na ofa kibao za cash, mijengo na post ya Waziri Mkuu au Naibu Waziri Mkuu!

Anyway, vyovyote vile wajue CHADEMA ni nguvu ya umma. Unaweza kuwanunua kina Mbowe, Halima, Lissu, Silinde, n.k. lakini hatimaye utakutana na people’s power pale pale na vile vile, whatever the name, whichever the faces.
 

..Nadhani Mbowe yuko sahihi.

..Naamini anamaanisha kuwa kina Halima walikwenda bungeni kwa MAAGIZO ya wakubwa serikalini.

..Kwa msingi huo wanatakiwa watolewe kwa mtindo uleule uliotumika kuwaingiza bungeni, yaani kwa MAAGIZO.

..Nadhani tatizo liko ktk namna ya kuwatoa bila kuziumbua mamlaka zilizowaingiza bungeni.

..Huo ndio MTIHANI alionao Ssh ktk kushughulikia mgogoro huu.

NB:

..Msiwaandame Mbowe na Mnyika wao wameshatimiza wajibu wao kwa kuwafuta uanachama kina Halima.
 
Hawa watakuwa wabunge mpaka 2025, tutake tusitake, hii ndo bongo..
 
Ndugu yangu elewa tu kina Mdee na wenzake wamefungua Id fake nyingi humu JF kwa ajili ya Psychological game. Hivyo ukute huyo unayemjibu ni Mh Buhala.
ID zote humu ni feki. Kwa nini Halima Mdee ndio aweke id yake ya ukweli?

Anyhow... mimi swali langu ni moja: ukipigiwa simu na Tume ya Uchaguzi au na Katibu wa Bunge au na Afisa Mawasiliano wa Ikulu ukaambiwa karipoti kesho Dodoma, umeteuliwa na chama chako au na Rais kuwa mbunge.

Utaondoka kuelekea Dodoma au utaanza kuhoji hicho kikao dondoo zake kasaini nani, nyinyi Tume nani kawapa taarifa, na huyo Rais alijadili huo uteuzi na washauri wake lini saa ngapi?
 
Kama ungeelewa vizuri maana ya neno taasisi kwenye hiyo kauli ya Mbowe naamini usingeshtuka.

Kwa maoni yangu sidhani kama Mbowe anaizungumzia taasisi ya Chadema kwenye hiyo kauli yake, kwani Chadema kwa upande wao walishamaliza kazi dhidi ya hao Covid.

Hapo naona Mbowe anaizungumzia taasisi ile inayowalinda hivi sasa, CCM. Hawa ndio waliwapeleka hao jamaa bungeni, na ndio wanatakiwa kuwaondoa.

Kutokana na vile wanavyowalinda toka enzi za Magufuli mpaka sasa kwa Samia ndio naielewa zaidi kauli ya Mbowe, hii issue huko kwao ni ya kitaasisi, haukuwa uamuzi wa mtu mmoja.

Japo kwa upande mwingine naona kwa Chadema kuendelea kuwasubiri CCM watoe hatma ya hao wanawake, ni sawa na kunyamazia uvunjifu wa sheria unaoendelea kuligubika hilo sakata la Covid.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…